Ijue historia ya Chifu Mkwawa (Sehemu ya kwanza)

Namkubali sana,ila kujiua ndio kitendo kilichonikwaza
 
Namkubali sana,ila kujiua ndio kitendo kilichonikwaza
Nilienda kalenga kama utalii wa ndani na kwa mujibu wa yule msimuliaji pale alisema alijiua kwasababu aliichukia ngoz nyeupe hivyo alitaka isimguse ndio maana akajiua. [emoji24] ndio maana walipo mkuta kafa waka mkata kichwa ili wapeleke uko kwao kuenda kuonesha mtu alie watesa na wanamkubali sana kwa mbinu zake maana ziliwatesa sana. But kichwa fuvu lilirudi na lipo kalenga pale yan jamaa alikua mchawi huyu alikua na kiti na chungu na mti nje pale
Kile kiti hukalia yeye tu mpaka leo kipo
Chungu kile kama kuna hatari hutoa damu automatic
Kama kuna neema hutoa maji ndio alikua akikitumia kujua what happens next
Mti wake ulikua ukikaa pale unapotea uo mti mpaka leo upo kalenga pale pale kwenye museum
 
Duh!...huku kwa kina mkwawa mzee wangu wa historia ya wazee wa kariakoo Mohamed Said sidhani kama ana ilim yoyote.
 
Bwana Mvika
Hii historia safi sana. Inaonekana sisi watu wa iringa kila msomi ana maelezo fulani ambayo yakikusanywa vizuri yanaweza kutoa picha sahihi ya utawala huu wa Wahehe. Jambo la kufanya ni kila mwandishi kuelezea vianzo vya historia ili kama mtu mwingine ana chanzo bora zaidi aweze kuongezea. Basi malizia hiyo historia kisha wengine tutasaidia kuelezea ama kwa kirefu zaidi au kuanzia mapema zaidi kabla ya Mutwa Munyigumba.
Pia historia ya Wahehe ukiileza vizuri utakuta Wahehe walianza kufikia hatua ya kuwa "taifa" linalojitambua, lenye nchi yenye mipaka inayotetewa na mgawanyo wa kazi unaotegemeana nje ya koo. Maendeleo ya taifa hili yalikatishwa na ujio wa ukoloni.
Ilifikia wakati ambao wale waliofanya mzaha kiasi cha kuhatarisha taifa hilo walishughulikiwa haraka na bila huruma. Hili suala la kusisitiza "mahomelo" katika medani za kivita ni mambo ya kisaikolojia zaidi. Kwwa hakika Wahehe walikuwa wapiganaji wenye akili ya kutisha. Ile vita ya Lugalo ambapo Mjerumani alipigwa kama mtoto ndiyo ilithibitisha uwezo wa kivita wa Wahehe. Wahehe waliwaona Wajerumani wakija wakiwa Usagara chini ya Mlima Kitonga. Lakini wakaamua wasianze vita mapema. Wakatafuta mahala ambapo wao Wahehe walikuwa wana nafuu (advantage) kivita. Wakawangoja mpaka walipoingia bonde la Lugalo. Wakawapiga hapo. Mjerumani anaandika kuwa mbinu ya aina hiyo ilikuwa ya Napoleon wa Ulaya hawakuitegemea kuikuta kwa Mwafrika. Hiki ndiyo kisa cha Wajerumani kutaka kichwa cha Mkwawa kipelekwe Ujerumani wakidhani wangeweza kubaini alikuwa na ubongo wa aina gani au pengine kichwa kingeonesha kuwa hakuwa Mwafrika!
Pia ushindi wa Wahehe ulitokana na kuwa Wahehe walikuwa taifa changa la mchanganyiko wa makabila mengi. Hiyo nguvu kazi mpya na akili mpya ya Wahehe ilikuwa tofauti na makabila jirani. Green card ya Marekani ya sasa ya kutaka vijana wenye vipawa mbali mbali kutoka sehemu yo yote nje ya Marekani kuhamia Marekani si suala la kubahatisha lilianza zamani. Taifa ambalo watu wake wanazaliana wenyewe kwa wenyewe baada ya muda mrefu linakuwa na vizazi dhaifu.
Historia ikifundishwa vizuri ni nguzo muhimu kwa taifa. Ndiyo maana nampongeza kwa dhati huyu mwandishi na tafadhali amalizie alichokusudia kutujuza. Kumbukeni imesemwa na watu wanaofikiri kwamba: Wale wanaoipuuza historia watairudia!
 
Dah nzuri ila gupi sana mtumalizie hiyo story!Pamoja na hayo wale wenye historia za machifu wengine pia watujuze itakaa njema zaidi
 
Nimebahatika kufika Makumbusho ya Mkwawa pale Kalenga. Kuna kiongozi wa Watalii( ana uhusiano na ukoo wa Mkwawa) anasimulia hiyo hadithi kama unatazama movie aisee. ..nilijaribu kumrekodi alivyosimulia mara ya kwanza nilipofika pale ni tamu zaidi kuliko mara ya pili.
Inadaiwa Mkwawa alikuwa na wake 62 ambao aliwagawa kwenye makundi takribani 7. Kila kindi lilikuwa na mke kiongozi. Sasa Mkwawa alikuwa na chungu fulani hivi chenye matundu matundu ambacho akiweka dawa kilikuwa kinamtonya iwapo kuna mmoja kati ya 62 amechepuka.....!!!!
Katika masimulizi ya yule tour guide ni kuwa katika jeshi lake Mkwawa alikuwa na wanjeshi (makomandoo) wa kike hao walikiwa balaa. Tena alikuwa na vikosi kama vinne hivi; kikiwemo cha Upelelezi (kuna jina la kihehe alitutajia nalo ni jina la eneo mashuhuri pale Iringa maeneo ya nyuma ya Ratco mpaka Idara ya Maji, pia askari wa chambo wa kumuingiza adui kwenye reli (mmoja ndiye aliwaingiza askari wa kijerumani kwenye reli wakauawa kama sisimizi kwenye sukari) hawa walikuwa dhaifu kwa mwili kama mateja wetu, lakini ni shupavu ubongoni balaa.
Kwa jinsi anavyosimulia tour guide kama tungekuwa na akina Mkwawa wa5 hakika tusingetawaliwa....
Kilichomponza ni USALITI wa Chifu wa Wabena na Wasangu, waliokuwa tayari kuwaonesha Wajerumani ya kufika Kalenga usiku usiku wakitokea maeneo ya Mafinga..
Ukienda pale utainjoi zaidi kuliko kisimuliwa hapa.
 
Hicho ni chungu kimojawapo kati ya vyungu alivyovitumia kubaini mahali walipo maadui, pia kuweka dawa kubaini UCHEPUKAJI wa wakeze.
 

Hili ndilo fuvu lake ambalo limeifadhiwa vema kabisa pale Makumbusho ya Mkwawa- Kalenga
 
hapo daraja la mungu alipoenda mama mkwawa ni kule mbeya na humo alipojirusha ni pale kwenye kijungu Mbeya
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…