Ili kupunguza tetesi za rushwa, Jaji Mkuu na Mahakama iwaondoe au iwalipe vizuri wasaidizi wa Majaji

Ili kupunguza tetesi za rushwa, Jaji Mkuu na Mahakama iwaondoe au iwalipe vizuri wasaidizi wa Majaji

chiembe

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2015
Posts
16,859
Reaction score
28,112
Kiuhalisia, wasaidizi wa Majaji ndio huandika hukumu, mishahara yao midogo, na inabidi waendelee kuishi.

Kuna tetesi kwamba wananchi wamefahamu kwamba hawa ndio huandika hukumu, zikiwemo za kesi za mauaji, na wanaishi mitaani na wananchi wa kawaida. Katika kuishi huko, basi Kuna tetesi kwamba ukitaka kutoboa, kesi yako, waone hao wasaidizi wa Majaji.

Na kutokana na wingi wa mashauri, Majaji Wana mida mchache wa kufanya uchambuzi wa majalada, hivyo wao hujikita kuangalia hukumu iliyokuwa drafted na Msaidizi wa Jaji.

Mahakama Ina mawili, iwalipe vizuri, hasa posho maalum ili waendane na hadhi ya wanayemsaidia, ama laa, mahakama ivunje hako ka tetesi kwa kuondoa wasaidizi hao, ili Majaji wafanye majukumu yao wenyewe, na hivyo inakuwa vigumu "kuingilika" kupitia wasaidizi hao.

Usaidizi wa Jaji wengi huuita kukaa "kijiweni"

Kwa kipindi kirefu Sasa mahakama kuu imekuwa haitoi haki halisi (substantive justice) hata kama inaonekana wazi, moja kati ya sababu ni hiyo, wakiona ushahidi "umebana sana" au hawana muda wa kusoma majalada mengi, mahakama yenyewe, bila kuulizwa au kuombwa na wadaawa, itaanza kufukunyua vikosa vidogo vidogo ili tu kuvuruga kesi.

Mahakama imegeuza mashauri ya wananchi kuwa mahali ya "hotuba na mihadhara" ya kisheria bila kujali mashauri hayo yamebeba haki za wananchi.

Wananchi wanasubiri hukumu kwamba shirika la bima limlipe au ardhi ni ya kwake, inatoka hukumu imejaa mahubiri ya sheria na makosa madogo madogo kabisa ambayo hayagusi haki za msingi
 
Wanaleta nadharia za sheria kwenye haki za watu. Jaji anasema hukumu ziangalie mihimili mingine na sio kuwa zibebe haki.

Ishu ya Rushwa ni uadilifu wa mtu mwenyewe ingawa nakubali kuwa kipato kidogo ni kishawishi cha kumbadilisha hata muadilifu kuwa mla rushwa. Kimsingi, watu wafanye kazi wanazozipenda au niseme watu wazipende kazi zao wanazofanya, ukiipenda kazi yako suala la maslahi haliwezi kukutesa kihivyo sababu priority yako ya kwanza ni kazi halafu ndio maslahi. Sasa wengi hawapendi kazi wanazozifanya, hapa ndipo masuala ya rushwa na vingine vinapofuata
 
Wanaleta nadharia za sheria kwenye haki za watu. Jaji anasema hukumu ziangalie mihimili mingine na sio kuwa zibebe haki.

Ishu ya Rushwa ni uadilifu wa mtu mwenyewe ingawa nakubali kuwa kipato kidogo ni kishawishi cha kumbadilisha hata muadilifu kuwa mla rushwa. Kimsingi, watu wafanye kazi wanazozipenda au niseme watu wazipende kazi zao wanazofanya, ukiipenda kazi yako suala la maslahi haliwezi kukutesa kihivyo sababu priority yako ya kwanza ni kazi halafu ndio maslahi. Sasa wengi hawapendi kazi wanazozifanya, hapa ndipo masuala ya rushwa na vingine vinapofuata
Kweli kabisa mkuu, Kuna kesi moja mawakili waliwasilisha hoja zao za rufaa kuhusu nani mmiliki wa ardhi kati ya wateja wao, wakamaliza, baadae Jaji akaanza kuwalazimisha waende kwenye mambo ya kisheria ambayo yataifuta kesi yenyewe, mawakili baadae wakiwa nje wanasema kwa utaratibu huo haki hazitapatikana kwa kuwa Majaji aidha ni wavivu kusoma majalada hivyo wanatafuta kamseleleko, au Wana kazi nyingi zimewaelemea, wanalazimisha upenyo jalada liondoke mikononi mwao.
 
Kweli kabisa mkuu, Kuna kesi moja mawakili waliwasilisha hoja zao za rufaa kuhusu nani mmiliki wa ardhi kati ya wateja wao, wakamaliza, baadae Jaji akaanza kuwalazimisha waende kwenye mambo ya kisheria ambayo yataifuta kesi yenyewe, mawakili baadae wakiwa nje wanasema kwa utaratibu huo haki hazitapatikana kwa kuwa Majaji aidha ni wavivu kusoma majalada hivyo wanatafuta kamseleleko, au Wana kazi nyingi zimewaelemea, wanalazimisha upenyo jalada liondoke mikononi mwao.
Hoja inakuwa haijabuliwa na upande wowote wa kesi, bali unakuta Jaji (Mahakama) inaibua yenyewe na kuiondosha kesi mahakamani. Mfano, hivi sasa mashauri yanafunguliwa kupitia Portal (mfumo wa kimtandao) inayoitwa JSDS, sasa kule unakuta wakili au muombaji amewasilisha maombi yake mapema ndani ya muda unaoruhusiwa kisheria, Msajili wa Mahakama kwa sababu anazojua mwenyewe, anakuja kuyapokea kimfumo maombi hayo muda wa kisheria ukiwa umepita.

Kesi inasajiliwa na nyaraka ngumu zinawasilishwa mahakamani, pande zote zinakuwa hazina ubishani kuhusu muda kwa kuwa zinajua waliochelewesha muda ni mahakama, Jaji anaibua hoja mwenyewe kuwa maombi yaliyo mbele yake yapo nje ya muda, anawataka mumuelezee uhalali wa maombi hayo, mnajieleza lakini anaamua kuyafuta maombi kuwa yapo nje ya muda. Hapo mmeshapoteza zaidi ya miezi 6 kusubiri kukutana na jaji halafu mnakutana nae ndio anatoa maamuzi ya aina hiyo, mnakata tamaa kabisa na haki inayocheleweshwa. Cha kushangaza ni kwamba majaji wenyewe wanajua changamoto ya mfumo ila hawajali
 
Back
Top Bottom