Ikifika 2030 hali haitakuwa nzuri kwa baadhi ya wanawake

Uko sahihi madam.
 
Wanaume bado wanaoa kwa Sababu jamii imeweka utaratibu wa unyumba wa mwanaume na mwanamke na kupata watoto kupitia makubaliano rasmi yanayopitishwa na wazee wa pande zote mbili yaani NDOA. Jamii imekubaliana kuwa Kufanya ngono kabla ya ndoa ni Uzinzi na ni dhambi na ni jambo lenye kuharibu kizazi.
HAUJALIFIKIRIA HILI KWA SABABU KWAKO WEWE HAKUNA KITU KINACHOITWA MAADILI UNAKIELEWA.
 
Unaandika nadharia na uongo mno napata wasiwasi malengo yako ni yepi kwa jamii inayojifunza kutoka kwako.

Moja Mwanamke ana vingi ambavyo hawezi kuvipata isipokuwa katika ndoa. Mwanaume anayemuhudumia Mwanamke ambae hajamuoa ana mipaka katika huduma hizo.

Wanaohangaikia ndoa Kwa waganga na Makanisani ni wanawake na hatuoni wanaume wapo huko Wanahangaika kisha uje useme uhitaji wa ndoa kwa mwanamke ni mdogo. Huna ujualo.

Pili Wanawake ndio wahusika wakubwa wa masuala ya kisaikolojia na hapa unajaribu kudanganya watu(labda ni akili za BALIMI) Mwanamke yupo more emotional Anahitaji kufarijiwa na hachelewi kulia na ni mwenye hisia za waziwazi.
Mwanaume ni shupavu anaweza kudhibiti machozi yake hisia zake na machungu yake ameumbwa hivyo mwanamke kinyume chake ni Dhaifu katika hayo yote. Wewe unalazimisha kuvaa viatu kinyume na size yako.

Tatu hisia za mwanamke zinatatuliwa na yule mwenye hisia nae (anayempenda kutoka moyoni) mda Mwengine hata wazazi hawatoshi kumfariji Mwanamke Isipokuwa Yule mwanaume anayempenda kihisia. Acha kupotosha umma.
 
Na ndio maana nasema sababu kubwa inayompeleka mwanamke kwenye ndoa ni financial security hizo nyingine ni minor reasons mwanamke akikosa hiko kwenye ndoa ana uwezo wa kukipata nje ya ndoa kwa kujitafutia mwenyewe pesa na mali zake,
Hawa wanaotafuta wanaume na wana uchumi wao wanataka nini?
ila mwanaume sababu kubwa inayompeleka kwenye ndoa ni mahitaji ya kisaikolojia na mahitaji haya ni ngumu kuyapata nje ya ndoa au mahusiano rasmi na mwanamke yani kwa kifupi hayo mahitaji huwezi kuyapata kwa kununua malaya,
Nadharia zako za ajabu.
Malaya hawezi kuja nyumbani kupika na kufua kila siku malaya hawezi kunizalia watoto malaya siwezi kumtambulisha nyumbani au kwa marafiki kuwa ni Mwenza wangu, Malaya hatuwezi kujenga Stable family. Mtu pekee anaeweza kuyafanya hayo yote ni mke. Ndio mana tunaoa.
Miaka 25 anasoma form ngapi? Jamii ipi hiyo kwao ndoa ni kuanzia miaka 35+.??

Kama ni Pressure ipo kwa wote ila miaka ya 20+ Binti ana soko kubwa la wanaume haoni haja ya kuwa katika kifungo cha ndoa sababu atapoteza uhuru wake wa kufanya anasa. Ikifika hiyo miaka ya 35+ soko linapungua au kufa kabisa ndio akili inarudi.
Tunahitaji familia iliyo Stable na Kufuata tamaduni zetu za kidini Katika Masuala ya familia. Mtu ambaye ana malengo mazuri ya familia na kizazi lazima achague Mwanamke mtiifu amuweke ndani na iwe rasmi kwa wazazi. Wengine wanaoa kwa sababu hawataki kuwa wazinifu.
 
Haha ukweli wanaujua ila wanajikaza tu humu mradi wasionekane wameshindwa hoja, we si unaona walivyopoteana hadi wanaanza kufukua comments za nyuma, siku zote ukiona mtu anahangaika na mtoa hoja ujue kashashindwa hoja huyo
Sisi tunafahamu fika ninyi wanawake wenye itikadi za ki Feminism ni aina gani ya wanawake tabia zenu na maadili.

Huenda wengine wakiona unaandika paragraphs wanaona ni mtu wa maana kabisa ila in reality ninyi ni aina ya wanawake wa hovyo kabisa katika jamii.

Tukipata evidence kama hizo kutoka kwenye Maneno yako mwenyewe tunatumia kuonesha watu kuwa ninyi ni wanawake wa anasa na maisha ya Starehe sasa ndoa hamuziwezi ndoa ni jambo la kimalengo zaidi ninyi mna akili bado za ku appreciate miili yenu na Maumbile yenu. We knew this very early.
 
Ukiachana na mambo mengine uliyoyaandika ambayo hayana uhalisia.

At least unakubali kuwa Utiifu wa mwanamke kwa mwanaume ni zaidi ya matakwa ya Binadamu yaani ni jambo la asili. Tofauti na mnywa balimi Jadda.

Nakuelewa unasisitiza kuhusu kuwajibika na kumpenda na kumheshimu mume mkewe. Hilo ni sahihi na hatujakataa.

Ila Hoja ni kwamba suala la Wanaume wachache au wengi kukosa mapenzi na uwajibikaji katika familia zao sio jambo lililopaswa kushughulikiwa kwa Kupiga vita utiifu na Kuvunja vunja misingi ya mgawanyo wa majukumu ya kijamii kati ya mwanaume na mwanamke katika jamii. HAPA NDIO KOSA LILIPO.

Kwa Sababu hata leo ikitokea Wanaume wakawa wanawajibika kama mnavyotaka na wanawapenda na kuwaheshimu kama mnavyodai bado kuirudisha jamii hii kwenye utiifu na mgawanyo mzuri wa majukumu ya kijamii kati ya mwanaume na mwanamke ni jambo Gumu sana.

Yaani halitokuja automatically bali itabidi tena zifanyike jitihada nyengine kurudisha hali kama mwanzo jambo ambalo sidhani kama litatokea au litafanikiwa.

Hivyo njia hiyo sio nzuri bali madhara yake kwa jamii ni makubwa ukilinganisha na faida wanazopata Wanawake wachache wenye nafasi furani furani tena katika kipindi furani cha Maisha yao (sio umri wao wote).

Kwa sababu hata wale wanaume waelewa wenye mapenzi wanapata Wanawake tayari wameshamezeshwa fikra za kiharakati na ukombozi yaani haki ni sawa. So kuna ndoa nyengine ni very innocent katika hili ila nazo zinavunjika kwa sababu ya wimbi hili la harakati hizi.

Mwanaume hata kama ni mpole muelewa bado ana hulka ya uanaume ya kutaka kusikilizwa,, kutiiwa na kauli yake ndio iwe inaongoza familia. Lakini nowdays kupata wanawake wa kukubali hili from the scratch ni ngumu.

Tena kama ndio ana ki degree ni balaa zaidi. Kumbe maisha sio mashindano ni maelewano na masikilizano na kila mtu avae viatu vyake.
 
Oiyeyai! Sshyee (in Maasai voice) Dunia sasa imekuwa kweli ni uwanja wa fujo. Kwa hiyo kila mwenye ngoma yake na Apige.
 
Huna Mume wewe na kama unaye Sijui ni aina gani ya mwanaume huyo.View attachment 3080919
Mke wa mtu huyu. Tena Unatudanganya una miaka 25 now kwenye ndoa aisee Mbona bado unaonekana una akili za 20+
Aiseee kwahiyo kunywa pombe ndio indicator ya marital status ya mtu mbona mna arguments za kitoto namna hii, wewe unajua hapo nilikuwa na nani vipi kama nilikuwa na mume wangu na vipi kama naye ni mnywaji na haoni shida mimi kunywa we unajuaje au umekariri kila mtu anayekunywa hajielewi na ni mlevi mbwa, mbona mnahangaika sana kutaka kujua uhalisia wa maisha yangu vipi spana zimezidi nipunguze au
Kwenye hilo mmefeli tafuteni lingine nikikuuliza una uhakika wa asilimia ngapi katika hayo unayoyaongea unaweza kunijibu, watu kama ninyi ndio huwa mnashitakiwa na kufungwa au kulipishwa faini kwa character defamation kwa sababu ya kuropoka na kujifanya mnawajua sana watu kiundani, kujifanya mnafukua comments za nyuma na kubisha hakubadili ukweli kama mimi nimeolewa na nina miaka hiyo kwenye ndoa na wala siyo jukumu langu kuwaaminisha ninyi hilo
Wewe nichukulie mimi hivyo ila mimi sina
haja ya kukuchukulia kama feminist na hoe you are a real hoe
Usinifananishe mi na wewe kisa wewe ni malaya basi unadhani kila mtu ni malaya kama wewe, kwanza nawaonea huruma hao wanawake wanaokuvulia nguo mlawiti na mfiraji kama wewe, wewe ni malaya uliye kubuhu unanuka dhambi ya uzinzi na ulivyo huna aibu huwa unajisifia kabisa humu jukwaani
Mwanaume hawezi kuenda huko kwa sababu yeye ndiye anayeoa maamuzi ya kuoa yapo mikononi mwake, lakini pamoja na hayo maamuzi bado hawaoi wanawake wenye sifa wanazozitaka ndio ushangae maajabu hayo, pamoja na maamuzi hayo bado wanaoa masingle mother na makahaba wastaafu na huko kwenye ndoa wanaenda kulalamika na hatimaye kuachana
Wewe una ushahidi gani wa kuwa mimi nimeongopa ni kauli gani ambayo nimeitoa inayoashiria kwamba mimi kusema nina ndoa ya umri huo ni uongo unaweza kunionesha, mkishakosa hoja mnaanza kutafuta mlango wa kutokea kwa kujifanya eti hamtaki kubishana na mimi sijui naandika uongo kwani ninyi maisha yangu yanawahusu nini, na ninayoyaandika humu yanahusiana nini na maisha yangu kwani marital status yangu ndio kielelezo cha wanawake wote kwenye jamii au ni nini mbona mna arguments za kipumbavu namna hiyo
Unaongelea kuhusu maadili ya jamii kana kwamba wanaume wanayafuata hayo maadili yani hawa hawa wanaume wanaosema mwanaume hata akitembea na wanawake wengi kiasi gani hana hasara ndio unasema eti wanaoa kwa kufuata maadili ya jamii, na hata kama ingekuwa ni kufuata maadili ndio muoe wanawake ambao mnajua kabisa wataenda kuwasumbua kwenye ndoa kwamba ninyi mmeamua kujitoa kafara kuoa wanawake wenye tabia mbovu kwa faida ya hao hao wanawake, hebu nyoosheni maelezo ni kipi kinawafanya muoe pamoja na malalamiko yote haya dhidi ya wanawake acheni kurukaruka na kukwepa uhalisia msitufanye sisi watoto wadogo bado hujanipa jibu la kwanini wanaume wanaendelea kuoa
Umekazania kwamba napotosha jamii ila bado mpaka sasa hujaniambia faida anayopata mwanamke kwenye ndoa, zaidi sana umetoa sababu ile ile ya uchumi ambayo nimeshaeleza kwamba uchumi mwanamke anaweza kuupata nje ya ndoa, kwa kujitafutia pesa na mali zake mwenyewe bila kumtegemea mwanaume

Halafu kwanza nipotoshe jamii kwa wanaume gani hasa waliopo yani ninyi magalasa ndio mnifanye niwapotoshe wanawake wenzangu ili wakose ndoa, aiseee yani the best advice mtu yeyote anayoweza kuwapatia mabinti wa sasa hivi ni kwamba wafanye yale yanayowapa furaha wao wenyewe na siyo yanayowapa furaha wanaume, kwa sababu wanaume wengi hamstahili kupata hiyo furaha mnayotaka wanawake wawape yani somebody just needs to tell you this with a straight face

Halafu wanaume hawawezi kuenda kwa manabii na waganga kwa sababu wao ndio wanaoamua ndoa maamuzi ya kuoa yapo mikononi mwa wanaume, lakini cha ajabu pamoja na hayo maamuzi kuwa mikononi mwao bado hawaoi wanawake wenye sifa wanazozitaka, wengi bado wanaangukia kwa wanawake wenye tabia ambazo ndio mnazilalamikia kila siku

Sasa kama kweli suala la ndoa lingekuwa rahisi hivyo kwenu kwanini nanyi bado mnastruggle kupata wanawake wenye vigezo mnavyovitaka hatimaye mnaamua kusettle na wale mnaoona wana afadhali, ambao nao mwisho wa siku mnajikuta mmeangukia pua na kuanza kuona ndoa chungu matokeo yake ni malalamiko kila siku au talaka, na kuhusu mahitaji ya kihisia bado sijaona hoja ya maana uliyoandika narudia mahitaji ya kihisia kwa mwanamke ni rahisi kutatuliwa bila mwanaume ila mahitaji ya kihisia kwa mwanaume hayawezi kutatuliwa bila mwanamke

Wewe unachosemea ni ile uwezo wa kuweka vitu moyoni hilo kweli wanaume mnaliweza na ndilo linalowafanya muwe na depression na stress nyingi ambazo mnahitaji wanawake wawafariji na wawaliwaze bila kuwaelezea, ilihali hiyo tabia ya wanawake ya kushindwa kukaa na vitu moyoni ndio inawasaidia inawafanya wasikae na stress na depression kwa muda mrefu kama ninyi, na ndio maana wanaoongoza kupata matatizo ya kisaikolojia na kufa mapema kwa msongo wa mawazo ni wanaume na siyo wanawake
Aiseee wewe jamaa una uelewa mdogo sana mbona nimeshasema kwamba wanawake wenye hela walio desperate na ndoa ni kwa sababu ya msukumo wa jamii, sasa kwanini unapinga hilo bila hoja yoyote ile haya hebu niambie ukiacha hela mwanamke anapata nini cha maana kwenye ndoa toka kwa mwanaume, hebu kielezee hapa acha porojo na propaganda

Nani kakudanganya kwamba watoto ni lazima wapatikane kwenye ndoa tu kama ni hivyo basi kusingekuwa na single mothers, ni wanaume wangapi wanasema kabisa wao hawataki kuoa ila lengo lao ni kuzalisha tu wanawake kisha wanahudumia watoto wakiwa huko huko kwa mama zao, halafu kumbe unajua kwamba mwanaume anahitaji kupikiwa na kufuliwa na hawezi kuyapata hayo bila ndoa sasa unabisha nini ninapokuambia ndoa ni muhimu zaidi kwa mwanaume mbona ni kama unajicontradict na ndio unazidi kuithibitisha hoja yangu kwamba ndio uhalisia

Duuh kwahiyo wewe umekariri kwamba kusoma ni shule tu na mtu aliye chuo anakuwa anafanya nini au hujawahi kuona watu wako chuo na miaka 25, kuna jamii haziwanyooshei vidole wanawake ambao hawajaolewa regardless ya umri wao wewe ni wazi huna exposure hebu tembea huko duniani acha kunibishia kwa vitu ambavyo huna experience navyo, halafu bado hujajibu hoja yangu ya kwanini mwanamke aanze kuona umuhimu wa ndoa akifika miaka 35 tena hadi apewe pressure, kwanini asianze kuuona huo umuhimu tangu akiwa binti mbona ninyi wanaume mnauona umuhimu wa ndoa tangu mkiwa vijana tena bila pressure yoyote, sasa hapo nani mwenye uhitaji zaidi yani mtu awe na uhitaji na jambo halafu yeye mwenyewe alikatae hadi apewe pressure we ulisikia wapi
Hivi unajua we jamaa una matatizo ya akili wewe ni lini uliyajua maisha yangu hadi unasema kwamba mimi ni mtu ninayependa maisha ya anasa na starehe una uhakika na unachokiandika, halafu ulivyo hauna aibu unasisitiza kabisa kiasi kwamba mtu mwingine akisoma anaweza kudhani ni kweli unanifahamu kumbe hunijui hata jina sasa kwanini unaandika mambo usiyoyajua kunihusu, kwanini mkiishiwa hoja msikae tu kimya kwanini mnaanza kutumia defensive mechanism ya kuleta personal attacks ili muonekane mna hoja maisha yangu mimi hayahusiani na uhalisia uliopo kwenye jamii ukweli lazima usemwe na tutaendelea kuusema you will never stop me
 
Na kuonea huruma ila ndio maisha uliyo ya chagua. Haya endelea na ligi.
 
Huyo huenda ana matatizo ya kizazi huenda hisia zishajifia ashakuwa mwanamme kimtindo
 
Wewe unapinga kwamba wanaume si special creatures?
 
Unajua maana ya neno kumfahamu mtu, wewe nichukulie vyovyote ila hainipunguzii chochote hata mimi naweza kuamua tu kukuchukulia kama shoga na huwezi kunizuia, nigga get a life!!
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] jamaniiiiii
 
Ulosha
Ulishawahi kuona mwanaume anataka aombewe apate mume?,kinachofanya wanawake kuombewa kanisani wapate waume ni nini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…