Ilibaki kidogo mvua ziniharibia mazao yangu

GITWA

JF-Expert Member
Joined
Apr 1, 2012
Posts
1,572
Reaction score
1,781
Nililima maharage mwanzo mwishoni mwa mwezi wa tatu wilayani Hanang, baada ya hapo mvua zikaanza kunyesha mfululizo na ardhi niliyopanda ni mbuga nyeusi.

Yaani maharage yalitaka kuniacha nayaona hivi ila nashukuru Mungu amemipa maarifa ya kuyapambania

Maharage yenyewe ndio hayo.
 
Jazia nyama bado haujaeleweka vema juu ya yaliyokusibu
 
Heka ngapi mbona kama kidogo kama umelenga kufanya biashara?
 
Yaani hapo mkuu kila baada ya siku tano nipo shambani na booster & dawa ya baridi na ukungu
 
Nipasua kichwa lakini ukivumilia mwaka kitakaokubari unasahau shida zako. Yaani mwaka mmoja tu ukiwa umelima kuanzia ekari kumi na kuendelea unaweza kuuga ufukara kama mazao yamekubari.
 
Hongera aisee hapo bila dawa za barid ungekua umezika pesa
 
Yaani hapo mkuu kila baada ya siku tano nipo shambani na booster & dawa ya baridi na ukungu
Hapo sawa kiongozi maana ukanda huo kuna baridi usipofanya hivyo utavuna mabua.
 
Hongera aisee hapo bila dawa za barid ungekua umezika pesa
Yaani mpaka majirani shambani wamenishangaa Kuna mmoja jirani kaunguza ekari tano za maharage Sasa hivi anataka kupanda dengu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…