Ijue Vita iliyopiganwa miaka therathini (thirty years' war)

Ijue Vita iliyopiganwa miaka therathini (thirty years' war)

marco polo jr

JF-Expert Member
Joined
Mar 31, 2020
Posts
362
Reaction score
1,771
Huku tukiendelea kujikinga na Corona nimeona kidogo tujikumbushe historia kidogo ya hii Vita maarufu huko barani ulaya .chanzo Cha Vita ni kushindwa kwa mkutano wa amani(An important cause of the war was the fairlure of peace of Ausburg to settle all the reliogius problem of Germany.)kuhusu mkutano huu uliwatambua pekee Lutheran huku wakalvini wakiaachwa pia ulishindwa katika kugawa Mali za kanisa baina ya wakatoliki na Lutheran sababu nyingine ni viongozi wengi walipenda kuingia katika Vita hivi ili kujipatia Mali . Germany ndio ilikuwa uwanja mkuu wa Vita hi ya miaka therathini ambayo ilianzia bohemia .Kwa Mara ya Kwanza Vita vilipigwa baina ya prostentant na Catholic .lakini baadaye nchi zikaingia vitani .kwa Mara ya Kwanza Denmark aliingia upande wa Protestant mwaka 1625 . Lakini majeshi ya Catholic yaliwashinda yakiwa chini ya kamanda Albrecht wellenstein yakawafukuza wadenimark .Vita haikushia hapo .Mwaka 1630 Sweden wakaja kuwasaidia Protestant ingiwa majeshi ya Sweden chini ya mfalme wait Gustavus Adolphus kupata ushindi Mara kadhaa mfalme wa Sweden aliuawa katika Vita hivyo mwaka 1632.when it seemed that the fighting had ended , suddenly France entered the war on side of Protestants.patamu apo Cha kushangaza kipindi France alikuwa ni pure Catholics county na uongozi ulikuwa chini ya cardinal Richelieu .baada ya Vita vikali France na washirika wake wakashinda na Vita ikaisha mwaka 1648 baada ya kupigwa kwa miaka therathini kwa kusaini mkutano wa amani Ali maarufu peace of Westphalia . Baada ya Vita France ndio akawa mbabe wa ulaya nzima baada ya kumtwanga mhispaniaola kwa hizi dini Kuna watu walimwaga damu zao wakizigania .Ajabu Leo Mambo waliyopigania kwa kumwaga damu Leo watu wanafanya kinyume .shukrani Sana munakarishwa kwa maoni na maswali .Marco Polo jr
 
Huku tukiendelea kujikinga na Corona nimeona kidogo tujikumbushe historia kidogo ya hii Vita maarufu huko barani ulaya .chanzo Cha Vita ni kushindwa kwa mkutano wa amani(An important cause of the war was the fairlure of peace of Ausburg to settle all the reliogius problem of Germany.)kuhusu mkutano huu uliwatambua pekee Lutheran huku wakalvini wakiaachwa pia ulishindwa katika kugawa Mali za kanisa baina ya wakatoliki na Lutheran sababu nyingine ni viongozi wengi walipenda kuingia katika Vita hivi ili kujipatia Mali . Germany ndio ilikuwa uwanja mkuu wa Vita hi ya miaka therathini ambayo ilianzia bohemia .Kwa Mara ya Kwanza Vita vilipigwa baina ya prostentant na Catholic .lakini baadaye nchi zikaingia vitani .kwa Mara ya Kwanza Denmark aliingia upande wa Protestant mwaka 1625 . Lakini majeshi ya Catholic yaliwashinda yakiwa chini ya kamanda Albrecht wellenstein yakawafukuza wadenimark .Vita haikushia hapo .Mwaka 1630 Sweden wakaja kuwasaidia Protestant ingiwa majeshi ya Sweden chini ya mfalme wait Gustavus Adolphus kupata ushindi Mara kadhaa mfalme wa Sweden aliuawa katika Vita hivyo mwaka 1632.when it seemed that the fighting had ended , suddenly France entered the war on side of Protestants.patamu apo Cha kushangaza kipindi France alikuwa ni pure Catholics county na uongozi ulikuwa chini ya cardinal Richelieu .baada ya Vita vikali France na washirika wake wakashinda na Vita ikaisha mwaka 1648 baada ya kupigwa kwa miaka therathini kwa kusaini mkutano wa amani Ali maarufu peace of Westphalia . Baada ya Vita France ndio akawa mbabe wa ulaya nzima baada ya kumtwanga mhispaniaola kwa hizi dini Kuna watu walimwaga damu zao wakizigania .Ajabu Leo Mambo waliyopigania kwa kumwaga damu Leo watu wanafanya kinyume .shukrani Sana munakarishwa kwa maoni na maswali .Marco Polo jr
Kiswanglish

Sent from my Infinix X624 using Tapatalk
 
Ahsante mheshimiwa!!!

Historia ni tamu sana, kweli wazungu hawakupenda tujue baadhi ya mambo yao ndo maana husikii hii vita ikisemwa semwa.
japo umeandika kwa kifupi lakini nimekuelewa.

Kuhusu kishwanglish nadhani ni kujiendekeza tu (mawazo yangu) tukiamua kuongea kiswahili halisi tunaweza maana ni lugha yetu, hivyo sisi (mimi, wewe na wenzetu wenye nia njema) ndo wenye kazi ya kutafuta misamiati mipya.
 
Ahsante mheshimiwa!!!

Historia ni tamu sana, kweli wazungu hawakupenda tujue baadhi ya mambo yao ndo maana husikii hii vita ikisemwa semwa.
japo umeandika kwa kifupi lakini nimekuelewa.

Kuhusu kishwanglish nadhani ni kujiendekeza tu (mawazo yangu) tukiamua kuongea kiswahili halisi tunaweza maana ni lugha yetu, hivyo sisi (mimi, wewe na wenzetu wenye nia njema) ndo wenye kazi ya kutafuta misamiati mipya.
shukrani Sana
 
Vita ya Mwamlima na Cheyo ililipasua kanisa la Moravian Mbeya, Hadi Augustine Lyatonga Mrema akiwa Waziri Mambo ya Ndani alipokuja kuumaliza mgogoro huo
 
Asante kwa kuleta mada lakini naona maelezo hapa kwenye wikipedia yanaeleweka kirahisi zaidi? Vita ya miaka 30 - Wikipedia, kamusi elezo huru
Vita ya miaka 30
Vita ya miaka 30
ilipigwa kati ya miaka 1618 hadi 1648. Ilikuwa vita ya Kiulaya lakini mapigano yake yalitokea hasa katika Ujerumani kwenye eneo la Dola Takatifu la Kiroma.

Madola ya Ujerumani yalipigana kati yao, na nchi za nje zilishiriki zikiwemo Hispania, Ufaransa, Uswidi, Uholanzi na Denmark.

Vita ilileta uharibifu kupita kiasi kwa ajili ya Ujerumani kushinda vita zote zilizofuata katika historia. Hukumbukwa hadi leo.

Hali ya kisiasa kabla ya vita
Ujerumani ilikuwa sehemu kubwa ya Dola Takatifu la Kiroma pamoja na majimbo ambayo leo ni Ucheki, Uholanzi, Uswisi, Ufaransa ya magharibi, Italia ya kaskazini na Austria. Dola Takatifu ilikuwa kama maungano ya madola madogo zaidi chini ya Kaisari.

Mkuu alikuwa Kaisari aliyetoka katika nasaba ya Habsburg akiwa mtawala wa Austria hasa na madaraka yake juu ya Dola Takatifu kwa jumla yalikuwa madogo. Maeneo mengine yalijitegemea kwa kiasi kikubwa chini ya watawala wao wa kikabaila.

Miaka 100 kabla ya vita matengenezo ya Kiprotestanti yalienea katika Ujerumani na sehemu ya madola ilipokea madhehebu mapya, lakini wengine walibaki Wakatoliki. Madola mengi yalisisitiza ya kwamba wananchi wote wafuate dhehebu moja tu, ama Ukatoliki ama Ulutheri; hapakuwa na uhuru wa dini kwa kila raia.

Uhusiano kati ya madhehebu ya Kikristo ulikuwa mbaya kwa muda mrefu. Karibu katika kila nchi Wakristo walilazimishwa kufuata madhehebu rasmi. Ikiwa mtawala fulani aliona vema kukubali mawazo ya Martin Luther mapadri wote walipewa chaguo la kufuata Ulutheri au kuhama nchi. Vilevile baada ya kifo chake ikiwa mtawala aliyefuata alikuwa na msimamo tofauti, mapadri wakarudi na wachungaji wa Kiinjili wakafukuzwa.

Raia hawakuulizwa wenyewe wanasadiki nini, isipokuwa katika miji iliyojitawala na kuwa na utaratibu wa kidemokrasia. Lakini hata mijini huko haikuwa kawaida kuruhusu madhehebu mawili mahali pamoja.

Mafundisho ambayo kwetu leo yanaonekana kuwa na tofauti ndogo yaliweza kumfikisha mtu gerezani au hata kifoni.

Uhusiano mbaya ulikuwepo vilevile kati ya wafuasi wa Luther na Wareformati. Katekisimu zao zilitumika kama bendera. Walishutumiana kuwa wazushi wasioelewa vizuri kiini cha imani.

Fitina ya kidini katika Bohemia
Vita ilianza kama fitina kati ya Kaisari aliyekuwa Mkatoliki Mwaustria na maungano ya madola ya Kiprotestanti ndani ya Dola Takatifu. Chanzo kilikuwa uasi wa makabaila wa Kiprotestanti katika jimbo la Bohemia dhidi ya siasa ya Kaisari Ferdinand II aliyechaguliwa pia kuwa mfalme wa Bohemia.

Ferdinand alikataa kukubali uhuru wa dini ulioahidiwa na mtangulizi wake kwa ajili ya Bohemia. Fitina hii ilikuwa vita baada ya gavana wa Kaisari kutupwa nje ya dirisha la chumba cha mkutano mjini Praha tarehe 23 Mei 1618. Wakubwa wa Bohemia waliendela kutamka ya kwamba Ferdinand si mfalme wao tena, wakamchagua kabaila wa Palentino kama mfalme mpya.

Kaisari alichukua silaha na kwenye mapigano ya kwanza tarehe 8 Novemba 1619 karibu na mji wa Praha waasi wa Bohemia walishindwa. Makabaila wengi wa Kiprotestanti kutoka madola mengine ya Ujerumani waliamua kuwasaidia wenzao wa Bohemia. Vita hii ilielekea kwisha kwa ushindi wa Kaisari mnamo 1623.

Uswidi kusaidia Waprotestanti
Hapo nchi jirani zilijiunga na vita. Nchi za Skandinavia zilifuata Uprotestanti na watawala wao waliamua kuwasaidia wenzao Wajerumani. Wadenmark kwanza halafu Waswidi walifika kwa wanajeshi wengi. Mfalme Gustav Adolf wa Uswidi alishinda jeshi la Kaisari mara kadhaa hadi alipouawa kwenye mapigano ya Lützen tarehe 16 Novemba 1632.

Kuingilia kwa Ufaransa
Baada ya kuona ya kwamba Kaisari aliendelea kusogea mbele, mfalme wa Ufaransa alijiunga na Uswidi akashiriki katika vita tangu mwaka 1635. Nia yake ilikuwa hasa kuzuia enzi ya nasaba ya Habsburg iliyotawala Hispania ikashika pia Austria pamoja na cheo cha Kaisari wa Dola Takatifu la Kiroma.

Hivyo vita iliyoanza kama mapigano ya kidini katika dola moja la Ujerumani iliendelea kuwa vita ya Kiulaya ambako nchi ya Wakatoliki kama Ufaransa ilishikamana na Uswidi ya Kiprotestanti dhidi ya Kaisari Mkatoliki.

Vita ilileta uharibifu mkubwa mno katika Ujerumani. Kuna makadirio ya kwamba karibu theluthi moja ya wakazi wote walikufa kutokana na mauaji, njaa na magonjwa. Katika maeneo ya Ujerumani ya Kusini zaidi ya nusu ya watu walipotea.

Wanajeshi walikuwa askari wa kukodiwa ambao mara nyingi hawakulipwa bali walipewa uhuru wa kupora chochote walichotaka.

Amani ya Westfalia
Uchofu ulileta majadiliano juu ya amani. Mwaka 1648 wawakilishi wa wafalme walipatana katika amani ya Westfalia kanuni za amani.

  • Madhehebu matatu yaliyokubaliwa Ulaya ni Wakatoliki, Walutheri na Wareformed.
  • Kila mtawala aliamua kwa dola lake ni dini ipi itafuatwa lakini raia walikuwa na haki ya kutoka katika nchi kama mtawala alikataa dini yao. Sheria ilikuwa: "Cuius regio, eius religio" (mwenye nchi ni mwenye kuamua dini)
  • Uholanzi na Uswisi zilitoka katika Dola Takatifu la Kiroma kama nchi huru za pekee.
  • Mfalme wa Uswidi alitwaa maeneo makubwa katika Ujerumani ya Kaskazini

Mapatano hayo yaliunda ramani ya kimadhehebu kule Ulaya yenye maeneo ya Wakatoliki, Walutheri au Wareformati watupu.

Jumuiya ndogo ziliendelea kugandamizwa wakapata ustahimilivu mahali pachache. Hivyo wafuasi wa madhehebu madogo walilazimika kuficha imani yao au kuhamahama katika Ulaya.

Wakati ule nafasi mpya ilitokea: Mfalme wa Uingereza alikuwa na makoloni Marekani lakini alikosa watu. Akatafuta walowezi kwa ajili ya makoloni yake akiwaahidia wote kwamba watapata shamba pamoja na uhuru wa dini. Hivyo watu kutoka nchi nyingi za Ulaya walianza kuhamia Marekani, hasa wale waliokosa uhuru huo.

Mpaka leo nchi mbalimbali za Ulaya zinafuata hasa madhehebu moja, na Marekani ina madhehebu makubwa ambayo hayana wafuasi wengi Ulaya, k.mf. Wabatisti.
 
Asante kwa kuleta mada lakini naona maelezo hapa kwenye wikipedia yanaeleweka kirahisi zaidi? Vita ya miaka 30 - Wikipedia, kamusi elezo huru
Vita ya miaka 30
Vita ya miaka 30
ilipigwa kati ya miaka 1618 hadi 1648. Ilikuwa vita ya Kiulaya lakini mapigano yake yalitokea hasa katika Ujerumani kwenye eneo la Dola Takatifu la Kiroma.

Madola ya Ujerumani yalipigana kati yao, na nchi za nje zilishiriki zikiwemo Hispania, Ufaransa, Uswidi, Uholanzi na Denmark.

Vita ilileta uharibifu kupita kiasi kwa ajili ya Ujerumani kushinda vita zote zilizofuata katika historia. Hukumbukwa hadi leo.

Hali ya kisiasa kabla ya vita
Ujerumani ilikuwa sehemu kubwa ya Dola Takatifu la Kiroma pamoja na majimbo ambayo leo ni Ucheki, Uholanzi, Uswisi, Ufaransa ya magharibi, Italia ya kaskazini na Austria. Dola Takatifu ilikuwa kama maungano ya madola madogo zaidi chini ya Kaisari.

Mkuu alikuwa Kaisari aliyetoka katika nasaba ya Habsburg akiwa mtawala wa Austria hasa na madaraka yake juu ya Dola Takatifu kwa jumla yalikuwa madogo. Maeneo mengine yalijitegemea kwa kiasi kikubwa chini ya watawala wao wa kikabaila.

Miaka 100 kabla ya vita matengenezo ya Kiprotestanti yalienea katika Ujerumani na sehemu ya madola ilipokea madhehebu mapya, lakini wengine walibaki Wakatoliki. Madola mengi yalisisitiza ya kwamba wananchi wote wafuate dhehebu moja tu, ama Ukatoliki ama Ulutheri; hapakuwa na uhuru wa dini kwa kila raia.

Uhusiano kati ya madhehebu ya Kikristo ulikuwa mbaya kwa muda mrefu. Karibu katika kila nchi Wakristo walilazimishwa kufuata madhehebu rasmi. Ikiwa mtawala fulani aliona vema kukubali mawazo ya Martin Luther mapadri wote walipewa chaguo la kufuata Ulutheri au kuhama nchi. Vilevile baada ya kifo chake ikiwa mtawala aliyefuata alikuwa na msimamo tofauti, mapadri wakarudi na wachungaji wa Kiinjili wakafukuzwa.

Raia hawakuulizwa wenyewe wanasadiki nini, isipokuwa katika miji iliyojitawala na kuwa na utaratibu wa kidemokrasia. Lakini hata mijini huko haikuwa kawaida kuruhusu madhehebu mawili mahali pamoja.

Mafundisho ambayo kwetu leo yanaonekana kuwa na tofauti ndogo yaliweza kumfikisha mtu gerezani au hata kifoni.

Uhusiano mbaya ulikuwepo vilevile kati ya wafuasi wa Luther na Wareformati. Katekisimu zao zilitumika kama bendera. Walishutumiana kuwa wazushi wasioelewa vizuri kiini cha imani.

Fitina ya kidini katika Bohemia
Vita ilianza kama fitina kati ya Kaisari aliyekuwa Mkatoliki Mwaustria na maungano ya madola ya Kiprotestanti ndani ya Dola Takatifu. Chanzo kilikuwa uasi wa makabaila wa Kiprotestanti katika jimbo la Bohemia dhidi ya siasa ya Kaisari Ferdinand II aliyechaguliwa pia kuwa mfalme wa Bohemia.

Ferdinand alikataa kukubali uhuru wa dini ulioahidiwa na mtangulizi wake kwa ajili ya Bohemia. Fitina hii ilikuwa vita baada ya gavana wa Kaisari kutupwa nje ya dirisha la chumba cha mkutano mjini Praha tarehe 23 Mei 1618. Wakubwa wa Bohemia waliendela kutamka ya kwamba Ferdinand si mfalme wao tena, wakamchagua kabaila wa Palentino kama mfalme mpya.

Kaisari alichukua silaha na kwenye mapigano ya kwanza tarehe 8 Novemba 1619 karibu na mji wa Praha waasi wa Bohemia walishindwa. Makabaila wengi wa Kiprotestanti kutoka madola mengine ya Ujerumani waliamua kuwasaidia wenzao wa Bohemia. Vita hii ilielekea kwisha kwa ushindi wa Kaisari mnamo 1623.

Uswidi kusaidia Waprotestanti
Hapo nchi jirani zilijiunga na vita. Nchi za Skandinavia zilifuata Uprotestanti na watawala wao waliamua kuwasaidia wenzao Wajerumani. Wadenmark kwanza halafu Waswidi walifika kwa wanajeshi wengi. Mfalme Gustav Adolf wa Uswidi alishinda jeshi la Kaisari mara kadhaa hadi alipouawa kwenye mapigano ya Lützen tarehe 16 Novemba 1632.

Kuingilia kwa Ufaransa
Baada ya kuona ya kwamba Kaisari aliendelea kusogea mbele, mfalme wa Ufaransa alijiunga na Uswidi akashiriki katika vita tangu mwaka 1635. Nia yake ilikuwa hasa kuzuia enzi ya nasaba ya Habsburg iliyotawala Hispania ikashika pia Austria pamoja na cheo cha Kaisari wa Dola Takatifu la Kiroma.

Hivyo vita iliyoanza kama mapigano ya kidini katika dola moja la Ujerumani iliendelea kuwa vita ya Kiulaya ambako nchi ya Wakatoliki kama Ufaransa ilishikamana na Uswidi ya Kiprotestanti dhidi ya Kaisari Mkatoliki.

Vita ilileta uharibifu mkubwa mno katika Ujerumani. Kuna makadirio ya kwamba karibu theluthi moja ya wakazi wote walikufa kutokana na mauaji, njaa na magonjwa. Katika maeneo ya Ujerumani ya Kusini zaidi ya nusu ya watu walipotea.

Wanajeshi walikuwa askari wa kukodiwa ambao mara nyingi hawakulipwa bali walipewa uhuru wa kupora chochote walichotaka.

Amani ya Westfalia
Uchofu ulileta majadiliano juu ya amani. Mwaka 1648 wawakilishi wa wafalme walipatana katika amani ya Westfalia kanuni za amani.

  • Madhehebu matatu yaliyokubaliwa Ulaya ni Wakatoliki, Walutheri na Wareformed.
  • Kila mtawala aliamua kwa dola lake ni dini ipi itafuatwa lakini raia walikuwa na haki ya kutoka katika nchi kama mtawala alikataa dini yao. Sheria ilikuwa: "Cuius regio, eius religio" (mwenye nchi ni mwenye kuamua dini)
  • Uholanzi na Uswisi zilitoka katika Dola Takatifu la Kiroma kama nchi huru za pekee.
  • Mfalme wa Uswidi alitwaa maeneo makubwa katika Ujerumani ya Kaskazini

Mapatano hayo yaliunda ramani ya kimadhehebu kule Ulaya yenye maeneo ya Wakatoliki, Walutheri au Wareformati watupu.

Jumuiya ndogo ziliendelea kugandamizwa wakapata ustahimilivu mahali pachache. Hivyo wafuasi wa madhehebu madogo walilazimika kuficha imani yao au kuhamahama katika Ulaya.

Wakati ule nafasi mpya ilitokea: Mfalme wa Uingereza alikuwa na makoloni Marekani lakini alikosa watu. Akatafuta walowezi kwa ajili ya makoloni yake akiwaahidia wote kwamba watapata shamba pamoja na uhuru wa dini. Hivyo watu kutoka nchi nyingi za Ulaya walianza kuhamia Marekani, hasa wale waliokosa uhuru huo.​

Mpaka leo nchi mbalimbali za Ulaya zinafuata hasa madhehebu moja, na Marekani ina madhehebu makubwa ambayo hayana wafuasi wengi Ulaya, k.mf. Wabatisti.
shukrani Sana kwa kujazia nondo
 
  • Thanks
Reactions: Sax
Hiyo michache,,Iran vs Roman empire,miaka 900
Samahani Mkuu, urudie historia kidogo.
Ni kweli Waroma wa Kale na Waajemi wa Kale walipigana kivita katika muda wa karne kadhaa. Lakini haikuwa vita moja! Katikati kulikuwa na vipindi virefu vya amani na pia ushirikiano mwema.
Upande mmoja kulikuwa ma Jamhuri ya Roma, baadaye Dola la Roma.
Upande wa Uajemi kulikuwa kwanza milki ya Waparthi, baadaye Wasasanidi

Mapigano ya kwanza yalitokea miaka 53 kabla ya Kristo, baada ya Roma kueneza utawala wake Syria. Mwanasiasa na jemadari Mroma Crassus (aliyegawana utawala juu ya Roma na Julius Caesar) alitaka ushindi ili aweza kulingana na Caeasar (aliyewahi kuvamia Gallia=Ufaransa). Alishambulia Waparthi katika "Syria" (leo mipaka ya Syria, Uturuki, Iraki) akashindwa pale Carrhae (Harran ya leo). Vita ilikwisha wakati wa Augusto (yule Kaisari ya historia ya Krismasi) mwaka 30 KK na Waroma walikubali mto Frati kuwa mpaka baina ya milki hizi mbili.
Kulikuwa tena na mapigano hapa na pale wakati wa makaisari Nero 54–63 baada ya Kristo, Traiano (114–117), Marko Aurelio 161–166), Septimi Sever (197/198) na Caracalla (216–18) pamoja na vipindi vya amani tena.
Baada ya kupinduliwa na Waparthi ni Wasasanidi waliotawala Iran = Uajemi hadi mwaka 632.
Katika kipindi hiki vita na ushirikiano vilibadilishana mara kwa mara. Katika kipindi hiki Dola la Roma la awali liliporomoka likaishia katika magharibi (=Ulaya) mwaka 476 likabaki katika Mashariki tu (mji mkuu Bizanti = Konstantinopoli, leo Istanbul, Uturuki).
Bizanti iliendelea na vita au ushirikiano na Uajemi, kipindi kibaya kilitokea kuanzia mwaka 603. Wakati ule yalitokea mapinduzi katika Bizanti (=Roma Mashariki) na jemadari alimpindua Kaisari. Mfalme wa Uajemi aliingilia kati ili kumrudisha mwana wa Kaisari mamlakani. Viti hiyo iliendelea zaidi ya miaka 20; toke lake lilikuwa nguvu za Uajemi na Roma Mashariki zilikwisha kabisa. Waajemi walifaulu kuteka Yerusalemu na kubomoa kanisa la KAburi la Yesu walishambulia hadi Bizanti=Konstantinopoli (Istanbul leo). waroma waliweza kuwarudisha hadi mji mkuu wa Uajemi (iliyokuwa nchini Iraki ya leo). 628 ilileta amani, lakini pande zote mbili zilikuwa ziliharibu uchumi na nguvu ya kijeshi.
Wadhaifu hao walikuwa tayari kushmauliwa na Waarbu Waislamu. Tangu 634 Waaabu Waislamu (miaka 2 baada ya Kifo cha Muhamad) walivamia Syria ya Kiroma pamja na Iraki ya Kiajemi.- Adui huyu mpya alikuta maadui waliodhoofika.
Uajemi wote ilitekwa na Waarabu na kuwa sehemu ya milki ya Waislamu.
Roma ya Mashariki = Bizanti ilipaswa kuacha Syria lakini iliweza kujitetea katika sehemu za Utrurukiwa baadaye kwa karne 6.

Hitimisho: ni kweli vita ya miaka 30 pale Ujerumani haikuwa vita ndefu katika katika historia.
Lakini ilikuwa "juzijuzi" maana miaka 4300 iliyopiat tu. Ilikuwa vita mbaya sana an matokeo kadhaa yanaonekana hadi leo.
 
Samahani Mkuu, urudie historia kidogo.
Ni kweli Waroma wa Kale na Waajemi wa Kale walipigana kivita katika muda wa karne kadhaa. Lakini haikuwa vita moja! Katikati kulikuwa na vipindi virefu vya amani na pia ushirikiano mwema.
Upande mmoja kulikuwa ma Jamhuri ya Roma, baadaye Dola la Roma.
Upande wa Uajemi kulikuwa kwanza milki ya Waparthi, baadaye Wasasanidi

Mapigano ya kwanza yalitokea miaka 53 kabla ya Kristo, baada ya Roma kueneza utawala wake Syria. Mwanasiasa na jemadari Mroma Crassus (aliyegawana utawala juu ya Roma na Julius Caesar) alitaka ushindi ili aweza kulingana na Caeasar (aliyewahi kuvamia Gallia=Ufaransa). Alishambulia Waparthi katika "Syria" (leo mipaka ya Syria, Uturuki, Iraki) akashindwa pale Carrhae (Harran ya leo). Vita ilikwisha wakati wa Augusto (yule Kaisari ya historia ya Krismasi) mwaka 30 KK na Waroma walikubali mto Frati kuwa mpaka baina ya milki hizi mbili.
Kulikuwa tena na mapigano hapa na pale wakati wa makaisari Nero 54–63 baada ya Kristo, Traiano (114–117), Marko Aurelio 161–166), Septimi Sever (197/198) na Caracalla (216–18) pamoja na vipindi vya amani tena.
Baada ya kupinduliwa na Waparthi ni Wasasanidi waliotawala Iran = Uajemi hadi mwaka 632.
Katika kipindi hiki vita na ushirikiano vilibadilishana mara kwa mara. Katika kipindi hiki Dola la Roma la awali liliporomoka likaishia katika magharibi (=Ulaya) mwaka 476 likabaki katika Mashariki tu (mji mkuu Bizanti = Konstantinopoli, leo Istanbul, Uturuki).
Bizanti iliendelea na vita au ushirikiano na Uajemi, kipindi kibaya kilitokea kuanzia mwaka 603. Wakati ule yalitokea mapinduzi katika Bizanti (=Roma Mashariki) na jemadari alimpindua Kaisari. Mfalme wa Uajemi aliingilia kati ili kumrudisha mwana wa Kaisari mamlakani. Viti hiyo iliendelea zaidi ya miaka 20; toke lake lilikuwa nguvu za Uajemi na Roma Mashariki zilikwisha kabisa. Waajemi walifaulu kuteka Yerusalemu na kubomoa kanisa la KAburi la Yesu walishambulia hadi Bizanti=Konstantinopoli (Istanbul leo). waroma waliweza kuwarudisha hadi mji mkuu wa Uajemi (iliyokuwa nchini Iraki ya leo). 628 ilileta amani, lakini pande zote mbili zilikuwa ziliharibu uchumi na nguvu ya kijeshi.
Wadhaifu hao walikuwa tayari kushmauliwa na Waarbu Waislamu. Tangu 634 Waaabu Waislamu (miaka 2 baada ya Kifo cha Muhamad) walivamia Syria ya Kiroma pamja na Iraki ya Kiajemi.- Adui huyu mpya alikuta maadui waliodhoofika.
Uajemi wote ilitekwa na Waarabu na kuwa sehemu ya milki ya Waislamu.
Roma ya Mashariki = Bizanti ilipaswa kuacha Syria lakini iliweza kujitetea katika sehemu za Utrurukiwa baadaye kwa karne 6.

Hitimisho: ni kweli vita ya miaka 30 pale Ujerumani haikuwa vita ndefu katika katika historia.
Lakini ilikuwa "juzijuzi" maana miaka 4300 iliyopiat tu. Ilikuwa vita mbaya sana an matokeo kadhaa yanaonekana hadi leo.
Ni kweli hiyo Ni Vita ya karibuni,maana miaka ya 1600 Ni karibuni,ukirudi miaka 3500 nyuma ,enzi za akina Babylon,Asyria,nchi za ulaya zilikuwa hazijaorganise Jamii zao kuform powerful empires,mpaka baadae enzi za akina Alexandra the great,
Iran vs Rome ilikuwa Ni series Kama ilivyo tu Vita ya marekani na taleban,
Sio kwamba kila dakika wanakuwa wanafight,
Same applied kwa crusade war,nayo ilukuwa in series,
 
Back
Top Bottom