Imani ya dini yako je ina nafasi katika uhusiano ??

Safety last

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2011
Posts
4,236
Reaction score
1,411
Nauliza sababu nimeshuhudia wamama wengi walioolewa na (waislam wakifika umri wa makamo wanarudia imani yao ya awali ya ukristo,au the opposite)dini inanafasi ya kuwa na uhusiano uliobora na kustawisha familia!ukiwauliza wanasema there's incompatibility in religion walioingia kwa kusema "nimempenda na dini si kitu bora mapenzi"je mtu anapendwa au dini inapendwa(inafuatwa) sababu ya mafundisho yake,imani ya mtu na mtu ni kitu kimoja au utofauti ni upi !!
 
Mh hilo angalizo lako linabagua na kunyanyapaa! Ina maana utamzuia mtu asiye na hulka ya dini (sijui ndo yukoje) asichangie hata kama ana mawazo mazuri yenye mafunzo!

Mimi ninaamini katika kumuabudu Muumba mmoja na alituumba sote kwa utofauti wetu itherwise asingekuwa anaruhusu kufall na watu wasio dini yako! Kama kuna namna ya kutafsiri dini kwani inawezekana kwangu nadhani nina tafsiri tofauti na yako!
 
Kimsingi ni vibaya kumbadili mtu dini ili tu umuoe....
Ni vizuri kabla ya kumbadilisha dini mtu umshawishi ili ajifunze imani yako na mwisho maamuzi
ya kubadili dini au la ywe ya kwake tu bila shinikizo

zipo ndoa nyingi imara ambazo watu wapo kila mtu na dini yake....
 
mshikaji wangu kakosa mke kisa dini. Kwao na mwanamke wametia ngumu binti haolewi na mtu asiye wa imani yao. I couldn't believe kitu hii yaweza kutokea katika dunia ya leo but seeing is believing
 
well said!! I like it!! Good night!!!!!!
 
Binafsi ina nafasi hasa kama ni mahusiano ya kuelekea kwenye ndoa.
Sipendi kubadili dini sababu ya kuolewa na nisingependa kumbadilisha mtu imani. Nachukulia kubadili dini ni kukosa msimamo na wengi ninaowajua waliobadili wameprove hilo. Hata mtu akibadili kwa ajili yangu nitamchukulia ni mtu asiye na msimamo.
 
To speak my mind nafasi ipo as far as birds of the same feather flock together....misingi ya kidini ikifanania it can make maisha ya wahusika yakawa smooth in different matters pattaining to them.
 

ukweli unabakia ya kuwa mahusiano ya kiroho yanongoza mahusiano ya kimwili kwa kila kitu............kama ya kiroho ni mabaya hata ya kimwili yatakuwa hovyo.................................ukiona wanarudia imani zao za awali ni baada ya kukamilisha malengo ya kidunia...............
 

Haya mawazo yana walakini Mungu wa wakristu ana jina na jina lake ni Yesu Kristu.......................na wengine wamemkataa hivyo hatuwezi wote kuwa tunamwabudu Mungu yuleyule.....................................ni lazima wako wanaomwabudu Mungu wa kweli na wengineo wanaabudu asiye wa kweli...............the deceiver.........kumbuka Lucifer naye anausongo wa kuabudiwa kama Muumba....................so watchout...........
 

The Boss umesema vema sana .nakubaliana na wewe
 

Biblia inakataza kuoana na wale wa mataifa kwa mfano, hilo unaliongeleaje?
 
<br />
<br />
nakupa mfano:


Tuseme we ni muislam!

unakutana na wanaume wawili, kati ya hao ukatokea kumpenda sana, lakini huyo uliempenda kwa dhati na yeye amekupenda unakuta ni mkristo,

sasa, uko tayari kuusaliti moyo wako kuwa na huyo ambae ni wa dini yako bt hujampenda na kumwacha mpendwa wako kisa dini?
 
bora kubadili kabila tu lol
Hapa ndio kila mwenye akili timamu atagunduwa kwamba kabila ndio lina maana zaidi kuliko dini ni takataka tu. maana huwezi kubadili kabila lakini unaweza kubadili dini. hapa naona dini haina mashiko na uzembe kuona dini ni kitu cha maana wakati hakina nguvu kushinda kabila lako.
 
Tupe aya....

Deuteronomy 7:1-4

American Standard Version (ASV)

Deuteronomy 7

1 When Jehovah thy God shall bring thee into the land whither thou goest to possess it, and shall cast out many nations before thee, the Hittite, and the Girgashite, and the Amorite, and the Canaanite, and the Perizzite, and the Hivite, and the Jebusite, seven nations greater and mightier than thou;

2 and when Jehovah thy God shall deliver them up before thee, and thou shalt smite them; then thou shalt utterly destroy them: thou shalt make no covenant with them, nor show mercy unto them;

3 neither shalt thou make marriages with them; thy daughter thou shalt not give unto his son, nor his daughter shalt thou take unto thy son.

4 For he will turn away thy son from following me, that they may serve other gods: so will the anger of Jehovah be kindled against you, and he will destroy thee quickly.
 
dini inanafasi ya kuwa na uhusiano uliobora na kustawisha familia! je mtu anapendwa au dini inapendwa(inafuatwa) sababu ya mafundisho yake,imani ya mtu na mtu ni kitu kimoja au utofauti ni upi !!

Mkuu .. Binafsi naamini kuna tafsiri mbili unapoongea kuhusu dini au imani.

1. Kuna wale wanaotumia dini kukinga mabaya yao na kwa maslahi yao binafsi na si vile Mungu anavyotaka. Wanatumia maandiko kupotosha nia njema ya imani na uhusiano na Mungu. Hapa namaanisha wale wanaopiga kelele kwa sauti kubwa kutumia kigezo cha dini (Kikiristu, Islam, Budha etc) lakini giza likiingia wanageuka kuwa simba wakali na wako tayali kuua hata wenzao wenye imani sawa na wao.

2. Kuna wale ambao wako kimya, Wana imani ya juu ya kile wanachoamini hadi wanakubali kuwa Mungu ni wa upendo na Amani. Aina ya watu hawa hawajali binadamu mwenzake ana dini gani ili mradi kama huyo mwenzake anayo amani na upendo na anamtukuza na kumtii Mungu kwa vile anavyoamini na siyo kinafiki. Mara nyingi watu kama hawa hawajali mwenza/mke wake ni wa dini gani. Imani imempeleka mbali zaidi na anaamini yeyote anayeamini Mungu wa kweli na kutii sheria zake basi ni mmoja wake bila kujali dini au dhehebu.

Swala la kuchanganya dini katika familia yako utaamua wewe mwenyewe kutokana na uko kwenye kundi gani la hapo juu, ingawa kama utakuwa kundi la pili unaweza kupata kipingamizi toka kwa baadhi ya mafundisho ya baadhi za dini na changamoto na jamii inayokuzunguka. Lakini mwisho wa yote.. Kitakacho kuweka karibu na Mola ni matendo yako kwa mwenzako na siyo kelele na unafiki wa hapa duniani.
 


Aksante Ruta nayaheshimu sana mawazo yako, tafadhali zingatia msitari wangu wa mwisho kwenye post yangu. Aksante

Biblia inakataza kuoana na wale wa mataifa kwa mfano, hilo unaliongeleaje?

...Na Biblia hiyo hiyo inatwambia Nendeni ulimwenguni mkawafanya mataifa kuwa watu wangu.................utawafanyaje watu wa MUNGU wako kama unawabagua?! Najua mtakuja na mwingine usemao 'Msifungiwe nira, na wasio amini!" laiti tungeielewa vema maana ya 'kufungiwa nira'. Nisingependa kwenda ndani sana na mjadala huu wa dini. Aksante kwa angalizo.
Ubarikiwe
 

Tulizo aksante natamani ungeongeza sauti ukasikika vizuri zaidi.

Unajua wengi tunatafsiri dini kutokana na mapatilizi ya Vitabu na mafundisho tunayojifunza. Tunakuwia kama tumekremu.....mtu anajiita mshika dini kwa kuwa tu anatoa zaka, anakwenda kwenye nyumba za ibada kila sikulakini anamchukia jirani, ana kisasi na ndugu, fisadi n.k. Unajiuliza dini ni nini kwa huyu mtu? hupati jibu. eh hebu nikae kimya mie!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…