IGP Wambura amuapisha kamishina Suzan Salome Kaganda

Idofu

Senior Member
Joined
Oct 24, 2022
Posts
116
Reaction score
199
CAPTION

Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Camillus Wambura, leo tarehe 28.10.2022 amemuapisha Kamishna wa Utawala na Rasilimali Watu CP Suzan Salome Kaganda baada ya kupandishwa cheo na kuteuliwa kuwa Kaimshna wa Utawala na Rasilimali Watu.

IGP Wambura amemuapisha kwa niaba ya Mhe, Rais na Amiri Jeshi Mkuu na hafla ya uapisho imefanyika katika Ofisi ya Mkuu wa Jeshi la Polisi, Makao Makuu ya Polisi Dodoma.

 
Tuna mtaka na Thiopister Mallya. Awe kamanda wa kikosi cha usalama barabarani. Wanaume mmezidi kula rushwa na kukiuka maadili ya kazi.
 
Salaam Wakuu,

Hatimaye yamekuwa. Kamishina wa Taifa kaapishwa. Sifa na utukufu kwa Mungu aliye juu🙏

Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Camillus Wambura, leo tarehe 28.10.2022 amemuapisha Kamishna wa Utawala na Rasilimali Watu CP Suzan Salome Kaganda baada ya kupandishwa cheo na kuteuliwa kuwa Kamishna wa Utawala na Rasilimali Watu.

IGP Wambura amemuapisha kwa niaba ya Mhe. Rais na Amiri Jeshi Mkuu na hafla ya uapisho imefanyika katika Ofisi ya Mkuu wa Jeshi la Polisi, Makao Makuu ya Polisi Dodoma.
 
Tuna mtaka na Thiopister Mallya. Awe kamanda wa kikosi cha usalama barabarani. Wanaume mmezidi kula rushwa na kukiuka maadili ya kazi.
Ni kweli kabisa rais ni Taasisi na hatumfundishi kazi wala kumshinikiza. Bali tunaomba ikimpendeza, amchukue Thiopister Mallya awe Mkuu wa Barabarani kwa Usitawi wa Taifa.

Japo atapata upinzani kutoka kwa wazee wa tochi na Wamiliki wa Mabasi yanayovunja Sheria sababu hapokei Rushwa wala 10%. Nilichojifunza, Askari Polisi aliye karibu na Wananchi kuwa ni mtenda haki.

Thiopister Mallya alipokuwa msaidizi wa Mkuu wa Usalama Barabarani(Afisa Mnadhimu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Tanzania) alikuwa anaruhusu kupigwa simu saa nane za Usiku, muhimu iwe ya kazi tu.
 
Tumuombeee kwa Mungu,Ila kwa nafasi tajwa hapo iko Chini ya Mamlaka ya IGP!!, nadhani IGP akiona inafaa basi itakuwa heri!!
 
ila polic jaman saiv daa wamezid rushwa jaman iwiiiiiii
 
Hayo majamaa yako na vyeo
 

polisi anayesifiwa,
1.hatimizi wajibu wake sawa sawa"msela"
2.anayemsifia ana maslahi naye"chawa"
3.kweli ametenda haki"mweledi"

wacha tufungue jalada la uchunguzi kwanza.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…