Ikulu Dar: Rais Yoweri Museveni na Rais Samia Suluhu washuhudia utiaji saini wa mikataba ya utekelezaji wa mradi wa bomba la mafuta

Tunaomba hii mikataba iwe inafafanuliwa kwa wananchi ili tuwe tunaelewa.
Sio ifafanuliwe ili tuelewe.

Iwekwe wazi ili tuisome.

Period.

Watufafanulie kwani sisi hatukusoma shule ?
 
Hapa ndipo Nimeshangaa, Hata Mwendazake pia alishasaini na Huyu Pia akaenda Huko Sasa kusaini Kusaini kusaini Kila Wakati.
Watakuwa wanasaini page moja moja wameanza 2015 kwa hiyo tutarajie mpaka 2025 watakamilisha utiaji saini page zote za mkataba.
 
Mhe. Rais Museveni na Mhe. Rais Samia watashuhudia utiaji saini wa mikataba ya utekelezaji wa mradi wa bomba la mafuta la kutoka Hoima nchini Uganda hadi Bandari ya Tanga nchini Tanzania
Sasa kuna tatizo. Kutokana na tatizo la mabadiliko ya mazingira (climate change), mataifa makubwa duniani yameweka mkakati wa kuacha kutumia mafuta kwa ajili ya magari na mitambo. Norway kwa mfano, wanasema kufikia 2050 wataacha kabisa shughuli za kuchimba mafuta.

Uingereza wanasema watapiga marufuku magari ya kutumia diesel kufikia 2025 nadhani. Japan, Germany na hata China, wote wanasema ndani ya miaka 15 ijayo wanataka kutoka kwenye kutumia mafuta kwenye magari na kuingia kwenye magari ya umeme (from internal combustion engines to electric vehicles)

Sasa hii inamaanisha nini kwa nchi kama Tanzania ambazo hadi sasa zimekalia tu uchumi wa mafuta bila kuuendeleza? Ina maana ndani ya miaka 20 ijayo, mafuta yatakuwa si mali kitu. Hata ukigundua una mafuta mengi kama bahari ya Hindi, hayatakusaidia tena kwa kuwa dunia imeanza kuondoka toka tekinolojia ya mafuta kwenda teknolojia ya umeme!

Hivyo basi, kama kweli tunataka kufaidika na rasilimali ya mafuta tuliyonayo, ni lazima iendelezwe ndani ya kipindi cha miaka kumi ijayo. La sivyo haya mafuta yatakuwa na rasilimali isiyohitajika tena duniani, na ndani ya kipindi cha miaka kumi ijayo tutaanza kushuhudia kuporomoka kwa bei ya mafuta kadiri magari ya umeme yanavyoingia sokoni. Leo hii hata Lamborghini wamesema wataacha kutengeneza gari za mafuta!

 
Huyu waziri Liberata anawaza Rwanda tu inakuwaje anakosea kuwa huu mkataba ni wa Tz na Rwanda badala ya Ug

Halafu huwa kama hajiamini hivi
 
Mara Pap Mtawala kikongwe wa UG amekuwa 1st Gentlemen. Watoto wa kike sio wakuwaamini sana. Tunaweza jikuta Dodoma inahamia Kampala. Tunasema mikataba ya bomba kumbe hati za ndoa.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Uganda pia wanataka Gesi kutoka Tanzania, lkn speed ya kusambaza gesi hapa Tanzania bado ni ndogo sana,
bado watanzania walio wengi hawajafaidika na gesi yetu.

Kabla hatujaiuza Uganda na Kenya kwanza gesi hiyo itufaidishe kwanza ndipo tuiuze nje.
 
Hivi kwann mikataba ni siri ya serikali?
 
Mara Pap Mtawala kikongwe wa UG amekuwa 1st Gentlemen. Watoto wa kike sio wakuwaamini sana. Tunaweza jikuta Dodoma inahamia Kampala. Tunasema mikataba ya bomba kumbe hati za ndoa.
Rais Samia pengine anao umri wa mama yako mzazi. Jaribu uwe na adabu japo za kinafiki.

Watu wa aina yako ndio mnaoanzisha uzi wa kudharau serikali ya sasa kila siku, ujumbe wenu wa msingi kabisa ni akili za kipumbavu kama hizi.
 
Huo utakuwa ni utiaji saini wa ujenzi wa bomba la maziwa, la mafuta walishamaliza zamani.
 
Mara Pap Mtawala kikongwe wa UG amekuwa 1st Gentlemen. Watoto wa kike sio wakuwaamini sana. Tunaweza jikuta Dodoma inahamia Kampala. Tunasema mikataba ya bomba kumbe hati za ndoa.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] teh teh teh[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji2956][emoji2956][emoji2956][emoji2956][emoji2956][emoji2956][emoji2956]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…