Imefika wakati serikali iangalie mishahara ya watumishi wa "Local government" maana hali zao za mishahara ni ngumu na mbovu sana

Ila ukiangalia vizuri, halmashauri ndio ina hudumia wateja wengi kuliko ofisi zoteee.

#YNWA
Kuna mambo ukiyaangalia ni ROHO MBAYA tu.

Imagine, mtumishi wa Halmashauri ndio anapambana KUZALISHA, KUHUDUMIA WANANCHI wengi na KUKUSANYA MAPATO.

Lakini hata pesa tu ya likizo ni shida.

Yaani, Halmashauri ziko tayari kutoa 10% za kisiasa kukopesha vikundi vya Wanawake, vijana na walemavu AMBAZO Mara nyingi hazirudi. Lakini siyo kumlipa mtumishi overtime.
 
Hilo swala la kuitambua Elimu ya Shahada ya Pili (Masters) naiomba serikali ikiona Kuna ulazima ilifanyie kazi...hii nahisi ni Tz tu, nenda Kenya au Uganda hapo masters Ina mshahara wake kwa kila idara
 
Unaonea huruma walimu kwanini isiwe masjala ,secretaries ,na wengineo
 
Binafsi nafikiri wangeangalia upya mfumo wa Posho kwani kuna kuwa hela nyingi sana inafloat. Namaanisha mfumo wa posho unanufaisha wachache na kuacha wengi na mishahara kidogo. Nahii inaweza kusaidia Kuboresha mishahara bila kuadhiri bajeti.
Nijuavyo huko sector Binafsi hakuna sana mfumo wa posho na ndio sababu watu hufikiri mishahara ni mikubwa.
Ila kiuhalisia huko Serikalini kuna idara nyingi tu zina mishahara mikubwa kuliko private tofauti yake huupata kupitia posho
 
Mifumo ya posho,sheria, KANUNI na taratibu za serikali nyingi siyo mbaya.

Tatizo kubwa hazitekelezwi na HAKUNA msaada.

Mfano, waraka wa serikali unataka posho ya kazi nje ya Kituo chako ni Tsh120,000 lakini usipopewa huna Cha kufanya au itabaki unadai mpaka siku ya kustaafu 😅
 
Umeandika point sana. Mama anasoma humu atasikia na atafanya.

Sent from my M10_Max using JamiiForums mobile app
 
Kumbuka kuna watu wanaitaka hyo pesa kidogo mkuu. Tushukuru tunachopata hata kama ni kidogo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…