Ikulu Yamwangukia Mkurugenzi aliyetimuliwa na Rais Kikwete

Ikulu Yamwangukia Mkurugenzi aliyetimuliwa na Rais Kikwete

Kiranga - a child molester, nani hapo mtoto?

Punguza chumvi kijana!

Nakuonyesha kwamba Kikwete anavyomfokea huyu mtu wa wilaya kuna forces ziko so disproportionate ni sawa na mtu mzima kum molest mtoto mdogo asiye na defence.

Kama Kikwete kweli anakerwa na maovu mbona kuna makubwa ya size yake kibao ma EPA na Meremeta huko? Haya si angewaachia watu wa level zinazohusika wa deal nayo tu?

Hapa anaua nzi kwa kutumia missile, this is so disproportionate, ndiyo maana nikasema Kikwete hapo anakuwa kama child molester.

Sasa wewe hapo hapo unauliza swali kama hujui halafu hapo hapo ushapass judgement.

Kikwete ni a highhanded usurping Draconian mangimeza, na hajaanza leo, ndio maana wakulima walimpiga mawe Mbeya huko na yule mchizi wa Mwanza alimpiga mtama.

Bisha!
 
Ni mambo yaleyale ya kila siku yanayotendeka kwenye wizara mbalimbali hadi sasa. Utendaji kazi umekuwa ni wamazoea. Mfano halisi ndo kama huo kuchanganya mambo,mtu anaetakiwa kufanyiwa upasuaji wa kichwa anapasuliwa mguu n.k. Bora uchaguzi ufike mapema tuanze upya, Mungu atujalie tufike salama. Tutakao kumbwa na hayo masahibu tujipe pole mapema,Mungu atunusuru.
 
Twende kazi tutafika tu na hii si ndo 2010? Utasikia ushindi wa kishindo sijui tsunami jamaa karudi tena kufanya vituko hivi ikulu.
 
PRESIDENT SPEAKING:.........."Nakumbuka nilipofanya ziara wananchi wale waliniambia wanayo dispensary (Zahanati ) lakini, hawana gari la wagonjwa na sio nyinyi!. Hatukupi bwana, sio lako hatukupi." "Hatuwezi kukupa gari; watafuteni wanaopaswa kupewa gari hii; hii ni kashfa kubwa; document zote zimeandikwa kwa Kijiji cha Engalinaibo, iweje tuwape watu wa Ngorongoro."

Duh! kaaaaaaaaaaaaazi kweli kweli!

Huyu jamaa amezidi uswahili mnoooo. Safari zooooooooote zile ng'ambo bado ujanja wa kucompose kama president hakuna!
 
Nadhani Ikulu kuna tatizo kubwa la uwajibikaji na mpangilio wa kazi.
Nadhani rais anahitaji watu wengine ambao wanajua kupanga na kuratibu mambo vizuri. Anahitaji kufanya hili sasa na siyo baadaye, otherwise atakuwa amechelewa sana na kitu kibaya zaidi kinaweza kutokea.
Hao watu unaosema wanatakiwa kutolewa ikulu,nadhani si sahihi,hapa dawa ni wao kupatiwa Rais mwingine maana huyu amewashinda,hashauriki na ni mkurupukaj sana
 
Ni mambo yaleyale ya kila siku yanayotendeka kwenye wizara mbalimbali hadi sasa. Utendaji kazi umekuwa ni wamazoea. Mfano halisi ndo kama huo kuchanganya mambo,mtu anaetakiwa kufanyiwa upasuaji wa kichwa anapasuliwa mguu n.k. Bora uchaguzi ufike mapema tuanze upya, Mungu atujalie tufike salama. Tutakao kumbwa na hayo masahibu tujipe pole mapema,Mungu atunusuru.

Si wizarani tu,hata mitaani,utaona oktoba,watu badala ya kumchagua .......,watamchagua Muungwana.
Kaaaaaaaaaaaaazz kwei kwei
 
yani kumwomba msamaha aitoshi ata kidogo kwa fedhea walomtwisha ivi mpaka inatokea hivi ikulu kuna tatizo gani yani lazima kuna usanii ulotaka kufanyika akuna makosa yoyote yale usanii tuu hapo

Hawa jamaa wa IKULU ni tiamajitiamaji mkulu asiogundue. Sasa jamaa kisha washitukia kuwa wanamdanganya mambo mengi ndiyo maana hata katika kuuliza maswali akawa ni skeptikal akijua mchezo uleule unaendelea.

JK kama huwaamini wanyikulu wako Fumua IKULU hiyo tafuta wapya uanze nao, vinginevyo "the buck stops with you"
 
Hii ndio nchi yetu ilivyo wasio na makosa wanafokewa na wenye makosa wanachekewa. Hivi ni kazi yake rais kuzungumza na hawa individuals? Kwanini asingesubiri aone mwisho kutatokea nini na hao wasaidizi wake (baada ya tatizo kutokea) watamwambia nini.

Kwa watu wenye akili za kawaida kabisa watamuona mheshimiwa kama mtu mwenye papara, japo katika hali ya kawaida inaonekana kama kuna kitu kimejificha katika hili. Haiingii akilini kosa kama hili kutokea!! halafu rais aka act kabla ya walio chini yake kutoa maelezo na yeye kukimbilia kumshambulia mtu asiye na makosa.

Hapa hata angekaa kimya na yaliyopangwa kwa makosa yakatokea, kwani gharama ya hilo gari ni shilingi ngapi kiasi kwamba mpaka anatamka kwamba ni kashfa kubwa, nchi hii imeshuhudia kashfa ngapi na za gharama kiasi gani itakuwa hii ya gari,afteral gari lingekwenda kuwatumikia wananchi bado ingawa kwa makosa sio wale walioahidiwa lingekuwa kosa dogo na linarekebishika kuliko hili doa alilojitia yeye mwenyewe na ikulu kwa ujumla.

Ina maana Ikulu mtu yoyote akiamua kwenda kucheza bao ataruhusiwa? Documents zilizo mruhusu kuingia ikulu zilikuwa zinaeleza nini? Aahh tuyaache yatatupotezea muda bure, wenyewe watakapo maliza mchezo wao wa kuigiza watatuambia mchezo ulikusudiwa kuwa na mafunzo gani.

NIKIPATA NAULI NITAENDA KUTEMBEA IKULU.

SIJAWAHI KUSIKIA IKULU YA HIVYO, HATA WAKATI WATU WALIKUWA WAKIMUITA FIRST LADY SHEMEJI, LAKINI TARATIBU ZA MIALIKO ZILIZINGATIWA. (Tuimbe wimbo wa taifa labda yaweza kuwa sala salama ya kuinusuru hii nchi).

Nakumbuka tulikotoka, lakini tuendako mmmmhhhhh!!!!!
 
mi nadhani rais tunamuonea,kabla hatujamlaumu kiasi hicho huyo mkurugenzi ndo atueleze kaitwa na nani?hao ndo wakurugenzi wanaogawa rushwa na zawadi huko wilayani kiasi cha maofisa wa serikali kuu kubabaika inapokuja suala la utawala bora. ukichunguza sana waweza kukuta mambo mengine. Hata ningekuwa mimi ndo Jk huyo mkurugenzi asingerudi ngorongoro mpaka nijue kiini cha kupachikwa yeye kuja kupokea gari badala ya Longido!!! maana hapo ni suala la to put things right. Hapo tushukuru rais amekuwa na kumbukumbu nzuri kwa hiyo wakati mwingine sisi tunaopaswa kutimiza majukumu yetu ndo wenye matatizo kwani hao watu wa ikulu hawalipwi mishahara? Hapo hata akija rais gani kama watanzania hatutaki kuwa responsible i'm afraid tutawalaumu hadi majirani zetu!!!
 
Mkuu IDIMI,

Happy new year to you

Nipo naangalia jamvi kila mara sema natumia muda mwingi kuwasiliana na watu kwa PM,nchi inakwenda kubaya sana kwa sasa mpaka naogopa.

watu wamekata tamaa..Hivi leo nikukuuliza ni nani unaona anafaaa kama Jk asipogombea?fikiria majedwali yale ya Mzee Wangu Mwanakijiji..lile jedwali lile..

Wananchi wanalia,watawala hawajui wafanyaje,Zanzibar moto mkubwa umeanza kuchochowa..

tatizo Mkulu hakutusikiliza toka mwanzoni..walitudharau sana na kujidai uswahili na usaniii utasaidia.Makamba hakuna kitu na sijui kwanini Muungwana alimpa kazi ambazo inamzidi uwezo!

tutafika na mwaka 2010 ni mwaka wa mabadiliko!

Umesomeka mkubwa.
Tuendelee kukamua issues!
 
Tatizo la Jakaya ni kutokujiamini as a result anadhani kuwadhalilisha watendaji in public kutamfanya watu wasahau mapungufu yake katika kutekeleza kazi tuliyomkabidhi!!
 
Back
Top Bottom