Ikitokea wachezaji 20 wa Yanga wanavunja mikataba katikati ya ligi. Itakuwaje?

Ikitokea wachezaji 20 wa Yanga wanavunja mikataba katikati ya ligi. Itakuwaje?

Hiyo isome kwa faida yako mkuu.

Mimi hainisaidii.
Ndio hapo sasa unapojinyima uelewa kwa sababu ‘constructive dismissal’ ni kitu kingine kabisa; hakina uhusiano na mikataba ya wanamichezo. Hayo ni mambo ya ajira za makazini.

Ukisoma hiyo pdf na kama unaelewa contract law aspects of consideration ni kitu kile kile ila hiyo pdf inaelezea namna mishahara ya wachezaji inavyolipwa.

Kutokutokea mazoezini au kugoma kucheza ni sababu inayoweza pelekea usilipwe mshahara.

Anyway kwakua umeamua kubaki na mtazamo na mimi wacha nibaki na wangu, ila dogo achomoki hapo bila ya kukaa chini na management kwanza kuangalia wanaenda mbele vipi ata kama wamruhusu kutoka, lakini kutokwenda mazoezini hakumfanyi kutokuwa mali ya Yanga ata wakiamua kutomlipa.
 
Ndio any time.
Sasa swali ni je FIFA ni wajinga kiasi hicho? Vipi ikitokea wachezaji wengi wa timu moja wakiamua kuvunja mikataba wakati ligi inaendelea? Ligi itaendelea?
 
Taarifa ikitolewa na chombo cha habari tena ikaambatanishwa na picha na haijawahi kukanushwa inaashiria ni habari sahihi.

Yaani Rais wa timu anatoka jukwaani anaenda kuongea na mchezaji wa timu pinzani baada ya mechi na wanafanya mazungumzo binafsi, huku hizo timu mbili zikitegemea kurudiana baada ya wiki chache, wewe unaona sawa?
Try again alisimema kasha ongea na Adebayor kipindi kile Simba wanacheza na Asec mbona haukuona shida?
 
Tusimung'unye maneno ndugu yangu. Kuendelea kumlipa mchezaji ambaye waziwazi amesema hataki kuchezea hiyo timu, inaonyesha Yanga hawaamini wanachokifanya. Hizi habari za mitego sijui nini ni utoto tu wa wazungumzaji.

Hii club inaendeshwa kihuni sana. Rais wa club anatoka jukwaani anaenda kuongea na mchezaji wa timu pinzani baada ya mechi kwa mazungumzo ya faragha ni jambo la ajabu sana. Tena ukizingatia timu hizi zinategemea kurudiana wiki chache zijazo.

Jana msemaji wao alisema waziwazi amemtafuta Kipre Junior wa Azam na ameanza kumpanga jinsi atakavyoondoka Azam kwenda Yanga.
Huyu ni Jemedari mtupu
 
Kwa nini wachezaji 20 wa Yanga ni wachezaji 20 wa Simba au timu nyingine. Kwa nini 20 na si chini ya hapo au zaidi ya hapo? Ni ipi hasa ajenda yako?
Yanga hapo imewakilisha timu yoyote ya mpira. Idadi hiyo inawakilisha 'idadi kubwa ya wachezaji'
 
Sasa swali ni je FIFA ni wajinga kiasi hicho? Vipi ikitokea wachezaji wengi wa timu moja wakiamua kuvunja mikataba wakati ligi inaendelea? Ligi itaendelea?
Ili swali gumu sana mkuu sidhani kama hawa mbumbumbu wa msimbazi wanajibu kamili.
 
Kwahiyo inawezekana wachezaji wote wa kikosi cha YANGA wakavunja mkataba kipindi ligi inaendelea?
Unajua historia ya Yanga? Ni mara ngapi Yanga wamekuwa na migogoro na wachezaji wao hadi kufikia kufukuza wachezaji wote? Mara nyingine timu iligawanyika mara mbili, nusu ya wachezaji wako kambi hii, nusu wako kambi nyingine. Jifunze historia ya timu yako.
 
Kama wachezaji wana haki ya kuvunja mikataba wakati wowote, kuna uwezekano wa kutokea kitu cha ajabu sana. Swali ni je pale Yanga ikitokea wachezaji zaidi ya 20 wamepata deals nzuri na wameamua kuvunja mikataba yao (kama alivyojaribu Feisal), timu itaendelea na kushiriki mashinano?
Utopolo hamnaga akili
 
Try again alisimema kasha ongea na Adebayor kipindi kile Simba wanacheza na Asec mbona haukuona shida?
Sawa na Manzoki alikuja kwenye uchaguzi wa Simba wakati siyo hata mwanachama. Two wrongs don't make it right.
 
Unajua historia ya Yanga? Ni mara ngapi Yanga wamekuwa na migogoro na wachezaji wao hadi kufikia kufukuza wachezaji wote? Mara nyingine timu iligawanyika mara mbili, nusu ya wachezaji wako kambi hii, nusu wako kambi nyingine. Jifunze historia ya timu yako.
Walifukuza wachezaji wote wakati ligi inaendelea?
 
Unajua historia ya Yanga? Ni mara ngapi Yanga wamekuwa na migogoro na wachezaji wao hadi kufikia kufukuza wachezaji wote? Mara nyingine timu iligawanyika mara mbili, nusu ya wachezaji wako kambi hii, nusu wako kambi nyingine. Jifunze historia ya timu yako.
Simba hajawahi kuwa na migogoro au kuna timu duniani haijawahi kuwa na migogoro na wachezaji? Juzi tu babu alitaka achomoe betri huko msimbazi
 
Simba hajawahi kuwa na migogoro au kuna timu duniani haijawahi kuwa na migogoro na wachezaji? Juzi tu babu alitaka achomoe betri huko msimbazi
Tunaongelea wachezaji wote kufukuzwa au timu kugawanyika pande mbili, nusu ya wachezaji wako huku na kocha wao, nusu wako kule na kocha mwingine. Mtafute Minziro atakwambia.

Timu chache sana duniani kama si Yanga pekee ndiyo zimewahi kuwa na aina za migogoro na wachezaji ambayo Yanga imekuwa nazo.
 
Back
Top Bottom