Imeniuma golkipa Ismail suma kufariki na kuzikwa Burundi.

Imeniuma golkipa Ismail suma kufariki na kuzikwa Burundi.

olekamaru

Member
Joined
Jun 23, 2017
Posts
78
Reaction score
74
Wiki hii taarifa za kufariki kwa golkipa wa zamani wa timu za simba na yanga Ismail suma kufariki dunia kule Bujumbura Burundi na amelazimika kuzikwa huko na majirani kutokana na kile kilichoelezwa Ndugu zake kushindwa kumudu gharama za kuufuata mwili wake.imeuma sana kwani sio Tff wala simba na yanga hata prison ya Mbeya ambao ni waajiri wake wa zamani walioguswa na hili.hata hawa wanaojiita sputanza chama cha wachaezaji Tanzania wamekaa kimya.soka letu lina malaria zaid ya milioni moja na sijui lini tutaimarika kwani soka sio uwanjani tuu hata nje ya uwanja pia.
 
Suma ametoa mchango mkubwa katika soka la nchi hii lakini leo TFF wanakaa kimya hadi kijana huyu anazikwa kama mkimbizi katika nchi jirani ya watu wengine, SHAMEFULLY ! Hawa mabalozi wetu katika nchi hizo wana faida gani ya kuwepo huko? Nimeumia sana kwa tukio la Suma.
 
Sijui kwann Tanzania kila kitu ni ubabaishaji.Wazir wa michezo anaecheza na mitandao kila siku cjui hili hajaliona au nn
 
Ingependeza azikiwe hapa nyumbani lkn pia ktk uislam, mtu (mwislam) akifa popote azikwe hapo as long kuna waislam na zikafuatwa taratibu zote za kuzika za kiislam. Dunia/Ardhi yote ni faradhi
Kiimani ni saw a na tunashkuru sana kwa walichokifanya ila kwa alivyotumikia soka ni kama familia ya soka imemtenga
 
Tanzania hakuna kitu tunajua, ni vile hakuna mashindano ya kiuongozi, vyuo, uvumbuzi/ugunduzi, kilimo, ufugaji, kutunza mazingira, mipango miji. nk

kila kitu tuko mwisho mwisho
 
Tunakomaa na ishu za uchochez tu na mitandaoni nn kinapostiwa
 
Back
Top Bottom