Ilikuwa rahisi kwa CHADEMA kuchukua nchi wakati wa Magufuli, huyu wa sasa amebow kwa mabeberu they will protect her position

CHADEMA ipi ya kuchukua Nchi?!!!!! Hii ambayo mtu mmoja yuko lockup na yenyewe imejifia!
Wale akina Msigwa niliowaona wanakula apples bila kunawa ndo waongoze Nchi! Ebu jaribuni kuwa serious na mambo ya msingi!
 
Kwa namna yoyote ile mtu anaeilaumu chadema kwamba ilifanya uzembe kwakutokutwaa madaraka anachochea machafuko kama njia sahihi maana njia za kidemokrasia zote zilihujumiwa barabara.
 
Kulikuwa na tume ya kuwatanga CHADEMA?
 
Kwa namna yoyote ile mtu anaeilaumu chadema kwamba ilifanya uzembe kwakutokutwaa madaraka anachochea machafuko kama njia sahihi maana njia za kidemokrasia zote zilihujumiwa barabara.
Kwanza hapa kuwa na uchaguzi isipokuwa ni uchafuzi tupu
 
CHADEMA ipi ya kuchukua Nchi?!!!!! Hii ambayo mtu mmoja yuko lockup na yenyewe imejifia!
Wale akina Msigwa niliowaona wanakula apples bila kunawa ndo waongoze Nchi! Ebu jaribuni kuwa serious na mambo ya msingi!
Siku dola itakapowaacha yatima ndio mtaelewa salama yenu ni kuajiri polisi wajinga waliofeli shule.
 

Unaona labda utatupoteza na huu upotoshaji wako, Magufuli si alitumia vyombo vya dola kubaki madarakani na kusema hili ni taifa huru? Hivyo mnavyosema wazungu wanafaidika navyo ni vipi hivyo ambavyo wakati wa Magufuli tulifaidika navyo, na sasa wazungu ndio wanavipata? Huu ujinga mnaoongea humu huwa mnaridhishana au mmezaliwa nao?
 

Huyu aliyeleta hii mada ana msongo wa mawazo na sasa hajui amtupie nani lawama.
 
Nakubaliana na wewe kwa 100%. Ila kama Magufuli angeendelea kuwapo angewaua viongozi wote wa CHADEMA kama ambavyo Paul Kagame anavyowaua wabaya wake.

Kuondoka kwa Tundu Lissu kupitia Germany embassy, Mbowe kukimbilia Dubai na Godbless Lema kupitia Namanga na kukamatwa Kajiado Kenya ni kwamba Waliepusha maisha yao baada ya Magufuli kutaka kuwapoteza mazima.

Kwa kweli baada ya Rais SSH kuwa madarakani walihitaji wamsome kwanza ndiyo wajue wanaweka mkakati gani kukabiliana naye.

Kuwa chama cha UPINZANI siyo lazima ushike madaraka ya Dola, ila ikitokea unashika. Yatosha tu kuwa pressure group ili kuifanya Serikali iwajibike.

Mama anaupiga mwingi, ni mtu mmoja mwema sana. Hana shida na mtu, hapendi DHULUMA. CDM wajifunze wajitafkari siasa zao za matusi waziache.

Waliolishwa tango pori ni akina Mbowe kuanza kum pump na Katiba mpya bila respect kuwa ni Rais wa nchi. I assure you timing ya Mbowe kwenye Katiba mpya ilikuwa ni grave mistake na sijui nani alimshauri afanye muda ule. Sasa angalia akina Lissu wanavyojuchukulia ujiko.

Nchi hizi za Kiafrika siasa zetu ni ngumu sana kumfanya mpinzani awe Rais. Ili ukubalike kuwa Rais lazima SYSTEM ikukubali. Waweza kuwa popular lakini usiwe Rais.

Tuangalie uchaguzi wa Kenya mwezi August 2022. Rutto ni popular kwa utajiri alionao, lakini system iko na Raila Odinga.
 
Ilishawahi kutokea Marekani walipandikiza Rais baadhi ya nchi kwa kutumia CIA kwa kumuondoa raisi aliekuwa madarakani, Dunia Ina Siri nyingi
 
Upo sawa kwamba Magufuli hakuwa backed na unaowaita mabeberu,lakini aliweza kuitumia nguvu kubwa inayoambatana na cheo cha uraisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania,mfano hata kabla ya uchaguzi wenyewe kufanywa tayari ccm ilikuwa na wabunge wanaozidi 50 kwa madai kwamba eti wamekosa mpinzani.
Ushauri wangu: Ili kuiondoa ccm madarakani,(1) katiba mpya ipatikane (2) Vyama vyote vya upinzani viungane na kusimamisha mgombea mmoja,iwe wa uraisi au ubunge.
 
Labda chadema waombe serikali ya umoja wa kitaifa angalau waingie serikali I wapate vyeo Kama spika, makamo etc
 
Rais kumbe anachaguliwa na mabeberu sio wananchi kwenye sanduku la kura
 
Huyu macho kumchuzi atajua hajui 2025,meko alijificha dom na kujitangaza wakati kapigwa kwa kura nyingi na cdm...ndio kazalisha wabunge wahovyohovyo
 
Mkuu, ukisoma hisia za makundi ya watu wengi hivi sasa, wameng'amua kuwa JPM alikuwa ni mlinzi bora wa rasilimali za nchi yetu. Licha ya uongozi wake wa kiimla, lakini alikuwa ni kiongozi thabiti, mwenye uchu mkubwa wa maendeleo ya nchi yake, na mwenye msimamo mkali na usioyumba.

Licha ya mapungufu yake ya kukandamiza demokrasia, lakini kwa hakika ni kiongozi ambaye ambaye Tanzania ilimuhitaji atufikishe hadi mwaka 2025. Ni kiongozi ambaye alichukia kujirahisisha kwa nchi tajiri kisa eti afikiriwe kupewa mikopo yenye masharti.

Baniani mbaya lakini kiatu chake sawa. Wengi wameanza kukumisi sana, ila inakuwa vigumu kufanya hivyo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…