Mpekuzi Tanzania
JF-Expert Member
- Mar 11, 2018
- 650
- 1,016
MWENYEKITI WA UDP AUNGA MKONO JUHUDI NA KUJIUNGA NA CCM
Mwenyekiti wa Chama cha UDP (United Democratic Party) Wilaya ya Igunga Mhe. Mbogo Athuman Yauha na Wanachama wenzake wameamua kuunga mkono juhudu za kuletea Maendeleo zinazofanywa na Serikali ya Chama cha Mapinduzi (CCM) inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan.
Akiambatana na Wanachama wenzake nane, kwenye Mkutano wa Hadhara wa Mbunge wa Jimbo la Igunga uliofanyika kwenye viwanja vya kumbukumbu ya Sokoine, Mhe. Mbogo (Mwenyekiti UDP) amesema,
"... Mimi ni Mwenyekiti wa UDP Wilaya na niligombea udiwani Mwaka 2020, lakini sioni sababu kubaki upinzani kwa kuwa yale yote niliyotamani kuyasimamia kwasasa yanafanywa kwa kasi na Mhe. Samia Suluhu Hassan.... Hata hapa Igunga Mbunge na Diwani wanafanya utekekelezaji wa Maendeleo kwa kasi ya Rais wa awamu ya Sita. Mbunge (Ngassa) kaeleza Miradi ya Maendeleo aliyoisimamia ndani na Mwaka Mmoja na miradi inayoendelea kutekelezwa kwenye Sekta za Elimu, Afya, Maji, Barabara, Umeme, Mikopo kwa Vijana, Wanawake na Walemavu. Nimeamua kuachia madaraka yangu na kuwa mwanachama wa kawaida wa CCM, nitakuwa mwaminifu na mtiifu kwa Chama cha Mapinduzi..."
Baada ya kurudisha kadi viongozi hao wameelekezwa tararibu za kujiunga na Chama cha Mapinduzi na kupatiwa nasaha na Katibu Mwenezi wa CCM Mkoa wa Tabora Ndg. Majaliwa Bilali aliyekuwa Mgeni Rasmi kwenye Mkutano wa Hadhara wa Mbunge wa Jimbo la Igunga. Mkutano umeudhuriwa na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Tabora Mhe. Jacqueline Kainja, Waheshimiwa Madiwani wa Kata za Jimbo la Igunga, Viongozi wa CCM Wilaya, Kata , Matawi na Mashina.
Kazi iendele.
Mwenyekiti wa Chama cha UDP (United Democratic Party) Wilaya ya Igunga Mhe. Mbogo Athuman Yauha na Wanachama wenzake wameamua kuunga mkono juhudu za kuletea Maendeleo zinazofanywa na Serikali ya Chama cha Mapinduzi (CCM) inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan.
Akiambatana na Wanachama wenzake nane, kwenye Mkutano wa Hadhara wa Mbunge wa Jimbo la Igunga uliofanyika kwenye viwanja vya kumbukumbu ya Sokoine, Mhe. Mbogo (Mwenyekiti UDP) amesema,
"... Mimi ni Mwenyekiti wa UDP Wilaya na niligombea udiwani Mwaka 2020, lakini sioni sababu kubaki upinzani kwa kuwa yale yote niliyotamani kuyasimamia kwasasa yanafanywa kwa kasi na Mhe. Samia Suluhu Hassan.... Hata hapa Igunga Mbunge na Diwani wanafanya utekekelezaji wa Maendeleo kwa kasi ya Rais wa awamu ya Sita. Mbunge (Ngassa) kaeleza Miradi ya Maendeleo aliyoisimamia ndani na Mwaka Mmoja na miradi inayoendelea kutekelezwa kwenye Sekta za Elimu, Afya, Maji, Barabara, Umeme, Mikopo kwa Vijana, Wanawake na Walemavu. Nimeamua kuachia madaraka yangu na kuwa mwanachama wa kawaida wa CCM, nitakuwa mwaminifu na mtiifu kwa Chama cha Mapinduzi..."
Baada ya kurudisha kadi viongozi hao wameelekezwa tararibu za kujiunga na Chama cha Mapinduzi na kupatiwa nasaha na Katibu Mwenezi wa CCM Mkoa wa Tabora Ndg. Majaliwa Bilali aliyekuwa Mgeni Rasmi kwenye Mkutano wa Hadhara wa Mbunge wa Jimbo la Igunga. Mkutano umeudhuriwa na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Tabora Mhe. Jacqueline Kainja, Waheshimiwa Madiwani wa Kata za Jimbo la Igunga, Viongozi wa CCM Wilaya, Kata , Matawi na Mashina.
Kazi iendele.