Mafiningo
JF-Expert Member
- Sep 5, 2016
- 4,435
- 4,662
Hakika kila mbabe ana mwamba wake, hivi ninavyoandika hii Dk 45 za first half zimemalizika na kwa kweli Azam ndio waliokuwa juu kwa kila kitu na kila idara.<br /><br />Kumbe Yanga ni timu mbovu kiasi hiki?<br /><br />Kama Azam wangekuwa makini mpaka dk hii wangekuwa wako mbele kwa mabao matano, ngoja tuendelee kuangalia .<br /><br />Kamusoko hoi kwa Salum Abubakar!<br />========<br /><br />Yanga imekubali kipigo cha magoli manne bila majibu kutoka kwa Azam FC mjini Zanzibar katika michuano ya mapinduzi inayoendelea ikiwa ni kipigo chake cha kwanza tangu michuano hio ianze.<br /><br />Sasa Yanga itasubiri mshindi kati ya Simba na Jang'ombe boys ambao watacheza kesho jioni.<br /><br />USHAURI - YANGA IJITOE KWENYE MICHUANO HII ILI KULINDA HESHIMA YAKE , SIKU IKIKUTANA NA MNYAMA WATAADHIRIKA ZAIDI , HERI LAWAMA KULIKO FEDHEHA .