Pre GE2025 Igunga: Mbunge Ngassa Kupiga Kambi Jimboni kwa Siku 30

Pre GE2025 Igunga: Mbunge Ngassa Kupiga Kambi Jimboni kwa Siku 30

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

IGUNGA: "MBUNGE NGASSA KUPIGA KAMBI JIMBONI KWA SIKU THELATHINI"

📌 Kufanya Ziara kwenye Vitongoji vyote vya Mamlaka ya Mji Mdogo wa Igunga kusikiliza kero na kuzipatia ufumbuzi

📌 Kukutana na Wananchi wa Kata Kumi na Sita za Jimbo la Igunga

Mbunge wa Jimbo la Igunga Mhe. Nicholaus George Ngassa Anaanza Ziara ya Kikazi Jimboni kwa ajili ya;

1. Kutoa mrejesho wa Bunge la Bajeti kwa Wananchi.
2. Kuona Maendeleo ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo.
3. Kuhamasisha Wananchi kujitokeza kwenye maboresho ya Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.
4. Kuhamasisha Wananchi kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa Mwaka 2024
5. Kusikiliza Kero za Wananchi na kuzipatia ufumbuzi
6. Kuzindua Mashindano ya Mpira wa Miguu ya Jimbo (NGASSA CUP 2024)

Wananchi Wote Mnakaribishwa. Mikutano itafanyika kuanzia ngazi ya Makundi ya Kijamii, Vitongoji, Mitaa, Vijiji na Kata kwenye maeneo yaliyoandaliwa na Viongozi.

"KAZI NA MAENDELEO"

Imetolewa na:
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Igunga

WhatsApp Image 2024-07-03 at 07.35.51.jpeg
 
Sasa hilo nalo linapaswa kuwa habari? Anachokifanya ndicho hicho anachopaswa kufanya siku zote kama mbunge. Kutangazia kama hivi ni kama vile anafanya msaada mkubwa kwa watu.

Hii ni sawa na mwalimu kusema leo ataingia darasani kufundisha.
 
Why now?

By the way, kwanini unaita kupiga kambi? Kwani anaishigi wapi siku zote? Nilidhani anaishi jimboni so miaka yote yupogo na wapiga kura wake, umaposema kupiga kambi ni kuwa haishi huko ila anakuja kwa siku 30
 
Tuna safari ndefu sana na hawa wawakilishi wa wananchi. Halafu kuna wananchi wenye shida pia, mtu haonekani jimboni. Ikikaribia uchaguzi ndiyo anajitokeaza na mnamchagua tena!!! Mwenyezi Mungu awasimamie.
 
Back
Top Bottom