IMF: Kasi ya Ukuaji wa Uchumi wa Uganda Kufikia 11% Kuanzia Mwaka 2025 Baada ya Pesa za Mafuta Kuanza Kumiminika

Rudi kwenye mada,achana na Egypt
Nipo kwenye mada ila hutaki kunielewa nini najaribu kukieleza.
Hilo la 40% misaada nitalifanyia tafiti kulihakikisha.

Tuje kwenye uchumi wa Ethiopia uliodai kuwa haujawapa mnufaiko kwasababu ya majanga ya kiasili kama ukame na vurugu za ndani.
-Egypt ni nchi yenye jangwa kubwa naweza sema kuliko Ethiopia,ila imeanzisha kilimo cha kisasa na sasa haina shida ya vyakula.
-Egypt imechimba visima vikubwa kuhakikisha uwepo wa maji kwa miji ya mbali iliyo na vyanzo haba vya maji.
-Egypt ina maendeleo ya kijamii makubwa sana kuanzia usafiri wa umma,elimu,afya n.k n.k.
Pia hii Egypt imepitia vita nyingi kubwa za ndani na nje kuliko hata Ethiopia.
Tukianzia 1967 six days war kuja 1973 Yomkippur War,kuja kwenye kupinduana viongozi kwa viongozi hadi kipindi cha kuuliwa Mohammed Morsi ambapo wafuasi wa Morsi walianzisha vita za mitaa ndani ya Cairo.
Ila Egypt haikuyumba kiuchumi.

Sasa hizo sababu ulizoziweka kwa Ethiopia mbona Egypt anazo mara mbili yake na bado kapiga hatua!???
Pia bajeti za fedha zote hizo Ethiopia wanazopitisha zinaenda wapi ilhali huduma za afya mbovu!??
Maana andiko uliloleta yaonesha Ethiopia ina bajeti kubwa sana kuliko Tanzania.
Ila sijaona miradi yenye tija ya kuwagusa wananchi hapo Ethiopia.
 
Mbona wetu haukuweza kupanda baada ya kuanza kuchumba dhahabu na sasa kuna gesi tunakosea wapi na kuuza loliondo na kubinafsisha hoteli za kitalii
 
Hilo la 40% ni uongo na halipo ndio maana unatapatapa.

Mada ni Tanzania kujifunza Kwa Ethiopia kufikia Ukuaji wa over 10% growth rates of GDP vinginevyo tutapitwa na Uganda.

Egypt Haina majanga Bali Ukame ndio hali Yao ya maisha ya Kila siku wametafita mbinu za ku survive na ku glorish kwenye Hali hiyo kinyume na Ethiopia au Tanzania ambazo zinategemea huruma ya hali ya hewa kwenye Kilimo so Ukame ukija inageuka kuwa janga.

By the way Nchi karibu zote Kwa Sasa ikiwepo Ethiopia imeanza kufanya irrigation farming.

Mwisho kwamba Egypt Ina internal wars kama Ethiopia au Ina vita na majirani kama Eritrea? Wacha blaa blaa.
 
Mbona wetu haukuweza kupanda baada ya kuanza kuchumba dhahabu na sasa kuna gesi tunakosea wapi na kuuza loliondo na kubinafsisha hoteli za kitalii
Fedha za dhahabu sio nyingi kama za MafutaπŸ‘‡πŸ‘‡


Cc August Vyote hivyo unavyosema vinafanyika Loliondo vinalenga kukuza zaidi Uchumi.
 
Hilo la huko juu liache mkuu nikishindwa kuthibitisha nitakwambia.

Egypt ina jangwa kubwa sana,nadhani unafahamu ubaya wa jangwa.
Egypt imepigana vita nyingi kuliko Ethiopia.

Sasa kwanini hiyo bajeti kubwa ambayo Ethiopia inaipitisha bungeni isifanye vital projects kwa raia wake!??
Nikuletee hali za huduma za kijamii za Ethiopia mkuu!??
Kuonesha kuwa nchi ina uchumi mkubwa ilhali raia hali taabani kuna kipi cha kujifunza hapo!??

Ni sawa unaambiwa "mwashambwa ana pesa nyingi tuige mfano wake"ila analala nyumba inavuja na anavaa nguo za kuchanika.
Kuna la kujifunza hapo!??

Uganda ndio hata usiongee tukianza kuielezea hapa.
 
Hivi unafahamu kwamba na Tanzania ni wabia wakubwa wa mradi? Hyo impact itaonekana na Tanzania pia japo sio kwa % kama hzo.
 
UCHUMI WA TANZANIA UTAFAIDIKA PAKUBWA NA MAFUTA YA UGANDA KWA KILA PIPA LITALOUZWA TANZANIA ITAPATA DOLA 12
 
Hivi unafahamu kwamba na Tanzania ni wabia wakubwa wa mradi? Hyo impact itaonekana na Tanzania pia japo sio kwa % kama hzo.
Tanzania tutapata tozo ya kupitishia Mafuta tuu sio zaidi ya hicho kulingana na percentage ya umiliki Wetu.

Na Kwa mwaka ni roughly less than 3 Trilion,lakini Uganda itapata hela za mauzo ya Mafuta na kiwanda Cha Kusafisha wanauza kiasi kwamba Oil down stream yake ni kubwa.
 
UCHUMI WA TANZANIA UTAFAIDIKA PAKUBWA NA MAFUTA YA UGANDA KWA KILA PIPA LITALOUZWA TANZANIA ITAPATA DOLA 12
Less than 3T per year Kwa hesabu ya mapipa 200k Kwa siku.

Sasa hiyo ni hela ya mboga tuu Kwa Tanzania
 
Sasa utaongeza GDP per Capita bila kuongeza GDP size?

Mapesa ambayo Uganda itavuna kwenye Mafuta yanaenda kuwekeza kwenye Huduma za jamii na Uchumi hivyo kuwarahisishia Waganda kuongeza vipato Vyao.
GDP inaweza kuongezeka lakini kama hakuna urari ktk distribution of national cake then large portion inabaki kwa akina Mo Dewji na Bakhressa
Vilevile inategemea na idadi ya watu uliyonao
 
Hayo sio maswali.Tofautisha wenye Hali Yao na ambao wame adapt vs ambao sio hali Yao ila yanawakumba ,means za kukabiliana itakuwa tofauti.

Mwisho Ukubwa wa Ethiopia sio sawa na Egypt on top of that Ethiopia Iko kwenye vita vya wenyewe Kwa wenyewe na baiana ya majirani mambo ambayo Ethiopia haipo.
 
GDP inaweza kuongezeka lakini kama hakuna urari ktk distribution of national cake then large portion inabaki kwa akina Mo Dewji na Bakhressa
Vilevile inategemea na idadi ya watu uliyonao
Sawa lakini Kwa Tanzania tuna urali mzuri kuliko maeneo mengi.
 
Tanzania tutaendelea kuwa maskini kwa muda mrefu sana mpaka tubadili aina ya siasa na namna tunavyopata watumishi wa umma.

Bila kufanya hivyo kila nchi hata Burundi itatupita tutabakia omba omba kwa muda mrefu sana.
 
Muda sio mchache UGANDA atatuacha tz kwenye all aspects za uchumi. Kule uganda neno eti mnyonge asilipe kodi wanakaribia kulifuta. Mnyonge asilipe kodi ipo tz tuuu sasa jana usiku alikula wapi kama hana kodi ya kulipa.
Mnyonge alipe kodi kwa viwango vinavyokubalika na viwango rafiki.

Siku KAINERUGABHA atakapo thibitishwa rasmi ndie rais wa UGANDA tz tutaachwa kwa kasi ya 4G
 
Usisingizie vita mkuu.
Vurugu ndogo za kikabila tu hizo.
Egypt kapita vita kubwa ambazo kama Ethiopia angevipitia asingesimama maisha yake yootee.


Sawa basi niambie,bajeti kubwa inayopitishwa kwenye bunge la Ethiopia inafanya nini!??
Maana hakuna mabadiliko kwa raia hata kwa nchi.
Hakuna hata mabadiliko ya huduma za kijamii.
Nielekeze mkuu HIZO PESA ZINATUMIKA WAPI YA BAJETI KUBWA HIVYO!?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…