Ikulu: Mkapa hawezi kupanda mahakamani; Hahusiki kesi ya Mahalu

Ikulu: Mkapa hawezi kupanda mahakamani; Hahusiki kesi ya Mahalu

Tehe tehe teheeee!
Kazi kwelikweli.
'Hawezi kutinga mahakamani' who is he!
samahan kama ntakukwaza,ila kama nimeelewa taarifa vizuri ni kwamba ikulu imesema hawez kutinga mahakaman coz hausiki nakesi ya msing iinayozungum,zwa
 
Kumbe Mwinyi ndie aliyeiuza Loliondo kwa waarabu? Duh!!!! Mwinyi alikuwa Fisadi lakini alikuwa mapema enzi hizo
 
ishu hapa ni hati inayo onyesha Mr clean kaapa na sio huyo Banyamlenge anavyo tetea Ikulu.
Kwanza ni mgeni na shughuli za Ikulu na mala nyingi amekuwa anajibu majibu mengi kwa ufahamu wake na si IKulu
kutokana na kuto jua maadili ya TIS na kazi zao.
Hana jipya zaidi ya kusoma magazeti na kukurupuka na majibu ya mizaha. Any way fadhila za uwana mtandao hizo.

Kikwete amezungukwa na maharamia ndio washauri wake;sasa kama Rostam akivuliwa gamba Salva atabaki Ikulu kwa mintaarafu gani? Salva alipelekwa Ikulu na Rostam ili kiwe kiungo chake kufanikisha mambo yake ya uharamia kwa nchi yetu sasa Jakaya kamstukia na kama ataendelea kumuacha Salva pale ajue ndio kitakuwa kisu mgogngoni pake !!
 
great thinkers mliocoment hii post mmepotoshwa.mwanahalisi hawakuzungumzia ikulu kumlinda mkapa bali kikwete.rweyemamu amechomeka kusudi jambo hilo la mkapa,akithibitisha kile gazeti limesema.anahaha kumlinda kikwete.ni hivi mahalu alifanya malipo halali kadiri ya gharama zilizokubaliwa.rais mkapa kathibitisha hivyo.so mkapa anamtetea mahalu.angalizo. Kikwete alikuwa waziri w mambo ya nje na alitoa tamko bungeni kutetea malipo aliyofanya mahalu. Sasa hoja haipo kwa mkapa bali kikwete ambaye anamshitaki mahalu kwa visasi wakati yeye mwenyewe ni muhusika.so ni kweli ikulu inahaha kumsafisha kikwete na siyo mkapa.someni tena habari ile siyo mpotoshwe na huyu mhaya wa kwanza kujipendekeza na kuathiri hadi utu wake
 
wana JF tusijadili sana suala la uraia wa reyemamu, hebu tulitazame kwa marefu na mapana suala la mstaafu Chinga kama nihaki afikishwe kizimbani au la; bado haijajulikana mbele ya sheria nani katoa melezo sahihi kati ya gazeti na Reyemam, naomba wanasheria mtufafanulie vizuri juu ya hili.:A S 39:

Ni muhimu pia kujadili uraia wake. Maake watu kama hawa ndio wanaonufaika na mfumo wa kifisadi na kui-yumbisha nchi yetu kwa vile hawana uchungu nayo
 
Nadhani Rwehemamu anafanya kazi Ikulu kama Expert kutoka nje ya nchni siyo kama Mtanzania.
 
Kwa kweli kama Salva kasema hivyo basi ameingilia uhuru wa mahakama na hakuna haki yeyote itakayotendeka hapo... Ni bora angesema kuwa hakuna summons yeyote iliyomuita Mhe. Mkapa mahakamani, lakini kusema kuwa Mkapa hahusika how did he know? Ina maana Ikulu ndio ofisi ya Presecutor? au ndio defensive counsel? INAMAANISHA IKULU INAJUA MWENENDO WOTE WA KESI HII...
 
"Ikulu inakanusha taarifa zilizochapishwa na gazeti moja linalotoka mara moja kwa wiki kuwa imekuwa ikihaha kumsafisha Rais Mstaafu wa awamu ya Tatu Mheshimiwa Benjamin Mkapa. "Na inasisitiza kamwe haiwezi kufanya hivyo, kwani yeye si mhusika katika kesi hiyo," alisema Rweyemamu na kuongeza kuwa kuandika habari hiyo huku kesi ikiendelea ni kuingilia uhuru wa mahakama.

Imbecile,

Gazeti haliwezi kuingilia uhuru wa mahakama. Gazeti ni subject kwa mahakama.

Rais Mkapa alipotoa tamko kuhusu kesi ya Kiwanda cha Sukari Morogoro ambayo bado ilikuwa Mahakamani, pale aliingilia uhuru wa mahakama kwa sababu yeye hakuwa subject wa mahakama na zaidi ya hapo alikuwa mteuzi wa majaji, mtu mwenye influence juu ya mahakama.

Huyu Salva Rweyemamu haelewi kuingilia uhuru wa mahakama maana yake ni nini. Mahakama haijatoa gag order kwa magazeti, magazeti yana uhuru wa kuelezea habari kama yanavyoona, ingawa hayana haki ya kuvunja sheria.

Kama gazeti limevunja sheria Ikulu ina haki ya kulipeleka mahakamani. Haya mambo ya kusemana rejareja, bila hata kutaja jina la gazeti, yanaonyesha Ikulu kuendeleza itikadi yake ya kutawala kwa vitisho na kuminya uhuru wa vyombo vya habari.

Zaidi ya hapo, kwa nini Ikulu imsemee Mkapa? Mkapa mwenyewe yuko wapi? Swala zima la kumuita Mkapa mahakamani kama kweli Mkapa ni msafi na hahusiki na kesi hii kabisa si linaweza kumpa Mkapa nafasi ya kusema upande wake na kujisafisha?

Kwa nini Ikulu inakuwa na kimbelembele kusema Mkapa msafi wakati swala bado liko mahakamani? Ikulu ambayo mkuu wake ana influence kubwa mahakamani haioni kwa kusema Mkapa msafi wakati swala bado liko mahakamani imeingilia uhuru wa mahakama zaidi ya gazeti ambalo halina influence kubwa mahakamani ?
 
Kwa kweli kama Salva kasema hivyo basi ameingilia uhuru wa mahakama na hakuna haki yeyote itakayotendeka hapo... Ni bora angesema kuwa hakuna summons yeyote iliyomuita Mhe. Mkapa mahakamani, lakini kusema kuwa Mkapa hahusika how did he know? Ina maana Ikulu ndio ofisi ya Presecutor? au ndio defensive counsel? INAMAANISHA IKULU INAJUA MWENENDO WOTE WA KESI HII...

Mkuu Limbani nimeandika bandiko hilo hapo juu kabla ya kusoma lako, lakini naona tunafikiri kitu kimoja.

Huyu Salva Rweyemamu mtupu kabisa. Anasema kigazeti kisicho na nguvu ya dola kinaingilia uhuru wa mahakama kwa kusema Mkapa atatinga mahakamani.

Wakati huo huo haoni kwamba yeye mwenye sauti ya juu kabisa katika dola letu, msemaji wa rais aliye juu ya sheria, rais anayeteua majaji wa mahakama, kwa kusema Mkapa ni safi na hana hatia katika swala ambalo bado liko mahakamani, haoni kwamba yeye ndiye anayeingilia uhuru wa mahakama.

Kama kuna jaji aliyepewa kesi hii, na jaji anaogopa ogopa watawala wa nchi, halafu anamsikia msemaji wa Ikulu anasema Mkapa hana hatia, halafu jaji akatazama kesi akaona Mkapa ana hatia, unafikiri hii kauli ya Rweyemamu haiwezi kupindisha haki katika hukumu ya huyu jaji kama jaji hana moyo wa ujasiri ?

Tayari kashajua Ikulu inataka Mkapa asipatikane na hatia kabla mahakama haijatoa hukumu.

Anayeingilia uhuru wa mahakama hapa ni nani? Gazeti au Rweyemamu na Ikulu yake ?
 
Mkuu Limbani nimeandika bandiko hilo hapo juu kabla ya kusoma lako, lakini naona tunafikiri kitu kimoja.

Huyu Salva Rweyemamu mtupu kabisa. Anasema kigazeti kisicho na nguvu ya dola kinaingilia uhuru wa mahakama kwa kusema Mkapa atatinga mahakamani.

Wakati huo huo haoni kwamba yeye mwenye sauti ya juu kabisa katika dola letu, msemaji wa rais aliye juu ya sheria, rais anayeteua majaji wa mahakama, kwa kusema Mkapa ni safi na hana hatia katika swala ambalo bado liko mahakamani, haoni kwamba yeye ndiye anayeingilia uhuru wa mahakama.

Kama kuna jaji aliyepewa kesi hii, na jaji anaogopa ogopa watawala wa nchi, halafu anamsikia msemaji wa Ikulu anasema Mkapa hana hatia, halafu jaji akatazama kesi akaona Mkapa ana hatia, unafikiri hii kauli ya Rweyemamu haiwezi kupindisha haki katika hukumu ya huyu jaji kama jaji hana moyo wa ujasiri ?

Tayari kashajua Ikulu inataka Mkapa asipatikane na hatia kabla mahakama haijatoa hukumu.

Anayeingilia uhuru wa mahakama hapa ni nani? Gazeti au Rweyemamu na Ikulu yake ?

Scratch mine back I will do to yours! Mmh nadhani vimechacha somewhere inabidi kila mtu amsaidie mwenzake, poleni vipofu wawili soon you will find yourselves falling in the den of hungry lions...
 
Back
Top Bottom