IGP Wambura, ukijiuzulu hutapungukiwa chochote zaidi ya kujiongezea Heshima mbele ya Jamii

Rabbon

JF-Expert Member
Joined
Apr 16, 2022
Posts
21,625
Reaction score
33,688
Salaam,Shalom!!

Kujiuzulu nyadhifa yoyote katika utumishi wa umma,Si lazima utokane na mapungufu binafsi katika ofisi Yako, la hasha, inawezekana kabisa kujiuzulu Kwa makosa ya Walio chini Yako Kwa uwajibikaji wa pamoja,

Mtu anapotea, ndugu wanazunguka vituo vyote vya polisi, polisi wanadai hawajui mtu huyo alipo, ndugu Wanatafuta mortuary zote bila mafanikio, wanaomba msaada kwenye mitandao ya JAMII, kelele zinapigwa, unapita mwezi mzima, ndipo polisi inakiri kuwa imemshikilia mtu huyo.

Sasa ndugu IGP usipojiuzulu na kupisha uchunguzi ya hao wahusika chini Yako Unadhani wananchi watakubali tena kukamatwa na watu wanaojitambuliasha kama askari?

Jiuzulu haraka ndugu IGP, msaidie Mh Rais ajikite na majukumu mengine ipasavyo sio Kila siku teua, tengua, teua tengua, teua tengua teua tengua teua tengua teua tengua,imetosha sasa!!

Mungu ibariki Nchi yangu nzuri niipendayo TANZANIA πŸ‡ΉπŸ‡Ώ. Amen

Karibuni πŸ™
 
Kujiuzulu ni tabia za kwenye nchi zenye watu.
 
Maisha ya Watanzania na uhuru wao ni muhimu sana,

Ukijiuzulu,hutapoteza Heshima Yako,

Utakumbuka sana!!
 
Reactions: I M
Huo msamiati ni mgumu sana kwa viongozi wa kiafrika,kwani ukipata cheo sio utumishi wa umma bali ni kuula,sasa elewa hapo mpaka atenguliwe

Juzi America kiongozi wa secret service kajiuzulu baada ya Trump kupigwa risasi
 
Ndiyo maana wanasema mstari wa "...wabariki viongozi wake..." uondolewe kwenye wimbo wa taifa
 
Ndiyo maana wanasema mstari wa "...wabariki viongozi wake..." uondolewe kwenye wimbo wa taifa
Itafika time wananchi watagoma kupelekwa polisi.

Tusiifikishe Nchi yetu huko.

Sisi ni kisiwa Cha Amani, hao zombies wapoteza raia wasituharibie image ya nchi yetu.
 
Reactions: I M
bongo hakunaga mtu anajiuzulu, unajiuzulu uache ulaji halafu watoto wale nini? mtu anafia hapohapo au la afukuzwe na mteuaji. hata ningekuwa mimi nsingejiuzulu kama kujirekebisha ningejirekebishia hapohapo tu. najiuzulu alafu nifanye kazi gani?
 
Accountability ni tatizo kwa viongozi na hata jamii. Am sorry unaongea haya kwa jamii ambayo haina hiko kitu
 
bongo hakunaga mtu anajiuzulu, unajiuzulu uache ulaji halafu watoto wale nini? mtu anafia hapohapo au la afukuzwe na mteuaji. hata ningekuwa mimi nsingejiuzulu kama kujirekebisha ningejirekebishia hapohapo tu. najiuzulu alafu nifanye kazi gani?
Sasa asipojiuzulu Leo,

Atakuwa IGP milele?
 
Uko sahihi sana. Haiwezekani polisi ikamteka mtu na kumtesa bila kumfikisha mahakamani. Yaani hadi naishangaa nchi yangu.
 
Uko sahihi sana. Haiwezekani polisi ikamteka mtu na kumtesa bila kumfikisha mahakamani. Yaani hadi naishangaa nchi yangu.
Hii ni Nchi imayoongozwa Kwa Sheria na Katiba,

Ni muhimu watu wawajibike Kwa nafasi zao!!
 
Ajiuzulu kisa vijistori na uzushi wa X
 
Kama ni kweli, si Wambura tu, hata waziri wa mambo ya ndani inabidi awachie ngazi. Ungetuwekea na anapokiri huyo polisi. Nje ya hapo inabaki kuwa ni porojo zako tu.

Si kila mmoja wetu anayejuwa matukio yote na mitandao ya kijamii inapindisha pindisha sana maneno, iungeweka maelezo na ushahidi wa pande zote mbili.
 
Anaitwa Kombo Mwana Twaha,

Alipotea Tanga 29 days ago, polisi wakafungua jalada kumtafuta, baadaye wamekuja kukiri kuwa mtu huyo walikuwa naye.

Sasa Nchi ikiwa Ina utawala wa Sheria, IGP, Mawaziri wa mambo ya ndani, RPC Tanga wanafanya nn ofisi za umma?
 
Reactions: I M
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…