IGP Sirro, Jinai huwa haifi! Kamata wote waliowahi kusema anayosema Askofu Gwajima

IGP Sirro, Jinai huwa haifi! Kamata wote waliowahi kusema anayosema Askofu Gwajima

Akili zako na askofu Rashidi zipo sawa kabisa tatzo lako hauna hela
Ni kweli Gwajima nampa big up sana kwenye hili swala. Kuhusu hela kawaulize wenzio. Mimi na Gwajima tunaweza kutofautiana hesabu tu,kama ilivyo kwa Mo hawezi kuwa sawa na Bakharesa.
 
Nimemsikia, kasema makosa ya Gwajima akiyarudia watamuita waziri wa mambo ya ndan...kwenye kamati. Swali namba moja, makosa ya Gwajima ni yapi? Si kukataa chanjo? Au

swali namba mbili logic ya kumuita waziri wa mambo ya ndan, maana yake kashindwa Kaz siyo?? Sasa huyo wazir yuko chini ya muhimili gan?

..Makosa ya Gwajima sio kukataa chanjo.

..Makosa ya Gwajima ni haya hapa:--

1. Viongozi wamehongwa ili watuletee chanjo.

2. Viongozi wamedungwa chanjo feki, na wananchi watadungwa chanjo yenyewe yenye madhara.

3. Chanjo zina magnetic chip inayoingia ktk mwili wa binadamu.

4. Chanjo zina nguvu ya umeme, pale ulipochanjwa ukiweka balbu inawaka.
 
Kwani kupinga chanjo ni jinai?
Haaahaaaa...kuchanjwa hata nchi zilizoendelea ni hiari. Marekani wanatoa dola 100 ukienda kuchanja. Kwanini iwe lazima kwetu? Mnajuaje nilishachanja kabla ya corona na ninadund poa tu? Mbona kufa kuko pale pale. Why Corona tumeipa special attention? Globalists at their best
 
Haaahaaaa...kuchanjwa hata nchi zilizoendelea ni hiari. Marekani wanatoa dola 100 ukienda kuchanja. Kwanini iwe lazima kwetu? Mnajuaje nilishachanja kabla ya corona na ninadund poa tu? Mbona kufa kuko pale pale. Why Corona tumeipa special attention? Globalists at their best
Marekani wanatoa dola 100 kwa sababu chanjo bado zipo kwenye majaribio.......huwezi kutumia watu kama panya wa majaribio bure bure tu....
 
Tumsifu Yesu Kristu IGP Simon Sirro!

IGP Sikufundishi kazi lakini naona kama unalazimishwa kumkamata Askofu Gwajima! Kwa maneno ya Mh Spika jana pale Bungeni ni kama alikerekwa na kauli yako yakutaka barua toka Wizara ya Afya ikionyesha jinai iliyofanywa na Askofu Gwajima, Spika amekushangaa kuwa jinai huioni?

Sasa IGP mi nakushauri tu, kwa mujibu wa sheria Jinai huwa haifi, record zote zipo za ao wapinga chanjo awamu 5 mi nakushauri wote kamata kaweke korokoni huko!
Anahitaji barua ya kibali cha kukamata

Sent from my Infinix X692 using JamiiForums mobile app
 
Anahitaji barua ya kibali cha kukamata

Sent from my Infinix X692 using JamiiForums mobile app
Yes ila si wanamshinikiza amkamate Askofu? Clip zipo wote waliowahi kuzungumza huko nyuma kupinga chanjo na wenyewe wakamatwe akiwemo waziri wa afya, maana kosa analotuhumiwa wapo waliowahi kulifanya huko nyuma.
 
Gwajima ni mchochezi na anaonyesha dharau kubwa kwa serikali ya awamu ya 6 .

Hakuna dini ya akina Gwajima na wanaofanana nao bila wazungu na Rumi na umagharibi.
Makristo wa aina ya Gwajima wapo kila mahali na wanawaaminisha watu kuwa wao wanajua kila kitu wakati sio kweli hata kidogo. Sio kwili kuwa Gajima anajua kila litu. Angekua anajua kila kitu angegundua hata dawa ya malaria. Malaria yapo Duniani tangu enzi ya mtume mpaka leo yapo Afrika na hakuna Mwafrika aliyegundua chanjo au dawa ya kuwamaliza mbu zaidi ya Neti zilizotengenezwa na Wakristo wa Ulaya na Mabudha wa China na India na waislam wa Misri. Hata hivyo hawamdharau mtu kuwa wao ndio majibu ya kila kitu bali wananyenyekea kwa Mungu ili azidi kuwapa maarifa wagundue zaidi.

Hivi gwajima anaweza hata kujenga Bwawa la umeme kwa miujiza ya kiroho ? Kamwe hawezi mana Mungu amempa kipaji chake kwa sehemu na vingine amewapa wengine ili Mungu abaki kuwa yeye ndiye mjuzi wa yote.
Gajima hawezi hata kutengeneza Dawa za Kisuna kama Ustadhi Mwaipopo.

Kifupi tu ni kuwa Hatutaruhusu Nyumba za ibada kuwa bunge la kutoa maamuzi ya serikali na kwa kuwamiliki watu na kupanga kwa lazima kuwa hapa wote hatuchanjwi.
No. Big not.
Waislam wakizungumza mambo yao misikitini yanayoingiliana na matamko ya serikali wanaitwa magaidi na kukamatwa mara moja ,why tusiheshimu wengine nao watoe ya kwao kwa kisingizio cha uhuru wa kuabudu.

Mbona waislama wana mambo mazuri na ya haki tena yapo mpaka kwenye biblia lakini wakiyajadili wanaitwa wachochezi ?
Mfano mahakama ya Kadhi, Kuoa mabinti chini ya miaka 18.
Kupinga suala la riba kwenye mabenki yenye mifumo ya kimagharibi.
Kupinga bima compressive kwenye mali.
Wanawake kuvaa nguo fupi zinazowatamanisha wanaume wa mitaani na kuhamasisha zinaa.
Kuoa na kuzaa bila ndoa.

Michepuko kila kona badala ya kuoa.
Kugawa mirathi kwa mifumo ya kimagharibi inayoitwa sheria za nchi ambazo ni kingume na dini zote.
Elimu ya kimagaharibi na mifumo yake ya kimagaharibi.
Yote hayo ni kinyume na Mitume na manabii na mila za mashariki ya kati na mila za kiafrika.

Wenzetu wanatulia ili kulinda amani lakini anaibuka mtu mmoja anataka kutumia dini kuhamasisha watu wapingane na serikali na kuwatisha kuwa watu watakufa na kuwa mazombi.
Kwa nini asiweke mikono yake juu ya hiyo dawa ya Chanjo na kuipa uponyaji kama wanavyoomvea maji ya upako ili sumu iliyoko ndani yake itoke na kugeuka kuwa uponyaji???

Gwajima atulie na kuheshimu wataalam wetu ambao kwa muda mrefu wamefanya mambo mazuri kwa kusomea huko Nje na kuja na utaalam na sasa wanapasua mpaka moyo na kuushona,wanapasua kichwa na uti wa mgongo kwa maarifa kutoka kwa Mungu aliyewapa kupitia Roho wake wa maarifa na Ufunuo wa Yesu Kristo.

Hua nikimsikiliza Gwajima na James Mbatia au Hashimu Rungwa napata jibu kuwa James Mbatia na Hashimu Rungwe ndio watumishi wa Mungu na manabii waliotumwa kuhubiri habari ya Haki na usawa na wema kwa wanadamu. Gwajima ni Mpiga debe wa CCM na mkabila na mbinafsi anayesaka mali za dunia.
 
Back
Top Bottom