IMF yaionya serikali ya Kenya kuhusu deni la taifa

IMF yaionya serikali ya Kenya kuhusu deni la taifa

REDEEMER.

JF-Expert Member
Joined
Feb 22, 2015
Posts
8,925
Reaction score
14,890
IMG_20171124_141853.JPG


Shirika la fedha duniani (IMF) limetoa wito kwa serikali ya Kenya kuchukua hatua za dharura kudhibiti ongezeko la deni la kitaifa ambalo sasa linakadiriwa kukaribia asilimia 60 ya pato la taifa.

Mwakilishi wa IMF nchini Kenya, Jan Mikkelsen ameonya kuwa kuongezeka kwa mkopo wa taifa kutaathiri vibaya bajeti ya taifa, shughuli za benki nchini na hatimaye kusababisha wakopeshaji kusita kutoa mikopo zaidi. “Tunatoa wito kwa serikali ya Kenya kuanza mikakati ya kudhibiti ongezeko mkopo wa taifa,” Mikkelsen alisema jijini Nairobi. Alieleza wasiwasi kuwa uchumi wa Kenya haukui kwa kasi ya kuweza kuzalisha fedha za kutosha kulipa deni ambalo sasa ni asilimia 57 ya pato la taifa.
 
Kenya mambo ya uchaguzi wa kuegemea ukabila yatawalaza njaa.
Ona sasa kuna mdororo wa uchumi ndio maana pesa haizalishwi ipasavyo
 
Back
Top Bottom