Ilani ya CHADEMA Hii Hapa

Ilani ya CHADEMA Hii Hapa

Tumaini,
Ni dhahiri Ilani huelewi mchakato wa Ilani. Ilani yeyote (Manifesto, Platform) jina lolote linavyoitwa huandaliwa na Wataalam, na kuridhiwa na vikao vya maamuzi ya Chama. Tuambie hata kama Wewe ni ccm damu damu au chama chochote kile, ya ILANI ya ccm inaanzia wapi? Si ndiyo ile ile ambayo JK alikiri alikuta imekwisha kuandaliwa na hakuwa na lakufanya japo alikuwa hakubaliani na baadhi ya maeneo? Si ndiyo hiyo hiyo ambayo kwa wakati Mkapa aliwahi kutangaza kuwa haitekelezeki? Nadhani, hakuna madhara ilani katika mchakato wake kuandaliwa na wataalam na kuridhiwa( kwa kupitia mchakato wa vikao vya maamuzi- unless utuhakikishie kuwa Ilani ya Chadema haikupitia mchakato wa vikao vya maamuzi, vinginevyo una lako jambo tu na Chadema!

Ubovu wa viongozi unapimwa na Wanachama na vyombo vya Chama siyo na individual. Ningelitamani kuona unashusha kwenye jamvi opinion polls au takwimu kuhusu ubovu wa uliowataja? Hisia zinaweza kutawala, lakini kumbuka zitabaki kuwa hisia za individual, na hakuna hata siku mmoja utapendezesha watu wote asilimia mia moja.

Sisi wengine tumeumbwa kupokea criticism, both constructive and non constructive, positive and negative, kwa sababu ndiyo kigezo cha kujipima. Hivyo ninakushukuru kwa mawazo yako mazuri either way.
Tunashukuru sana kwa michango yote uliyoitoa hapa na kuona jinsi gani CHADEMA walivyofanya vizuri. Ni kweli kabisa CHADEMA wanaweza kufanya vizuri sana katika maeneo mengi sana waliyopewa na kuona hata CCM wanaiga mambo mengi sana
 
MMJ,
Aksante sana kwa maelezo yako. Ni kweli Ilani ya Chadema haikutekelezwa kitaifa kwa vile hatukushika dola, na Ilani hutekelezwa kwa kodi ya Mwananchi na anayekusanya kodi na kupewa mandate ya kukusanya ni chama kilichoshinda ndiyo maana sifa au lawama zote huenda kwa chama Tawala at any given time. Hata hivyo, Ilani ya Chadema imekuwa Tested katika maeneo ambako Chadema ni "chama Tawala", kwa yale mambo ambayo ni local, na mengi ya hayo mambo yamekwisha kuchukuliwa na Taifa. Ukitaka kupima nenda Halmashauri ya Wilaya ya Tarime ambayo iko chini ya Chadema, Kwa sehemu, Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma, ambaye inaongozwa kwa ushirikiano baina ya Chadema na CCM. Mathalan, Wilaya ya Karatu ndiyo iliyoanzisha ujenzi wa Sekondari katika kila kijiji na imeisha kukamilisha jambo hilo wakati Taifa liko bado ngazi ya Kata, ujenzi wa Zahanati katika ngazi ya Kijiji, na kutokea mwaka 2004 Halmashauri ya Karatu iliisha kukamilisha kazi hiyo na sasa tumevuka hata lengo kwani tuna zahanati hata kwenye ngazi ya vitongoji katika baadhi ya vijiji kutokana na jiografia ya eneo. Karatu ni mwalimu kwa Serikali ya CCM katika mengi, na mengi hayo bado hayafanyiki kitaifa, licha ya kuwa JK aliisha kuiga na kutangaza baadhi ya mambo hayo kuwa Sera yakitaifa. Hivyo, Chadema imekuwa Tested tayari kuliko chama kingine chochote cha upinzani na imefanya delivery ya tangible products ambazo zinaweza kuwa verified iwapo mtu ana nia njema.

Dr Slaa,

Hongereni sana kwa hatua ya maendeleo mliyofikia hasa kwa wilaya ya karatu.


Pamoja na hayo mafanikio naamini wengi wetu tutapenda kujua iwapo mna walimu wa kutosha katika kila shule na iwapo pia wafanyakazi wa afya nao wanatosheleza.


Kwa upande mwingine je mna mpango wowote wa kuanzisha shule za kidato cha tano na sita hasa kwa combinations za PCB na PCM?.


Vipi kuhusu Vyuo vya Ufundi hapo Karatu vipo?

Jaribuni pia kuangalia uwezekano wa kuwa na kipindi cha Redio na Televisheni kila wiki, mkielezea kwa undani nini ambacho Chadema inafanya katika maeneo na sekta mbalimbali hapa nchini na kitawafanyia nini Watanzania pindi kikiingia madarakani.
 
reason no.1 and 3 naweza kusema kuna mantiki pale to be debated kuongeza vat au kupunguza vat hakufanyi serikali kuwa na mapato mengi unaweza ukaongeza vat ukawafanya walipa vat aidha washindwe kufanyabiashara na kukimbiza wawekezaji au ukawafanya wakwepe ulipaji wake na ku create tatizo lingine la rushwa

kuhusu bajeti ya elimu kutoka 18% hadi 33% si kwamba ongezeko la bajeti litatoka wapi pesa ya bajeti inaweza kuwa ni ile ile ila elimu kupewa kipaumbele zaidi first priority mfano rahisi wa hesabu kama una bajeti ya sh.100 (15+40+45=100) na(10+30+60=100) hapa bajeti ni ileile ya sh 100 lakini umebadili tu mgawanyo
Bull,
Nashukuru kwa hoja zako. Tanzania inafanya biashara na nchi zilizotuzunguka. Hoja ya kushasha VAT ni ya siku nyingi, na wale wanaofuatilia wanaelewa madhara ya kuwa na VAT ya juu jambo ambalo linaweza kuathiri uchumi wa nchi. Hivyo, ni kuangalia principles za uchumi zinasema nini. Hoja zingine zimekwisha kuwa commented on, nadhani hazihitaji kujibiwa. Ila nataka kusema Ilani siyo Project write up, ambapo unaweka na Bajet na breakdown ya fedha. Ilani ni dira ya mambo ambayo chama inataka kufanya iwapo itapewa ridhaa na wananchi. Wala ilani nayo siyo mwisho baada ya kupata ridhaa ni lazima kupitia bajet ya kila mwaka Serikali inaanza kutekeleza ilani yake kwa kuomba kila mwaka kibali cha kukusanya fedha ili iweze kutekeleza miradi hiyo. Naona tatizo ni la ufahamu wa nini ni Ilani na inafanya kazi namna gani. Ukitaka kuona bajet ndani ya ilani, haitapatikana kwa chama chochote kile. Ilani inaweza kuwa na some figures na zenyewe ni malengo tu. Swala kubwa ni je Chama kiko serious kiasi gani katika kuweka programs zake baada ya ushindi kufuatana na Ilani yake, na inazisimimamia vipi ahadi zake zilizotolewa kupitia ilani yake.
 
VAT si ulishushwa na Bunge kwenye bajeti ya mwaka 2009/2010 kutoka 20% na kuwa 18%?

Kwa hiyo CCM wametekeleza ilani ya CHADEMA?

Wanaosema haiwezekani wajiulize mbona imefikia 18 na CHADEMA walisema 16? so huenda inawezekana.
 
Ala! kumbe wanachama wakiwakubali wanakuwa bora? basi JK ni bora kwasababu wamemkubali wananchi wa Tanzania..ndio line of thinking!

Nathibitisha ni wabovu kwasababu zifuatazo

a) Mbowe amekuwa mwenyekiti bila kufuata demokrasi (undugunization na club of business people) sitegemee chochote kwa watanzania zaidi ya loyality kwa elites wa chadema ambao bahati mbay ni wachaga na wafanyabiashara wanaotengeneza business network. Pili elimu yake inatia mashaka hajasoma (kihiyo), tatu hana mkakati wowote zaidi ya kuongelea ufisadi huo ndi wimbo anaoufahamu period! chama ni zaidi ya wimbo huo

b) Slaa ni sawa na sumaye kiburi na dharau, above all elimu ya kuendesha kanisa (church management) ameipeleka kwenye chama anashirikiana na mbowe kuendeleza ukatoliki wao...Slaa ni mlalamisha anafaa huko huko karatu aendelee kulalama kitaifa ana hoja yoyote.
Tumaini,
Thanks. I have no comment kwa kuwa ni mtuhumiwa I should not be the right person to make any comment on your postings. Nilikuwa nafanya kwa manufaa ya wana JF, na nitaendelea kutoa ufafanuzi kwa wale wenye nia njema ya kutaka kujua Ilani ya Chadema.
 
Bull,
Nashukuru kwa hoja zako. Tanzania inafanya biashara na nchi zilizotuzunguka. Hoja ya kushasha VAT ni ya siku nyingi, na wale wanaofuatilia wanaelewa madhara ya kuwa na VAT ya juu jambo ambalo linaweza kuathiri uchumi wa nchi. Hivyo, ni kuangalia principles za uchumi zinasema nini. Hoja zingine zimekwisha kuwa commented on, nadhani hazihitaji kujibiwa. Ila nataka kusema Ilani siyo Project write up, ambapo unaweka na Bajet na breakdown ya fedha. Ilani ni dira ya mambo ambayo chama inataka kufanya iwapo itapewa ridhaa na wananchi. Wala ilani nayo siyo mwisho baada ya kupata ridhaa ni lazima kupitia bajet ya kila mwaka Serikali inaanza kutekeleza ilani yake kwa kuomba kila mwaka kibali cha kukusanya fedha ili iweze kutekeleza miradi hiyo. Naona tatizo ni la ufahamu wa nini ni Ilani na inafanya kazi namna gani. Ukitaka kuona bajet ndani ya ilani, haitapatikana kwa chama chochote kile. Ilani inaweza kuwa na some figures na zenyewe ni malengo tu. Swala kubwa ni je Chama kiko serious kiasi gani katika kuweka programs zake baada ya ushindi kufuatana na Ilani yake, na inazisimimamia vipi ahadi zake zilizotolewa kupitia ilani yake.

Nashukuru Dr Slaa kwa majibu yako ingawa ume quote post yangu niliyomjibu Bull lakini all in all ujumbe uliokusudiwa umefika asante
 
Ulitaka kujibu swali 1 na 2 lakini bado unanipa wasiwasi pia kuhuisu wafuasi wa chadema wasivyo kua makini nadhani wengi bado ni wafuata upepo, kabila au dini unao ongozwa na chadema.

Mmeshindwa kabisa kujaribu kujibu (3 and 4) inanithibitishia chadema wanakimbia na hawaelewi kero ya jamii, pamoja kua Slaa aliahidi hapa jf kuwa swala la OIC na kadhi court atalitolea ufumbuzi kwenye ilani ya 2010 lakini swala hilo kaliepa, SHAME!!!!

Chadema watfuatilia mikataba, wakati ZITTO alikua mjumbe kwenye ufuatiliaji wa kwanza, lakini wenye kampuni ya chadema hawakumuamini kwa hiyo wataunda tume ingine, SHAME!!!!

Wataongeza bajeti ya elimu, wewe unatetea unasema (bajeti ya sh.100 (15+40+45=100) na(10+30+60=100) hivi uelewi maana ya kuengeza bajeti ninini? hiyo unayosema wewe ni piriotised bajeti, sasa ni sehemu zipi kwenye elimu chadema watapunguza? SHAME !!!

Watapunguza VAT,(hakuna figa za kitaalam kiasi gani kitaathiri pato) wata ongeza pato la serikali kwa njia gani ili kuongeza bajeti ya elimu?

Mi sio member wa Chama chochote nataka ku vote, you have the last chance to convince me, kwanini ni vote chadema? kuna ilani ingine au ni huu usaniii ?
Bull,
Kama unasoma vizuri threads, nadhani utaelewa Slaa alisema nini kuhusu OIC. It is not the same thing as what you are saying. Do justice to statements zilizowekwa, hata kama hutaki kumfanyia justice mtu. Nilisema na ninarudia, Ilani ya Chama haiwekwi na mtu, bali na vyombo vya maamuzi ya chama. Chadema ndio inafanya review ya Ilani yake kama vinavyofanya vyama vyote sasa. Hivyo ni unfair ku fanya judgment kabla hujauliza kama vikao husika vimekaa au la, na kama ni wakati mwafaka kutoa ilani sasa au la. Nadhani tutaendelea kuelimishana ili kujua proper procedures na ninajua kuwa ... kwa wakati mwafaka "kitaeleweka" kama si kwa mtu mmoja mmoja basi kwa sehemu kubwa ya jamii.
 
Tumaini,
Thanks. I have no comment kwa kuwa ni mtuhumiwa I should not be the right person to make any comment on your postings. Nilikuwa nafanya kwa manufaa ya wana JF, na nitaendelea kutoa ufafanuzi kwa wale wenye nia njema ya kutaka kujua Ilani ya Chadema.

Tunaomba msikatishwe tamaa na watu kama hawa wewe uendelee kutuletea ufafanuzi hawa huwa hawakosekani sehemu yoyote hata makazini wapo ni kuwavumilia maana ni sehemu ya jamii nina swali Dr kama bado upo hewani mpango wa Redio ya Chadema umefikia wapi maana hiyo inaweza kusaidia kuwafikia wananchi wengi kwa muda mfupi.
 
Nakushukuru sana Dr Slaa kwa kujitokeza na kujibu hoja za hii thread,asante sana..Bull,Waberoya ,na Tumain wako kazini kwaajili ya kuiponda vibaya CHADEMA.,sio watu wazuri kabisa kwani wanataka kupoteza kabisa mwelekeo wa mjadala.Hawana hoja bali wanalalamika bila facts zozote.
 
Tumaini,
Thanks. I have no comment kwa kuwa ni mtuhumiwa I should not be the right person to make any comment on your postings. Nilikuwa nafanya kwa manufaa ya wana JF, na nitaendelea kutoa ufafanuzi kwa wale wenye nia njema ya kutaka kujua Ilani ya Chadema.

Asante mkuu kwakuwa na guts za kujibu comment zangu!

Nilitegemea ungesema "Kweli au Si kweli" nakutoa ufafanuzi lakini naona umekimbia maswali ya msingi na concern yangu ya msingi kama mwananchi

Anyway ndio aina ya wanasiasa wetu unaendelea kunifanya niamini usemi maarufu kwamba ni vigumu kuamini wanasiasa kwa kuwa hawako specific...

Naona umeanza kulalamika upate huruma ya wana JF kwamba maswali yangu hayana nia njema isipokuwa wewe ndio una nia njema ...mimi nakuuliza pia kwa nia njema isije chama chenu kikachukua madaraka tukajikuta tunaongozwa na viongozi wanaoegemea kwa jamii fulani...

Nimategemeo yangu utanipa ufafanuzi badala ya kuondelea kujificha kwenye nyasi fupi huku ukijua hii ni concern ya watanzania wengi.
 
Nakushukuru sana Dr Slaa kwa kujitokeza na kujibu hoja za hii thread,asante sana..Bull,Waberoya ,na Tumain wako kazini kwaajili ya kuiponda vibaya CHADEMA.,sio watu wazuri kabisa kwani wanataka kupoteza kabisa mwelekeo wa mjadala.Hawana hoja bali wanalalamika bila facts zozote.

Gender S. pole sana kwakukerwa na michango yetu kama ulivyo wewe kazini na sisi wengine tuko kazini. ndio line yako ya thinking very low for you
 
Asante mkuu kwakuwa na guts za kujibu comment zangu!

Nilitegemea ungesema "Kweli au Si kweli" nakutoa ufafanuzi lakini naona umekimbia maswali ya msingi na concern yangu ya msingi kama mwananchi

Anyway ndio aina ya wanasiasa wetu unaendelea kunifanya niamini usemi maarufu kwamba ni vigumu kuamini wanasiasa kwa kuwa hawako specific...

Naona umeanza kulalamika upate huruma ya wana JF kwamba maswali yangu hayana nia njema isipokuwa wewe ndio una nia njema ...mimi nakuuliza pia kwa nia njema isije chama chenu kikachukua madaraka tukajikuta tunaongozwa na viongozi wanaoegemea kwa jamii fulani...

Nimategemeo yangu utanipa ufafanuzi badala ya kuondelea kujificha kwenye nyasi fupi huku ukijua hii ni concern ya watanzania wengi.

Tumain hebu kuwas na heshima hata kidogo..Dr Slaa hawezi kujisema mwenyewe hata siku moja.Wala hukuwa na Consern ya msingi ambayo ingetakiwa kujibiwa na Dr Slaa.Dr Slaa wala hahitaji huruma ya wanaJF kwani haimsaidii kitu.
Ni kweli kabisa wewe huna nia njema kwani uko kazini kwaajili ya kuishambulia CHADEMA na nido maana kila thresd ya CHADEMA lazima uchangie tena negatively.Majibu ya Dr Slaa ni mepesi tu lakini jamaa umahamaki ile mbaya,kama sio uko kazini ni nini?Hulali kazi kuisema vibaya..Hebu kuwa na soni hata kidogo.Lol
 
Gender S. pole sana kwakukerwa na michango yetu kama ulivyo wewe kazini na sisi wengine tuko kazini. ndio line yako ya thinking very low for you

Kumbe kuna watu mko kazini basi ni vizuri mmeweka wazi tumewajua lakini tunashukuru ukiona hivyo ujue JF imeanza kupiga ngumi za uso hadi inawekewa watu kuichunguza
 
Gender S. pole sana kwakukerwa na michango yetu kama ulivyo wewe kazini na sisi wengine tuko kazini. ndio line yako ya thinking very low for you

Ni kweli mimi pia niko kazini lakin i sio kama wewe.Mimi niko kwaajili ya kujadili facts na sio kufanya propaganda..Na ndio maana pamoja na kukufahamu nia yako kwa CHADEMA nimekuiwa nikikupongeza pale ambapo ulikuwa unasema kitu cha kweli.,nadhani hili hata wewe walifahamu..Lakini mwenzangu uko humu kwa njia ya kusema vibya vyama vya wenzakeo na hasa kuwasema vibaya viongozi wetu na hii ni kwa kuwa.Viongozi hawa wanakunyima usingizi kwa umahiri wao na kukubalika katika jamii ukilinganisha na hicho kichama chako cha kulia lia.lol.
 
Ni kweli mimi pia niko kazini lakin i sio kama wewe.Mimi niko kwaajili ya kujadili facts na sio kufanya propaganda..Na ndio maana pamoja na kukufahamu nia yako kwa CHADEMA nimekuiwa nikikupongeza pale ambapo ulikuwa unasema kitu cha kweli.,nadhani hili hata wewe walifahamu..Lakini mwenzangu uko humu kwa njia ya kusema vibya vyama vya wenzakeo na hasa kuwasema vibaya viongozi wetu na hii ni kwa kuwa.Viongozi hawa wanakunyima usingizi kwa umahiri wao na kukubalika katika jamii ukilinganisha na hicho kichama chako cha kulia lia.lol.

Unafaa kuwa mpambe kama Makamba kuliko kuwa Mbunge, may be nawe upo tayari kwenda jela kwa ajili ya Mbowe/Slaa.
 
Ni kweli mimi pia niko kazini lakin i sio kama wewe.Mimi niko kwaajili ya kujadili facts na sio kufanya propaganda..Na ndio maana pamoja na kukufahamu nia yako kwa CHADEMA nimekuiwa nikikupongeza pale ambapo ulikuwa unasema kitu cha kweli.,nadhani hili hata wewe walifahamu..Lakini mwenzangu uko humu kwa njia ya kusema vibya vyama vya wenzakeo na hasa kuwasema vibaya viongozi wetu na hii ni kwa kuwa.Viongozi hawa wanakunyima usingizi kwa umahiri wao na kukubalika katika jamii ukilinganisha na hicho kichama chako cha kulia lia.lol.

Unajua GS mimi huwa nawashangaa sana watu wa aina hii yaani mtu huwezi kuwa huru kifikira umenunuliwa hadi mawazo yako yamelipiwa kwamba hutakiwi kuchangia kutokana na weledi wako ila kutokana na ulivyopangiwa na bosi wako

huo ni utumwa wa ki psychologia ukishafikia hali hiyo huwa vigumu sana kurudia hali ya kawaida hata uambiwe vipi ni kama kupenda ukiambiwa mke wako ana chongo utasema hayo ni makengeza tu ndiyo maana utakuta mtu anang'ang'ania hoja kile kile hata kama kimejibiwa.
 
Unafaa kuwa mpambe kama Makamba kuliko kuwa Mbunge, may be nawe upo tayari kwenda jela kwa ajili ya Mbowe/Slaa.

Naona umeamu kurudi kwa jina lingine Bull..Umesahau hata wewe ni mpambe wa.....tena sio mpambe tu ni kibaraka.Mimi ninawatetea kwa kuwa ni vionozi wangu mahiri na ninawakubali na hawana kosa katika hili.Hapa tunajadili Ilani ya CHADEMA na si vinginevyo.
 
Tumain hebu kuwas na heshima hata kidogo..Dr Slaa hawezi kujisema mwenyewe hata siku moja.Wala hukuwa na Consern ya msingi ambayo ingetakiwa kujibiwa na Dr Slaa.Dr Slaa wala hahitaji huruma ya wanaJF kwani haimsaidii kitu.
Ni kweli kabisa wewe huna nia njema kwani uko kazini kwaajili ya kuishambulia CHADEMA na nido maana kila thresd ya CHADEMA lazima uchangie tena negatively.Majibu ya Dr Slaa ni mepesi tu lakini jamaa umahamaki ile mbaya,kama sio uko kazini ni nini?Hulali kazi kuisema vibaya..Hebu kuwa na soni hata kidogo.Lol

Mwache Slaa ajibu tafadhali wewe amekutuma umsaidie ujue huyo ni mwanasiasa ndio kazi yake kama hataki kujibu hakuna wa kumlazimisha asilalamike kwamba mimi sina nia njema yeye anajuaje kwamba sina nia njema? amekuwa yahaya?

Badala ushukuru nachangia kila thread ya chadema (negatively kuliko kusifiana ujinga) unakasirika kweli huko chadema kuna problem mnapenda ku-burst..nigekuwa silale ningekuwa mzima?

Pole sana kama unanifuatilia mimi nakupongeza kwa kazi uliyopewa ndio ajira zimeongezwa hongera..
 
Bull,
Kama unasoma vizuri threads, nadhani utaelewa Slaa alisema nini kuhusu OIC. It is not the same thing as what you are saying. Do justice to statements zilizowekwa, hata kama hutaki kumfanyia justice mtu. Nilisema na ninarudia, Ilani ya Chama haiwekwi na mtu, bali na vyombo vya maamuzi ya chama. Chadema ndio inafanya review ya Ilani yake kama vinavyofanya vyama vyote sasa. Hivyo ni unfair ku fanya judgment kabla hujauliza kama vikao husika vimekaa au la, na kama ni wakati mwafaka kutoa ilani sasa au la. Nadhani tutaendelea kuelimishana ili kujua proper procedures na ninajua kuwa ... kwa wakati mwafaka "kitaeleweka" kama si kwa mtu mmoja mmoja basi kwa sehemu kubwa ya jamii.


Asante sana Dr. Slaa kwa kujitokeza;

Kweli iko haja ya kufanya review kwenye ilani yenu ya 2010, kwa sababu hiyo ilani iliyowekwa na GS hapa jf ya 2005 nikchekesho,

Ilani ya 2010 inatakiwa iwe ya kitaalam na iangalie concern za wananchi, wataalam wa uchumi washirikishwe ili ionyeshe vipi ukipunguza VAT utaongeza pato la serikali na kwa njia gani

Ni kweli VAT kubwa inaathiri uchumi, lakini pia kumbuka kupunguza VAT kunaweza kusababisha inflation na kupunguza pato la serikali, matokeo wake uchumu kuaribika na engezeko la 35% kwenye elimu unalotaka litabaki ndoto!

Ilani ya 2005 imekaa kama maubiri, haiwezu kum convince mtu asiehudhuria kwenye mahubiri, safari hii wataalam wa uchumi washirikishwe. Thanks
 
Mwache Slaa ajibu tafadhali wewe amekutuma umsaidie ujue huyo ni mwanasiasa ndio kazi yake kama hataki kujibu hakuna wa kumlazimisha asilalamike kwamba mimi sina nia njema yeye anajuaje kwamba sina nia njema? amekuwa yahaya?

Badala ushukuru nachangia kila thread ya chadema (negatively kuliko kusifiana ujinga) unakasirika kweli huko chadema kuna problem mnapenda ku-burst..nigekuwa silale ningekuwa mzima?

Pole sana kama unanifuatilia mimi nakupongeza kwa kazi uliyopewa ndio ajira zimeongezwa hongera..

Ha ha ha!
 
Back
Top Bottom