Ilikuwa ni busara kuendelea kiujumla na mipaka iliyoachwa na Wakoloni kwa nchi huru za Africa baada ya uhuru?

Ilikuwa ni busara kuendelea kiujumla na mipaka iliyoachwa na Wakoloni kwa nchi huru za Africa baada ya uhuru?

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Mojawapo ya maazimio na makubaliano ya mwanzo kabisa waliyowafanya viongozi wa nchi za Africa zilizojipatia uhuru miaka ya 1960's ni kuendelea kuheshimu mipaka ya nchi iliyoachwa na wakoloni.

Haya makubaliano ya kiujumla jumla hivi yalikuwa sahihi ukizingatia mipaka ya mataifa ya Africa iliamuliwa na watu huko Berlin mwaka 1884 kwa vigezo vya kijinga na kipuuzi sana? Watu wenyewe waliokuwa wanaamua mipaka ya nchi za Africa walikuwa hawajui mengi sana kuhusu Africa na watu wake.

Je, Haikuwa busara kwa viongozi wa Africa huru kukaa chini miaka hiyo na kukubaliana kwa kurekebisha mipaka iliyoachwa na wakoloni wao?
 
Back
Top Bottom