Ihefu FC yamtema Kocha wake Zuberi Katwila

bakundande jr

JF-Expert Member
Joined
Oct 22, 2021
Posts
507
Reaction score
672
Uongozi wa timu yetu umefikia makubaliano ya pande mbili ya kuvunja Mkataba na aliyekua Kocha wetu Mkuu Zuberi Katwila.

Hata hivyo ongozi wa timu unamshukuru Kocha katwila kwa wakati wote aliokua nasi ndani ya timu kama Kocha Mkuu tangu alipojiunga nasi mwaka 2020.

Ihefu Sc inamtakia kila la kheri Kocha Katwila katika maisha yake mapya ya soka na atabaki kuwa Mwanafamilia wa MbogoMaji.

Kwa kuongezea ihefu fc chini ya kocha wao zuberi katwila ndio timu pekee ilioweza kupata ushindi mara mbili dhidi ya mabingwa wa kihistoria wa ligi kuu Tanzania yanga sc katika misimu miwili.

Kuna watu watakuwa wamefurahi na kuna watu watakuwa na huzuni.
 
Moja ya makocha wazawa vijana wenye uwezo wa kufundisha Mpira. Naamini atafanya vizuri aendako. Wengine ni Mexime na Matola ( huyu anadeka Simba)
 
Hapo ndo walipokosea wakikutana na yanga tena watakula za mvua
 
Moja ya makocha wazawa vijana wenye uwezo wa kufundisha Mpira. Naamini atafanya vizuri aendako. Wengine ni Mexime na Matola ( huyu anadeka Simba)
Kijana?baba ake q chief . Ana watoto na wajukuu plus vitukuu bado una muita kijana?
 
Sababu anaifunga Yanga tu au kuna lingine?
Nadhani Wenye Yanga Yao wamamfanyia firigisi ili aondolewe.
Huyo alikuwa pale kwa akili ya kuifunga Yanga tuu Simba akienda anajiokotea points za bure kama ilivyokuwaga Matola alipokuwa anaifundisha Lipuli ya Iringa, timu mpaka imeshuka daraja ilifanikiwa kuifunga Yanga tuu, hao ndiyo makocha wazalendo wa kitanzania[emoji2][emoji2][emoji2]
 
Tunaleta kocha Mhindi, kutoka Bombay



Deepak Tanna
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…