IGP Wambura, nakushauri mtafutieni kazi nyingine ya kufanya RPC Mbeya, amenikwaza sana

Dharau iliyopitiliza dhidi ya Wananchi huwa ni dalili ya mwisho kabisa kabla ya Serikali, Utawala au Mtawala yoyote yule kukumbwa na dhahama ya anguko lake. Karibia kila Mtawala au Tawala zote kabisa hapa duniani ambazo zilikumbwa na anguko la aibu zimewahi kupitia hatua kama hii ya kuwadharau Sana Raia au Wananchi, na Kisha muda mfupi baadaye Tawala hizo zimekumbwa na dhahama kubwa ya kuangushwa.
Mfano mzuri zaidi kwenye suala hili ni kisa Cha kupinduliwa kwa Rais Samuel Doe, aliyekuwa Rais na Dikteta hatari sana katika nchi ya Liberia. Miezi michache kabla ya siku za mwisho za Utawala wake aliwahi kutoa Hotuba kali Sana huku akitumia Lugha ya kebehi, kauli za dharau zilizojaa matusi, dharau na kashfa akiwalenga Wananchi waliokuwa wakimkosoa na Wapinzani wake kisiasa. Wananchi wengi wa Liberia wakati wa wakati huo walichukizwa Sana na hotuba yake hiyo, hivyo mioyoni mwao walidhamiria kwamba lazima siku moja watakuja kumuadhibu Rais huyo mwenye majivuno na kiburi kilichopitiliza.
Haikupita miezi mingi Sana baada ya Rais Samuel Doe kutoa hotuba hiyo ndipo alipojitokeza Mwananchi mmoja Bw. Prince Johnson, Mpinzani mwenye Walinzi wake binafsi (Bodyguards) alipoweka mtego ili amkamate Rais Samuel Doe kwa lengo la kumuadhibu kutokana na Utawala wake mbaya usiowafurahisha Wananchi wengi wa nchi hiyo ya Liberia. Mtego wake Bw. Prince Johnson ulifanikiwa kumnasa na kumkamata Rais Samuel Doe wakati alipofanya safari ya kutembelea Bandari ya Monrovia, hii ni baada ya kupewa taarifa kutoka kwa Wananchi waliokuwa wakiishi jirani na Bandari hiyo. Baada ya kukamatwa na kutokana na chuki kubwa sana waliyonayo Wananchi dhidi ya Rais huyo pamoja na Utawala wake, Wananchi hao baadhi yao walimweleza Bw. Prince Johnson amfanyie udhalilishaji Rais huyo sawa sawa na ule udhalilishaji aliokuwa akiwafanyia Wananchi wa nchi hiyo ya Liberia. Hatimaye kweli Rais Samuel Doe alifanyiwa udhalilishaji mkubwa sana ambao haujawahi kufanyika mahali pengine popote pale hapa duniani, kwani alivuliwa nguo zote kabisa na kisha kubaki uchi wa mnyama huku akirekodiwa mubashara na Waandishi wa Habari.
Nini ninachotaka kusema au kumaanisha hapa? Ninachotaka kusema ni kwamba ni hatari Sana kutumia mbinu chafu za Utawala katika kuongoza nchi au jamii ya watu fulani, ni hatari pia katika nchi vyombo vya usalama kuhubiria chuki dhidi ya kikundi fulani au dhidi ya jamii fulani fulani ya Watu. Vyombo vya usalama daima vijiepushe kufanya vitendo vyovyote vile ambavyo vitasababisha kuibuka kwa chuki na uhasama katika jamii kwani madhara yake ni makubwa sana ambayo huwa hayawezi kurekebishika katikà siku za usoni. Siku zote Watawala wa nchi wanapaswa kuongozwa na Hekima na Busara kubwa ktk kutekeleza majukumu yao.

Rais Samuel Doe alikuwa jeuri Sana alifikia Hadi hatua ya kuwaita na kuwafananisha wakosoaji /wapinzani wake kuwa ni "Vinyesi" ambavyo Makazi yake ya kudumu ni "vyooni' na kwamba alijitapa kuwa Wapinzani wake hao wasingeweza kumfanya kitu chochote kile Rais huyo zaidi ya Wapinzani hao kuendelea kubaki milele huko 'vyooni' walikokuwa.
Na kwa taarifa yako, Bw. Prince Johnson aliyefanikiwa kumkamata Rais Samuel Doe na kisha kumfanyia udhalilishaji, alipongezwa na hata baadhi ya Watawala wengine wa karibu kabisa waliokuwa wakifanya kazi na Rais Samuel Doe ambao walikuwa hawafurahishwi na vitendo vya Rais huyo, na Kamwe Bw. Prince Johnson hakuwahi kuitwa mahali popote pale wala hajawahi kuitwa na/au kuhojiwa na chombo chochote kile Cha Usalama katika nchi hiyo ya Liberia baada ya yeye kufanya tukio Hilo hadi leo hii ninavyoandika comment hii. Aidha, Bw. Prince Johnson aliyehusika na tukio hilo bado yupo hai hadi leo hii na Wananchi wengi wa Liberia bado wanaendelea kumlinda na kumtetea, na pia Wananchi hao wameapa kupambana na mtu yoyote yule atayethubutu kutaka kumshtaki Mahakamani au kumhoji Bw. Prince Johnson kwa kufanya kitendo hicho Cha kumkamata, kumdhalilisha na kumuua Rais Samuel Doe.

Tujiepushe Sana na vitendo vya kuhubiria chuki kwani madhara yake ni makubwa sana.
 
Hili la CP linaweza kuleta matatizo zaidi katika jeshi la polisi na kushindwa kufuata miiko ya kazi zao.
 
Hili la CP linaweza kuleta matatizo zaidi katika jeshi la polisi na kushindwa kufuata miiko ya kazi zao.
Ufike wakati polisi wanaotenda uhalifu wa waziwazi namna hii kwa wananchi wasio na hatia, nashauri vijana wafanye kazi ya Kutafuta taarifa zao na familia zao ikiwa ni pamoja na mahali wanapoishi, wazazi wake, watoto wao wanasoma shule gani na wapi, na kama kuna ndugu zake wajukikane pia, na ikibidi taarifa hizo ziambatane na picha zao then najua kuna watz watashukukuru kuipata hiyo taarifa.
 
Sehemu yako ya kutolea taka ngumu inawakuwasha sana
 
Wewe siku zote ni mpumbavu tu lini wana Mbeya wameanzisha vurugu?
 
Safi sana hii
 
Sikujua kama bado tuna majitu majinga sana hii nchi, uliyeleta uzi ona aibu kidogo
 
Kwa mchango huu wa kijana wa ki Tanzania ndio maana nchi haiendelei kwa kasi inayotakiwa wakati mataifa mengine yakipiga mbio za maendeleo .
 
I am feeling very sorry to you with crippled brain, to the extend worthing nothing to anybody, including to the nation. Better you were created warthog, and enjoy good company of those you resemble in brain.
 
Nonsensical alafu waraka mrefu, mtu mzima hovyo pyeeeee
Tukubali tu kuwa kwa nchi ya watu wengi kama ya kwetu, hatuwezi kuwakosa mashetani na majitu yenye uwendawazimu. Hili ni mojawapo. Tuombee tu lisilete madhara kwa wanadamu.

Watu sijui wanamwonaje Rais Samia!! Yaani mpaka majitu yenye uwendawazimu, utasikia yanamshauri Rais.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…