Ijue historia ya Wahaya wa Kiziba ''Wenye Kagera Yao''

Ijue historia ya Wahaya wa Kiziba ''Wenye Kagera Yao''

Waarabu hawakuja. Kumbuka hilo.

Waarabu Afrika ni kwao hata jina Afrika ni la Kiarabu, pengine hata jina Bukoba ni la Kiarabu.

Ukiwa mtumwa ni mtumwa tu, huwezi kutofautisha tena ni heri ya utumwa wa biashara kuliko utumwa wa kudhalilishwa utu, hususan ulioandikwa post namba moja, wa ngono. Hiyo ni sex slavery.

Waarabu Afrika ni kwao hata jina Afrika ni la Kiarabu, pengine hata jina Bukoba ni la Kiarabu


Hii kali. Umeiokota wapi ndugu?

Unique Facts about Africa: Origin of the Name 'Africa'
 
Historia ya Uislam Kagera siijui na wala sijawahi kuifuatilia. Waislam Kagera ni wachache sana kama ilivyo mikoa ya Kilimanjaro,Mbeya,Iringa,Mara.

Labda kuna waislam maarufu kama wakina Suedi Kagasheiki, Ali Migeyo, , Abdallah Rutabanzibwa, Kaitaba.

Kuna mji wa Katoro uko Bukoba Vijijini, huko ndiko kuna waislam asilimia kubwa. Waislamu hao wana itikadi kali sana na kama sio mwislam basi kuishi mazingira ya hicho kijiji ni ngumu sana, kiufupi ni wabaguzi sana.

Kule wanafundisha Ilm Akhera na elimu dunia hawajaipa kipaumbele.
Wapo pale katoro barabarani tu na wala siyo katoro vijijini, wapo maeneo ya mjinimjini tu sehemu chache walipoishi waarabu kama vile katoro mjini nshamba na kamachumu na kwnyewe ni sehemu za njiani tu ukiingia vijijini kwa ndani unakuta ukristo umetia mizizi.
 
Kwa kifupi wakati mimi niko shule ya msingi katika miaka ya arobaini, Tanganyika ilikuwa imegawanywa katika majimbo (provinces) 8, ambayo ni: Lake, Northern, Tanga, Eastern, Southern, Central, Western na Southern Highlands. Lake Province ilikuwa na wilaya (districts) 11, ambazo ni Mwanza, Bukoba, Biharamulo, Ngara, Shinyanga, Geita, Musoma, Kwimba, Maswa, Mara (ambayo sasa ni Tarime) na Ukerewe. Idadi hii ilikuja ikaongezeka mwaka 1956 wakati Karagwe ilipopewa hadhi ya wilaya. Kabla ya 1956, wilaya ya Bukoba ilijumuisha wilaya za sasa za Bukoba, Muleba, Missenyi, Karagwe na Kyerwa.

Wenyeji wake waliitwa na wakoloni Wahaya, ingawa baada ya kupata wilaya yao, baadhi ya wenyeji wa Karagwe walikataa kuitwa Wahaya. Akifafanua chanzo cha jina hilo, Mjerumani Stuhlmann aliandika mwaka 1899 kuwa lilikuwa ni jina la maeneo ya Mukama Kisebuka na Mukama Bwahama wa Kiamutwara, hasa yale yaliyo kwenye mwambao wa ziwa.

Wajerumani walipoona mila zetu na lugha zetu zinafanana wakaamua kutuita Wahaya. Hivyo jina Wahaya linajumuisha Bahyoza, Bahendangabo, Baziba, Bahamba, Banyaihangiro, Banyambo, Bakara na Babumbiro. Wakoloni waliwaunganisha Wahaya katika Buhaya Council iliyokuwa na makao makuu yake pale Rwamishenye.

Kiongozi wa secretariat yake aliyekuwa na umaarufu mkubwa alikuwa ni Omwami Francisco Xavier Rwamugira aliyejulikana kama Omukama wa mwenda. Kwa kuwa alikuwa Mziba, alisababisha watu wengine kuwachukia Waziba, kutokana na hisia kuwa Rwamugira alikuwa anapendelea watu wa Kiziba.

Kila moja ya makabila haya ilikuwa inatawaliwa na Mukama (king), na kila Bukama (kingdom) iligawanywa katika gombolola zilizokuwa zinaongozwa na abami (palatines). Kila gombolola ilikuwa na vijiji kadhaa vilivyoongozwa na abakungu. Kabla ya wakoloni kuja, Mukama alikuwa absolute ruler, kwa maana kwamba, neno lake lilikuwa ni sheria na ardhi yote ilikuwa ni mali yake.Kadhalika hata watu, mifugo na misitu vyote vilikuwa ni mali zake.

Kiziba ilikuwa na gombolola 8 ambazo ni: Kanyigo, Bwanja, Buyango, Gera, Bugandika, Kitobo, Ishozi na Kibumbiro. Wakati wa utoto wangu mwami wa Kanyigo alikuwa Omulangila Lukambaiga mtoto wa Omulangila Lushanzilana, mtoto wa Mukama Mutatembwa. Lukambaiga ndiye baba yake Omutemba Bernado wa Bugombe.

Mzungu wa kwanza kukanyaga Bukoba alikuwa ni Mjerumani Emin Pasha aliyewasili tarehe 31 Oktoba, 1890, ingawa miaka 30 kabla ya hapo Waingereza wawili, T.H. Speke na T.A Grant waliwahi kufika Karagwe na kukutana na Omukama Rumanyika l (Rugundu). Gavana wa kwanza wa kijerumani ni Julius von Soden (1891-1893) na wa mwisho ni Heinrich Schnee (1912-1916).

Gavana wa kwanza wa kiingereza ni Sir Horace Byatt (1916-1924) na wa mwisho ni Sir Richard Turnbull (1958-1961).

Sisi Bahaya (wakiwemo Banyambo) tunajulikana kama Western Interlacustrine Bantu. Tulihama kutoka Uganda Magharibi katika karne za 15 na 16, hasa kutoka Bunyoro na Ankole. Koo nyingi kama ule wa kwangu (abaziba/ababiito) asili yetu ni Bunyoro na chache kama abamiilo/abagabo asili yao ni Ankole.

Kihanja, Ihangiro na Bukara Bakama wao ni Bahinda wakati wale wa Kiamutwara na Bugabo ni Bankango waliowaasi Bahinda na kujitangazia uhuru yapata mwaka 1820 wakati Mukama Kalemera ll alipofariki. Uasi huu uliongozwa na Kitekere na baadaye kuimarishwa na mtoto wake Omukama Kaitaba (1860-1888). Bakama wa Kiziba ukoo wao ni Baziba/Babiito. Baada ya kifo cha Mukama Burungu ll (1800-1835) walipendelea kuitwa Abayobya. Sababu ni kwamba wanatokana na Omulangila Luyobya, mtoto wa Mukama Ruhangarazi l. Kutokana na ukatili uliopitiliza wa Burungu ll, baba yake mdogo, Omulangila Luyobya, alishindwa kumvumilia, na hivyo akaanzisha vita ya kumng’oa. Katika vita hii alisaidiwa sana na mtoto wake aliyeitwa Rutahilwa. Luyobya kwake kulikuwa ni Bukwali, Kanyigo.

Burungu ll alijikuta katika hali ngumu ya kushambuliwa kutoka ndani na nje, kwani Bahyoza walikuwa pia wanamshambulia. Baada ya Burungu kuuawa na maadui mwaka 1835, Rutahilwa, mtoto wa Ruyobya alitawala na akapewa jina Kibi ll. Baada ya Kibi ll, alitawala mtoto wake Rugangarazi ll (1858-1865), halafu Mutatembwa (1865-1903), halafu Mutahangarwa (1903-1916), halafu Mboneko ll (1916-1926), halafu Mutakubwa (1926-1937), halafu Lutinwa (1937-1974).

Mutakubwa aliondolewa na wakoloni mwaka 1937 na hakuwa na mtoto. Hivyo ndugu yake Mboneko aitwaye Nestor Lutinwa alichaguliwa kumrithi, na akatawala mpaka Nyerere alipofutilia mbali utawala wa Bakama.

Katika Kanyigo nzima mtu pekee aliyezaliwa wakati wa utawala wa Mutahangarwa amebaki mmoja tu, naye ni mzee Ta Baltholomayo wa Bugombe. Huyu kuzaliwa kwake ni datable kwani nilipomhoji aliniambia kuwa wakati Mutahangarwa anafariki alikuwa na umri wa kuanza shule wa watoto wa siku hizi.

Sababu ya kuondolewa kwa Mutakubwa ni ufuska uliokithiri, ukiwemo ule wa kulazimisha. Mama yake Muchureza alijaribu kumkanya lakini hakusikia. Hivyo alikwenda kumuomba DC wa kikoloni amsaidie kumkanya. Badala ya kumkanya DC alimfukuza, kwani kwa mzungu kubaka ni dhambi isiyosameheka. Lakini DC hakuelewa kuwa Mukama hawezi kuwa na hatia ya kumbaka mwanamke au kufanya uasherati, kwani kwa mila zetu wanawake wote ni mali ya Mukama. Hivyo watu wakawa wanamuimba Muchureza kuwa ni kilimi nyakwelega ayagambiile omujungu ati Omukama nasiyana. Maana yake, wimbo ulikuwa unamsuta Muchureza kwa kujichongea (okwelega) bila sababu ya msingi.

Mutakubwa, baada ya kufukuzwa, alimalizia maisha yake pale Kigarama, kwa Edward Kasano, kwani baba yake Edward alikuwa tumbo moja na Mutakubwa, wote wakiwa ni watoto wa Muchureza. Alifariki mwaka 1948 na kuzikwa pale Kigarama. Jambo la ajabu nililoshuhudia ni kwamba wazee pale kijijini waliendelea kumpa heshima kama Mukama wakimwamkia Habuka Izoba, Habuka Lugaba, Habuka Nyakusinga, nk.

Baadaye nilikuja kuelewa kuwa mtu akishasimikwa kama Mukama anakuwa na namna ya uungu (semi-divine). Hivyo ukimnyima heshima yake unaweza ukapatwa na mabaya.

Enock L. Kamuzora
Ukisoma habari nzima utaona unagusia kusia Wanyambo kwa sababu unajua ujataja historia yao na kingdom yao ilivyokuwapo miaka hata kabla ya wazungu kufika. Na kama unavyojua wazungu nia yao ilikuwa divide and rule kwa hiyo walifanya kuwagawa wanyambo ambao walikuwa na kingdom iliyokuwa na nguvu na kuwaweka chini ya kibaraka wao. Na ndiyo maana katika kutaja ujataja asili ya wanyambo na watawala wao. Umeishia kumtaja Mukama Rumanyika aliyekutana na Speke.
Rudi ukasome kitabu cha Marehemu Professa Katoke utapata tafiti nzuri ya kisomi.
Kifupi tu ni kwamba huwezi kusema Wahaya (Wakiwemo Wanyambo) Ni makosa makubwa, Wahaya wanajitegemea na Wanyambo wanajitegemea pamoja na kwamba lugha zinashabiana kama walivyo Wasubi, Wazinza, Wakara, Wakelewe, wanyankole, Wanyoro na watoro wote lugha zikiwa zinafanana kwa mtu ambaye hazijui
 
Waarabu Afrika ni kwao hata jina Afrika ni la Kiarabu, pengine hata jina Bukoba ni la Kiarabu

Hii kali. Umeiokota wapi ndugu?

Unique Facts about Africa: Origin of the Name 'Africa'

Huyo aliyeandika hiyo article hana uhakika, huioni "probably"?

Hizo nchi alizotaja zote zinaongea Kiarabu.

Afrika ni neno la Kiarabu linalomaanisha kuliko jificha. Linatokana na Afrit au wengine hutamka Ifrit kwa maana aliyejificha "hideous one".

Hata wewe una asilimia fulani ya Kiarabu sema hujui tu maana ya Uarabu.

Wewe kama Muhaya tuambie maana ya Bukoba ni nini?

Unauliza nimeokota wapi? Source ni mimi mwenyewe.
 
Usithubutu ku comment bila kusoma mpaka mwisho
Kwa kifupi wakati mimi niko shule ya msingi katika miaka ya arobaini, Tanganyika ilikuwa imegawanywa katika majimbo (provinces) 8, ambayo ni: Lake, Northern, Tanga, Eastern, Southern, Central, Western na Southern Highlands. Lake Province ilikuwa na wilaya (districts) 11, ambazo ni Mwanza, Bukoba, Biharamulo, Ngara, Shinyanga, Geita, Musoma, Kwimba, Maswa, Mara (ambayo sasa ni Tarime) na Ukerewe. Idadi hii ilikuja ikaongezeka mwaka 1956 wakati Karagwe ilipopewa hadhi ya wilaya. Kabla ya 1956, wilaya ya Bukoba ilijumuisha wilaya za sasa za Bukoba, Muleba, Missenyi, Karagwe na Kyerwa.

Wenyeji wake waliitwa na wakoloni Wahaya, ingawa baada ya kupata wilaya yao, baadhi ya wenyeji wa Karagwe walikataa kuitwa Wahaya. Akifafanua chanzo cha jina hilo, Mjerumani Stuhlmann aliandika mwaka 1899 kuwa lilikuwa ni jina la maeneo ya Mukama Kisebuka na Mukama Bwahama wa Kiamutwara, hasa yale yaliyo kwenye mwambao wa ziwa.

Wajerumani walipoona mila zetu na lugha zetu zinafanana wakaamua kutuita Wahaya. Hivyo jina Wahaya linajumuisha Bahyoza, Bahendangabo, Baziba, Bahamba, Banyaihangiro, Banyambo, Bakara na Babumbiro. Wakoloni waliwaunganisha Wahaya katika Buhaya Council iliyokuwa na makao makuu yake pale Rwamishenye.

Kiongozi wa secretariat yake aliyekuwa na umaarufu mkubwa alikuwa ni Omwami Francisco Xavier Rwamugira aliyejulikana kama Omukama wa mwenda. Kwa kuwa alikuwa Mziba, alisababisha watu wengine kuwachukia Waziba, kutokana na hisia kuwa Rwamugira alikuwa anapendelea watu wa Kiziba.

Kila moja ya makabila haya ilikuwa inatawaliwa na Mukama (king), na kila Bukama (kingdom) iligawanywa katika gombolola zilizokuwa zinaongozwa na abami (palatines). Kila gombolola ilikuwa na vijiji kadhaa vilivyoongozwa na abakungu. Kabla ya wakoloni kuja, Mukama alikuwa absolute ruler, kwa maana kwamba, neno lake lilikuwa ni sheria na ardhi yote ilikuwa ni mali yake.Kadhalika hata watu, mifugo na misitu vyote vilikuwa ni mali zake.

Kiziba ilikuwa na gombolola 8 ambazo ni: Kanyigo, Bwanja, Buyango, Gera, Bugandika, Kitobo, Ishozi na Kibumbiro. Wakati wa utoto wangu mwami wa Kanyigo alikuwa Omulangila Lukambaiga mtoto wa Omulangila Lushanzilana, mtoto wa Mukama Mutatembwa. Lukambaiga ndiye baba yake Omutemba Bernado wa Bugombe.

Mzungu wa kwanza kukanyaga Bukoba alikuwa ni Mjerumani Emin Pasha aliyewasili tarehe 31 Oktoba, 1890, ingawa miaka 30 kabla ya hapo Waingereza wawili, T.H. Speke na T.A Grant waliwahi kufika Karagwe na kukutana na Omukama Rumanyika l (Rugundu). Gavana wa kwanza wa kijerumani ni Julius von Soden (1891-1893) na wa mwisho ni Heinrich Schnee (1912-1916).

Gavana wa kwanza wa kiingereza ni Sir Horace Byatt (1916-1924) na wa mwisho ni Sir Richard Turnbull (1958-1961).

Sisi Bahaya (wakiwemo Banyambo) tunajulikana kama Western Interlacustrine Bantu. Tulihama kutoka Uganda Magharibi katika karne za 15 na 16, hasa kutoka Bunyoro na Ankole. Koo nyingi kama ule wa kwangu (abaziba/ababiito) asili yetu ni Bunyoro na chache kama abamiilo/abagabo asili yao ni Ankole.

Kihanja, Ihangiro na Bukara Bakama wao ni Bahinda wakati wale wa Kiamutwara na Bugabo ni Bankango waliowaasi Bahinda na kujitangazia uhuru yapata mwaka 1820 wakati Mukama Kalemera ll alipofariki. Uasi huu uliongozwa na Kitekere na baadaye kuimarishwa na mtoto wake Omukama Kaitaba (1860-1888). Bakama wa Kiziba ukoo wao ni Baziba/Babiito. Baada ya kifo cha Mukama Burungu ll (1800-1835) walipendelea kuitwa Abayobya. Sababu ni kwamba wanatokana na Omulangila Luyobya, mtoto wa Mukama Ruhangarazi l. Kutokana na ukatili uliopitiliza wa jBurungu ll, baba yake mdogo, Omulangila Luyobya, alishindwa kumvumilia, na hivyo akaanzisha vita ya kumng’oa. Katika vita hii alisaidiwa sana na mtoto wake aliyeitwa Rutahilwa. Luyobya kwake kulikuwa ni Bukwali, Kanyigo.

Burungu ll alijikuta katika hali ngumu ya kushambuliwa kutoka ndani na nje, kwani Bahyoza walikuwa pia wanamshambulia. Baada ya Burungu kuuawa na maadui mwaka 1835, Rutahilwa, mtoto wa Ruyobya alitawala na akapewa jina Kibi ll. Baada ya Kibi ll, alitawala mtoto wake Rugangarazi ll (1858-1865), halafu Mutatembwa (1865-1903), halafu Mutahangarwa (1903-1916), halafu Mboneko ll (1916-1926), halafu Mutakubwa (1926-1937), halafu Lutinwa (1937-1974).

Mutakubwa aliondolewa na wakoloni mwaka 1937 na hakuwa na mtoto. Hivyo ndugu yake Mboneko aitwaye Nestor Lutinwa alichaguliwa kumrithi, na akatawala mpaka Nyerere alipofutilia mbali utawala wa Bakama.

Katika Kanyigo nzima mtu pekee aliyezaliwa wakati wa utawala wa Mutahangarwa amebaki mmoja tu, naye ni mzee Ta Baltholomayo wa Bugombe. Huyu kuzaliwa kwake ni datable kwani nilipomhoji aliniambia kuwa wakati Mutahangarwa anafariki alikuwa na umri wa kuanza shule wa watoto wa siku hizi.

Sababu ya kuondolewa kwa Mutakubwa ni ufuska uliokithiri, ukiwemo ule wa kulazimisha. Mama yake Muchureza alijaribu kumkanya lakini hakusikia. Hivyo alikwenda kumuomba DC wa kikoloni amsaidie kumkanya. Badala ya kumkanya DC alimfukuza, kwani kwa mzungu kubaka ni dhambi isiyosameheka. Lakini DC hakuelewa kuwa Mukama hawezi kuwa na hatia ya kumbaka mwanamke au kufanya uasherati, kwani kwa mila zetu wanawake wote ni mali ya Mukama. Hivyo watu wakawa wanamuimba Muchureza kuwa ni kilimi nyakwelega ayagambiile omujungu ati Omukama nasiyana. Maana yake, wimbo ulikuwa unamsuta Muchureza kwa kujichongea (okwelega) bila sababu ya msingi.

Mutakubwa, baada ya kufukuzwa, alimalizia maisha yake pale Kigarama, kwa Edward Kasano, kwani baba yake Edward alikuwa tumbo moja na Mutakubwa, wote wakiwa ni watoto wa Muchureza. Alifariki mwaka 1948 na kuzikwa pale Kigarama. Jambo la ajabu nililoshuhudia ni kwamba wazee pale kijijini waliendelea kumpa heshima kama Mukama wakimwamkia Habuka Izoba, Habuka Lugaba, Habuka Nyakusinga, nk.

Baadaye nilikuja kuelewa kuwa mtu akishasimikwa kama Mukama anakuwa na namna ya uungu (semi-divine). Hivyo ukimnyima heshima yake unaweza ukapatwa na mabaya.
By Emanuel Kamuzora
 
Nitarudi ngoja niende chooni kwanza 🤸‍♀️🤸‍♀️
 
Katerero hujailezea, kuna ngono nayo sijaiona, Ukimwi nao sijauona, tetemeko, rambi rambi yaani vingi umeviacha.

Hayo makabila kila mtu anayo nyinyi ni wakabila kama wa kule Rwanda-Burundi. Kamkoa kamasikini kama majimbo ya ccm alafu sijui matajiri wa kujidai kama Kaijage
 
Nimekumbuka kuisoma mwaka jana.. nilipotumiwa link.. haikunihusu nikasoma nikapita.. kama navyopita post yako pia

Sentensi ya kusema miaka ya 40 ilinikumbusha.. google nayo kwa kasentensi kamoja umerusha.. ikanipeleka kwa kusechi maneno uliyochukua bila kunukuu ulipoyapata..😁
1537889105927.jpg
 
Nimekumbuka kuisoma mwaka jana.. nilipotumiwa link.. haikunihusu nikasoma nikapita.. kama navyopita post yako pia

Sentensi ya kusema miaka ya 40 ilinikumbusha.. google nayo kwa kasentensi kamoja umerusha.. ikanipeleka kwa kusechi maneno uliyochukua bila kunukuu ulipoyapata..[emoji16]
View attachment 877653
Huyu jamaaa kakopiiii kumbee[emoji1] [emoji1] [emoji1] wahaya bhana
 
Back
Top Bottom