Ina maana ripoti zilizopita za CAG zilizokuwa zinawasilishwa ndani ya utawala Wa awamu ya 5 zilikuwa zinafanyiwa "editing"?

Ina maana ripoti zilizopita za CAG zilizokuwa zinawasilishwa ndani ya utawala Wa awamu ya 5 zilikuwa zinafanyiwa "editing"?

Mystery

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
15,843
Reaction score
31,057
Inasikitisha sana tena inahuzunisha kuona ripoti ya CAG ya safari hii baada ya mwendazake kuzikwa, ikiibua madudu mengi mno, tofauti na ripoti zilizokuwa zikiwakilishwa hapo nyuma wakati wa utawala huu wa awamu ya 5 ambazo zilikuwa zinampamba sana mwendazake na kueleza Taifa letu linapaa sana kiuchumi!

Ushahidi wa mazingira ya ninachokisema hapa ni kutokana na kauli aliyoitoa Rais Samia Suluhu Hassan, wakati akipokea ripoti hiyo akimwelekeza CAG kicheere kuwa hapaswi kuwa na kigugumizi chochote na anapaswa kueleza kila kitu kwa uwazi katika ripoti yake ili watanzania ambao ndiyo walipa kodi wa nchi hii, waelewe namna pesa yao inavyotumika.

Nasema kuwa ripoti za awali zilikuwa zinakuwa "edited" kwa kuwa katika ripoti za nyuma za CAG tulikuwa tukiambiwa kuwa ATCL imetengeneza faida ya Shilingi bilioni 28, wakati katika ripoti hii ya CAG inasema wazi kuwa katika miaka 5 ya nyuma mfululizo, ATCL imekuwa ikipata hasara na katika mwaka Wa fedha wa 2019/2020 ilipata hasara ya shilingi bilioni 60!

Vile vile tujikumbishe kile kilichompata CAG aliyepita, Profesa Mussa Assad baada ya kuibua ufisadi wa shilingi trillion 1.5 nini kilimpata baada ya kuibua ufisadi huo?

Kila mwananchi wa nchi hii ni shahidi namna CAG huyo alivyoundiwa "zengwe" na Spika Ndugai na Mwendazake, kwa kudhalilishwa sana hadi akatishiwa na Spika Ndugai kuwa akigoma kuja kuhojiwa na Kamati yake ya maadili, basi ataviagiza vyombo "vyake" vya dola vimlete pale bungeni akiwa amefungwa pingu mikononi!

Nini kilimpata CAG huyo kila mwananchi ni shahidi, namna CAG huyo alivyofurushwa kwa nguvu na kutimuliwa kazi!

Hivi kwa hii "trend" inayoendelea hapa nchini, ni mwananchi gani atakayeamini takwimu zilizokuwa zonatolewa chini ya utawala wa mwendazake, ambazo kwa maoni ya wananchi walio wengi zilikuwa ni za kughushi na zilizojaa uzushi na propaganda nyingi?
 
Mkuu ndani ya miaka mitano iliyopita hapakuwa na ripoti za CAG zaidi ya usanii uliopitiliza. Watu "walishikiwa bastola" kuwasilisha kile mkubwa alipenda kukisikia. Ona sasa wanavyofunguka; you can note something.
 
Usiamini ripoti ya CAG 100%. Kama Clouds Media Group wana uthibitisho wa malipo ya risiti na CAG alipewa, lakini bado report yake inaonyesha kuna ufujaji kwanini tumuamini?
 
Tumshukuru Mungu kwa muujiza kutuepusha na balaa life time, kasikia kilio cha Watanzania, nina imani Mama atajenga mifumo imara kwa katiba bora.
Kwanini alikuwa anasisitiza "Mtalimia meno" kwanini tulimie meno badala ya matrekta na zana bora za kisasa?
Mwendazake alikuwa na kusudi gani na maisha yetu?
 
Usiamini ripoti ya CAG 100%.Km Clouds Media Group wana uthibitisho wa walipo ya risiti na CAG alipewa,lakini bado report yake inaonyesha kuna ufujaji kwanini tumuamini?
Wewe na genge lako ndo hamuamini usitulishe matangopori. CAG ameongelea kutokuwepo kwa mkataba wa malipo na stakabadhi za kielektlonic. Unajua anamaanisha nini? Unamlipaje mtu mil.600+ bila maandishi zaidi ya stakabadhi za kuandika kwa mkono?
Kama hujaelewa niko tayari kukuelewesha zaidi.
 
Mkuu we acha tu
Hawa watu inaonekana wanakujaga na ripoti mbili
Moja ni ya kumfurahisha jiwe na nyingine ambayo ni original
... ile kauli ya Mama "msifiche kitu" wakati akipokea ripoti ya CAG ilikuwa na maana nzito sana. Akiwa part of the inner circle alijua michezo yote michafu iliyokuwa inachezwa enzi za hayati ila ndio hivyo she was second in command angefanya nini. Na jamaa alivyokuwa mshenzi hakuwahi hata kumkaimisha even for a second! Zaidi alikuwa anatuma kumwakilisha ili awe free zaidi kucheza na figures za taifa.

Mungu ni mwema; usipokaimishwa na mwanadamu; Mungu atakusimika.
 
Mkuu we acha tu
Hawa watu inaonekana wanakujaga na ripoti mbili
Moja ni ya kumfurahisha jiwe na nyingine ambayo ni original
Exactly.

Refer maneno ya Mama Samia alivyomuagiza CAG kuwa asipatwe na kigugumizi na aripoti kila kitu kwa uwazi ili kila mwananchi wa nchi aelewe namna pesa zao za walipa kodi "zinavyotafunwa"
 
Inasikitisha sana tena inahuzinisha kuona ripoti ya CAG ya safari hii baada ya mwendazake kuzikwa, ikiibua madudu mengi mno, tofauti na ripoti zilizokuwa zikiwakilishwa hapo nyuma wakati wa utawala huu wa awamu ya 5 ambazo zilikuwa zinampamba sana mwendazake na kueleza Taifa letu linapaa sana kiuchumi!

Ushahidi wa mazingira ya ninachokisema hapa ni kutokana na kauli aliyoitoa Rais Samia Suluhu Hassan, wakati akipokea ripoti hiyo akimwelekeza CAG kicheere kuwa hapaswi kuwa na kigugumizi chochote na anapaswa kueleza kila kitu kwa uwazi katika ripoti yake ili watanzania ambao ndiyo walipa kodi wa nchi hii, waelewe namna pesa yao inavyotumika.

Nasema kuwa ripoti za awali zilikuwa zinakuwa "edited" kwa kuwa katika ripoti za nyuma za CAG tulikuwa tukiambiwa kuwa ATCL imetengeneza faida ya Shilingi bilioni 28, wakati katika ripoti hii ya CAG inasema wazi kuwa katika miaka 5 ya nyuma mfululizo, ATCL imekuwa ikipata hasara na katika mwaka Wa fedha wa 2019/2020 ilipata hasara ya shilingi bilioni 60!

Vile vile tujikumbishe kile kilichompata CAG aliyepita, Musa Assad baada ya kuibua ufisadi wa shilingi trillion 1.5 nini kilimpata baada ya kuibua ufisadi huo?

Kila mwananchi wa nchi hii ni shahidi namna CAG huyo alivyoundiwa "zengwe" na Spika Ndugai na Mwendazake, kwa kudhalilishwa sana hadi akatishiwa na Spika Ndugai kuwa akigoma kuja kuhojiwa na Kamati yake ya maadili, basi ataviagiza vyombo "vyake" vya dola vimlete pale bungeni akiwa amefungwa pingu mikononi!

Nini kilimpata CAG huyo kila mwananchi ni shahidi, namna CAG huyo alivyofurushwa kwa nguvu na kutimuliwa kazi!

Hivi kwa hii "trend" inayoendelea hapa nchini, ni mwananchi gani atakayeamini takwimu zilizokuwa zonatolewa chini ya utawala wa mwendazake, ambazo kwa maoni ya wananchi walio wengi zilikuwa ni za kughushi na zilizojaa uzushi na propaganda nyingi?
Unauliza mavumbi stoo?
 
Inasikitisha sana tena inahuzinisha kuona ripoti ya CAG ya safari hii baada ya mwendazake kuzikwa, ikiibua madudu mengi mno, tofauti na ripoti zilizokuwa zikiwakilishwa hapo nyuma wakati wa utawala huu wa awamu ya 5 ambazo zilikuwa zinampamba sana mwendazake na kueleza Taifa letu linapaa sana kiuchumi!

Ushahidi wa mazingira ya ninachokisema hapa ni kutokana na kauli aliyoitoa Rais Samia Suluhu Hassan, wakati akipokea ripoti hiyo akimwelekeza CAG kicheere kuwa hapaswi kuwa na kigugumizi chochote na anapaswa kueleza kila kitu kwa uwazi katika ripoti yake ili watanzania ambao ndiyo walipa kodi wa nchi hii, waelewe namna pesa yao inavyotumika.

Nasema kuwa ripoti za awali zilikuwa zinakuwa "edited" kwa kuwa katika ripoti za nyuma za CAG tulikuwa tukiambiwa kuwa ATCL imetengeneza faida ya Shilingi bilioni 28, wakati katika ripoti hii ya CAG inasema wazi kuwa katika miaka 5 ya nyuma mfululizo, ATCL imekuwa ikipata hasara na katika mwaka Wa fedha wa 2019/2020 ilipata hasara ya shilingi bilioni 60!

Vile vile tujikumbishe kile kilichompata CAG aliyepita, Musa Assad baada ya kuibua ufisadi wa shilingi trillion 1.5 nini kilimpata baada ya kuibua ufisadi huo?

Kila mwananchi wa nchi hii ni shahidi namna CAG huyo alivyoundiwa "zengwe" na Spika Ndugai na Mwendazake, kwa kudhalilishwa sana hadi akatishiwa na Spika Ndugai kuwa akigoma kuja kuhojiwa na Kamati yake ya maadili, basi ataviagiza vyombo "vyake" vya dola vimlete pale bungeni akiwa amefungwa pingu mikononi!

Nini kilimpata CAG huyo kila mwananchi ni shahidi, namna CAG huyo alivyofurushwa kwa nguvu na kutimuliwa kazi!

Hivi kwa hii "trend" inayoendelea hapa nchini, ni mwananchi gani atakayeamini takwimu zilizokuwa zonatolewa chini ya utawala wa mwendazake, ambazo kwa maoni ya wananchi walio wengi zilikuwa ni za kughushi na zilizojaa uzushi na propaganda nyingi?
Bado tunaendelea na maombi yetu, Maulana atufanyie wepesi bungeni kama alivyotufanyia Ikulu...
 
"CCM PRODUCTIONS" hii ni studio mahsusi kwajili ya kufanya editing kumbuka kipindi kile Kwenye hotuba za kambi rasmi bungeni,kila mara walikataliwa baadhi ya page zisisomwe na sometimes zilinyofolewa ilimradi wananchi wasijue kitu..

huu UJINGA wa ku-edit report wameanza kitambo Sana pengine watanzania wengi ni wasahaulifu tu
 
Hao clouds wameweka hadharani huo uthibitisho? Unazani watakubali report inayowachafua?

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
Hebu jiongeze ndugu yangu,yaani taasisi km Clouds waseme kuwa wanarisiti wakati hawana? Unazani baada ya ripoti ya CAG mambo huishia hapohapo. Hivi tunavyoongea taasisi na mashirika yote yaliyoshutumiwa yatatakiwa kujieleza na kutoa uthibitisho/utetezi wao. Huko ndo wataonyesha hizo risiti.
 
Usiamini ripoti ya CAG 100%.Km Clouds Media Group wana uthibitisho wa walipo ya risiti na CAG alipewa,lakini bado report yake inaonyesha kuna ufujaji kwanini tumuamini?
Hizo risiti za clouds umeziona mkuu?

Clouds katka majibu na utetezi wao , wamesema vitu vingi, ila mwisho wa siku kwenye swala la risiti, wamekiri kutokuwepo kwa risiti za kielectroniki.
 
Hawa nzige tukiendelea kuwachekea, kuna siku wataifilisi nchi. Kila anayepewa nafasi, anawaza kupiga tu! Kisa yuko kwenye chama cha mafisadi nchini (ccm)!!
 
Back
Top Bottom