Ili Tanzania ibadilike lazima haya yafanyike

Ili Tanzania ibadilike lazima haya yafanyike

Lord denning

JF-Expert Member
Joined
Jun 3, 2015
Posts
15,819
Reaction score
33,255
1. Katiba Mpya - Lazima itungwe katiba mpya yenye meno inayoweka hatua anazopaswa kuchukuliwa kiongozi endapo ataivunja. Katiba hii iweke misingi ifuatayo;

a) Rais ateue Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama na Mawaziri tu- Akishateua lazima hao watu wathibitishwe na Bunge. Mawaziri wasiwe Wabunge

b) Majaji waombe kazi na kufanyiwa usahili kwenye public hearing na wanaofuzu ndo wateuliwe na Tume ya Utumishi wa Mahakama. Walindwe kweli na Katiba iliyo na meno.

c) Mikoa itambulike kama Kanda za kiuchumi na Wakuu wa Mikoa waombe kazi na kufanyiwa usahili unaofanyika kwa Public Hearing. Majukumu yao yawe kusimamia masuala ya kiuchumi katika mikoa
hiyo. RAS ndo wasimamie masuala yote ya Mikoa na wawe watumishi wa Umma wanaopangiwa kazi na Katibu Mkuu Kiongozi

d) Nafasi za Wakuu wa Mashirika ya Umma zisiwe za kuteuliwa. Watu waombe hizo kazi na wachujwe kwa kufanyiwa usahili. Wawajibike kwa Bodi zao na sio Wanasiasa.

e) Nafasi za DAS, DED zote ziwe ndani ya Utumishi wa Umma. Asipewe nafasi hizo nje ya Utumishi wa Umma. Na watumishi wa Umma waombe hizo nafasi na kufanyiwa usahili. Wawe na Kinga ya kutoingiliwa na mtu yeyote katika maamuzi ikiwemo wanasiasa.

f) Bunge- Kigezo cha kuwa Mbunge kiwe Elimu ya Chuo Kikuu

g) Siasa na Utendaji- Watendaji walindwe kikatiba dhidi ya Wanasiasa.

Tukifanikiwa kuwa na Katiba mpya na tukaweka haya tumetoboa
 
Ninahitajika kimoja tu.
Waelimike wananchi.
 
1. Katiba Mpya - Lazima itungwe katiba mpya yenye meno inayoweka hatua anazopaswa kuchukuliwa kiongozi endapo ataivunja. Katiba hii iweke misingi ifuatayo;

a) Rais ateue Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama na Mawaziri tu- Akishateua lazima hao watu wathibitishwe na Bunge. Mawaziri wasiwe Wabunge

b) Majaji waombe kazi na kufanyiwa usahili kwenye public hearing na wanaofuzu ndo wateuliwe na Tume ya Utumishi wa Mahakama. Walindwe kweli na Katiba iliyo na meno.

c) Mikoa itambulike kama Kanda za kiuchumi na Wakuu wa Mikoa waombe kazi na kufanyiwa usahili unaofanyika kwa Public Hearing. Majukumu yao yawe kusimamia masuala ya kiuchumi katika mikoa
hiyo. RAS ndo wasimamie masuala yote ya Mikoa na wawe watumishi wa Umma wanaopangiwa kazi na Katibu Mkuu Kiongozi

d) Nafasi za Wakuu wa Mashirika ya Umma zisiwe za kuteuliwa. Watu waombe hizo kazi na wachujwe kwa kufanyiwa usahili. Wawajibike kwa Bodi zao na sio Wanasiasa.

e) Nafasi za DAS, DED zote ziwe ndani ya Utumishi wa Umma. Asipewe nafasi hizo nje ya Utumishi wa Umma. Na watumishi wa Umma waombe hizo nafasi na kufanyiwa usahili. Wawe na Kinga ya kutoingiliwa na mtu yeyote katika maamuzi ikiwemo wanasiasa.

f) Bunge- Kigezo cha kuwa Mbunge kiwe Elimu ya Chuo Kikuu

g) Siasa na Utendaji- Watendaji walindwe kikatiba dhidi ya Wanasiasa.

Tukifanikiwa kuwa na Katiba mpya na tukaweka haya tumetoboa
si muhimu sana,
nadhani tunakwendra vizur sana hivi tulivyo sasa 🐒
 
Tukiendelea kwenda hivi siku si nyingi tutakuwa failed state
kutokana na misingi tulowekewa na waasisi wa Taifa letu,

kuna vitu ni ndoto za mchana kutokea Tanzania mathalani ulichokisema hapo juu 🐒

na sababu ya msingi ya uimara huo ni kwamba tumeweza kuwadhibiti vibaraka kupenya hususani kwenye maeneo mengine ya kutawala 🐒

Failed states nyingi, lakini pia hata zinazopitia hali ya mapigano na vita, ni kwasababu walizembea kuwadhibiti vibaraka katika nchi zao 🐒

haiwezekani Rais akawa anaegemea upande wa Ufaransa, halafu waziri Mkuu akawa rafiki wa karibu zaidi na Russia na mkuu wa majeshi ni kipenzi cha Uchina then eti mkwaza kuongoza nchi 🐒

haiwezekani,
coz there will be no comom leading or governing ideology. Mtafeli na mtapinduana tu 🐒
 
kutokana na misingi tulowekewa na waasisi wa Taifa letu,

kuna vitu ni ndoto za mchana kutokea Tanzania mathalani ulichokisema hapo juu 🐒

na sababu ya msingi ya uimara huo ni kwamba tumeweza kuwadhibiti vibaraka kupenya hususani kwenye maeneo mengine ya kutawala 🐒

Failed states nyingi, lakini pia hata zinazopitia hali ya mapigano na vita, ni kwasababu walizembea kuwadhibiti vibaraka katika nchi zao 🐒

haiwezekani Rais akawa anaegemea upande wa Ufaransa, halafu waziri Mkuu akawa rafiki wa karibu zaidi na Russia na mkuu wa majeshi ni kipenzi cha Uchina then eti mkwaza kuongoza nchi 🐒

haiwezekani,
coz there will be no comom leading or governing ideology. Mtafeli na mtapinduana tu 🐒
Mifumo itamlinda Rais.

Rais awe na control ya Wanasiasa ila sio Utendaji na mambo ya msingi ya Utendaji.

Hapo ndo tutakwenda mbele. Nchi nyingi zimefanikiwa kwenye mifumo hii inayotekeleza separation of powers hatutakuwa wa kwanza wala wa mwisho
 
Mifumo itamlinda Rais.

Rais awe na control ya Wanasiasa ila sio Utendaji na mambo ya msingi ya Utendaji.

Hapo ndo tutakwenda mbele. Nchi nyingi zimefanikiwa kwenye mifumo hii inayotekeleza separation of powers hatutakuwa wa kwanza wala wa mwisho
mi nadhani,
kama Tanzania ni kuongeza tu uwajibikaji zaidi na uwazi kwenye mihimili ya dola na kurekebisha machache ambayo labda ndio changamoto au kikwazo cha kusonga mbele kama ambavyo wachache mnapendekeza

hata hivyo mabadiliko unayopendekeza ni machache mno ukilinganisha na mazuri mengi sana ndani ya katiba iliyopo 🐒

na mabadiliko mengi itakua labda kubadili lugha, nukta, koma au paragraphs. Coz mengi ni yaleyale tyuuuu 🐒
 
Tanzania sio tu ni shamba la bibi tu, sasa limekuwa maabara ya tafiti za Demokrasia, Uundwaji wa Serikali, Uteuzi, Ufisadi, Uuzwaji wa Nyara za Serikali, Uangamizaji wa Jamii n.k n.k

Nchi hii, mawakala wa mabeberu wamejipanga kila kona kutaka kubadilisha Nchi! Wameifanya nchi yetu kuwa maabara ya mifumo ya Demokrasia.
====
Ukishabadilisha nchi, unapoteza utambulisho wako, unapoteza mila, desturi na Utamaduni wako.

Hayo yakishatokea, unapotea.

Hatahivyo....

Maboresho siku zote yanakaribishwa, ila isiwe kwa matakwa ya mabeberu na kutulazimisha kufuata mila, desturi na utamaduni wa Kigeni ili waje waseme 'sasa mmendelea' .Tuwakemehe na kupinga dhana ya kwamba, tukifanya yanayo washindwa wao, basi tutaendelea.

Stop disrupting our country and stop insulting the countries Intelligence.
 
Back
Top Bottom