Elections 2010 Igunga wakisahihisha makosa yao tutawasamehe... ?

DSN

Sijui unazungumzia Wasukuma wepi tusiowajua sisi, unaposema kiongozi wa familia wa wasukuma, wanyamwezi, wanyaturu ni mwanamke nakushangaa sana, kwa makabila uliyoyataja mwanamke hahesabiki kabisa kama sehemu ya familia sembuse kuwa kiongozi, hadi leo mtoto wa kike hatambuliki hata katika masuala ya urithi wa familia, mfano mdogo tu wanaume wakiwa wanajadili jambo fulani la kifamilia au kijamii mwanamke hatakiwi kuwepo sehemu ile hata kama akiwepo hatakiwi kuchangia chochote wana msemo 'wewe mwanamke utatuambia nini nenda jikoni'.

Bado mfumo dume unatawala sana makabila hayo na kiongozi wa familia bado ni mwanamme, labda sema kutokana na mwingiliano wa tabia za makabila mbalimbali na uchumi tegemezi kwenye familia siku hizi mwenye sauti ni yule mwenye nguvu ya uchumi awe kijana, mwanamke au mwanamme.

Nakubaliana nawe kuhusu upole wa makabila hayo lakini elewa mtu mpole akiamua kubadilika ni vigumu sana kum- convince otherwise, mfano ni matokeo ya uchaguzi wa mwaka jana ambayo yaliishtua hata CCM, wabunge wengi wa upinzani wametoka sehemu hizo na kura nyingi za urais za upinzani zimetokea kule, jiulize Mwanza na Shinyanga ya miaka ya Nyerere ulinganishe na leo labda Tabora ya kina Rage ambayo nayo tunaweza kuanza kuona mabadiliko kwenye uchaguzi huu.
 
Mwanakijiji tafadhali sana naomba hii itoke kwenye magazeti ya kila siku na toleo moja maalum siku ya jumapili, wapiganaji wajitahidi gazeti lisambazwe igunga hata bure badala ya kurusha chopa tu!

Huu ujumbe unasomeka vyema na wana Igunga wanajuwa kusoma na kuandika.
 

Article inakosa mfuto kwa kupersonalize issue ya ufisadi arround one person "ROSTAM" na kusahau role played by other key participants Lowassa, etc..

You are always at very front attacking personalities of certain group of citizen in Tanzania..

Hatuna sababu ya kukuamini kwamba unaendeleza fikra zako za kijumuiya hapa pia...
 
Nilitegemea baada ya comment yako utachangia chochote.
 
Nilitegemea baada ya comment yako utachangia chochote.

Nichangie nini wakati issue ya ufisadi in fact si ufisadi hasa unaolengwa ila personalities of certain group of citizen...

Wananchi wana haki ya kumchagua yeyote tu lakini ...si kwasbabu ana nia ya kupambana na ufisadi..hoax

wapiganaji wenyewe kina (Sitta, Mwakyembe, Mwanakijiji ect) kimya baada ya doawans kuuziwa mmerakani..

So the fight was about certain group of citizen period..lakini mkiliwa na mzungu poa tu..
 
......

wapiganaji wenyewe kina ( J M Kikwete ,Sitta, Mwakyembe, Mwanakijiji ect) kimya baada ya doawans kuuziwa mmerakani..

Nimemuongeza Rais wetu JK kama mpiganaji number moja wa ufisadi sabau so far Liyumba, Mramba, Yona wana kesi za kujibu.

Je

  • Hizo ndizo "personalities" na certain group of citzen wanaolengwa kwa ufisaidi wa tanzania?
  • Personality gani ya Kitanzania aliyonayo RA tofauti na hao wengine wachache nlitaja hapo juu kumfanya asitakiwe kusemwa au kuwa criticized?
  • Kwa nini kutajwa kwa RA iwe mwiba kwako?
Ebu fafanua
 
Kwa mtazamo wangu kuna mambo mengi yanayoathiri siasa za Tanzania. La kwanza kabisa siasa za Tanzania hazijakaa katika mwelekeo wa kuwapa wapiga kura usahihi wa amchague nani na kwa sababu gani. Nachukulia mifano ya nchi nyingine ambazo makundi siasa ya nchi hizo yanaeleweka kiuchumi (nichague mjamaa au mbepari?), kiutamaduni (nichague mhafidhina au mliberali?), kidini (nichague mkatoliki au mprotestanti?). Na ndio maana kwa kesi ya Igunga ilikuwa rahisi sana kwa Rostam kukaa pale muda mrefu. Watu wa Igunga hawakuwa na sababu ya kumkataa kwa sababu hawana dira ya wanataka wafike wapi na Rostam atawafikishaje pale. Na kwa vile Rostam ni tajiri aliweza kuwapofusha watu wa Igunga kwa kuwatuliza kinamna pale watu fulani fulani walipomwendea na kumpigia magoti (siasa za kifalme) wakimwomba awape hiki na hiki (maskini ataomba nini kama si unga na mchele wa siku moja?).

La pili mimi naona kama siasa za Tanzania kwa ujumla wa nchi na kimajimbo hazitabiriki kwa sasa na zinabadilika kievolution (mabadiliko ya pole pole kadiri muda unavyosonga kutegemea na watu husika na kwa sababu tofauti). Kwa mfano siasa za bukoba ni tofauti na siasa za iringa. Siasa za ubungo ni tofauti na ilala. Ili ni jambo ambalo linanishangaza hata mimi, na nitawaachia watu wa political science wafanye uchambuzi wao wanafahamu kuliko mimi. Lakini component ya dini huwezi kuipuuza. Waislam wanapenda sana block vote na sehemu zenye waislamu wengi usitegemee kupata kura nyingi kama ukipuuza matakwa yao.

Yapo mambo mengine pia kama hela za chama au mgombea husika, elimu ya wapiga kura eneo husika, historia ya mgombea kwenye jimbo hilo, akili na charisma ya mgombea (hii inaeleza ubunge wa watu kama Lissu, Zitto, Mnyika, Kafulila, ingawa hawakuwa matajiri na wanatoka vyama vya upinzani; naweza pia kusema kwamba kati ya mtaji wa Chadema kisiasa ni kuvutia vijana wenye charisma), vyote hivyo vinaelezea kwamba siasa za Tanzania sio monolithic, hazitabiriki, lakini zinatoa matumaini kwamba huko mbele chama lege lege haikitakuwa na nafasi kwenye mioyo ya watanzania walio wengi.
 

wakichagu ccm hatutawasamehe kamwe kwani watakuwa wameonyesha kiburi kikubwa sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…