Ina maana DAWASA hawasafishi na kuzibua visima hadi kutokee uhaba wa maji?

Ina maana DAWASA hawasafishi na kuzibua visima hadi kutokee uhaba wa maji?

Black Butterfly

Senior Member
Joined
Aug 31, 2022
Posts
130
Reaction score
368
Jamani hivi mmegundua kuwa tangu itangazwe kuwa kuna upungufu wa Maji unaosababisha mgawo, DAWASA wameanza kuzibua Visima 161 mitaani huko ambavyo havikuwa vikifanya kazi.

Kwa jinsi hali ilivyo ni wazi kabisa kuwa hawa jamaa DAWASA hawana kawaida ya kuchukua tahadhari yoyote kuhusu dharula ya Maji hasa kwa nyakati za kiangazi au hali yoyote itakayojitokeza hasa kwa jiji la Dar es salaam.

Nadhani imefika wakati sasa Serikali ifikirie kutoa nafasi kwa sekta binafsi ziendeshe miradi yenye mahitaji muhimu ikiwemo umeme na maji ili kuleta ushindani kwenye huduma lakini iweke sheria za udhibiti wa bei na ubora.

Maana kwa hal hii tunaenda kubaya sana huko mbele, wiki ya pili mitaani hakuna maji na viongozi bado wako ofisini, uwajibikaji uko wapi sasa jamani?

1667561853288.png
 
Aisee hata mimi nimeshangaa sana,na hawana hata aibu na video wakapigwa..kuna wakati mambo yanayofanyika hii nchi unabaki unawaza huenda sisi ni binadamu toleo la mwisho.
 
We are not proactive, we are reactive.
MTU anatoka kwake baada ya kula supu ya utumbo, anaingia kwenye V 8. Akifika ofisini anafikiria kumkomoa deputy wake ambae Ni kabila tatauti na lake, au anawaza wanawake hada wafanyakazi wake, huo muda wa kuwaza maendeleo ya shirika ataupata wapi?
 
Tungekuwa serious as a nation tungeweza jiandaa juu ya ili tuwe basi ata na satelites kwa ajili ya climate/weather maana uchumi wetu kwa kiasi kikubwa unategemea kilimo that employs more than 60% ya watu wetu.
Ila sishangai utaratibu wa zima moto ndio tumezoea sie.
Utashangaa mvua ikianza kila kitu kitakuwa abandoned mpaka ukame mwegine utokee watu hawako serious na kazi zao leading the nation into panic
 
Tanzania inabidi tuwaige wadada wa Iran
 
Back
Top Bottom