Ina maana ripoti zilizopita za CAG zilizokuwa zinawasilishwa ndani ya utawala Wa awamu ya 5 zilikuwa zinafanyiwa "editing"?

Ina maana ripoti zilizopita za CAG zilizokuwa zinawasilishwa ndani ya utawala Wa awamu ya 5 zilikuwa zinafanyiwa "editing"?

"CCM PRODUCTIONS" hii ni studio mahsusi kwajili ya kufanya editing kumbuka kipindi kile Kwenye hotuba za kambi rasmi bungeni,kila mara walikataliwa baadhi ya page zisisomwe na sometimes zilinyofolewa ilimradi wananchi wasijue kitu..

huu UJINGA wa ku-edit report wameanza kitambo Sana pengine watanzania wengi ni wasahaulifu tu
Exactly mjinga ni msahulifu, mwerevu sio msahulifu
 
Toa hoja utaeleweka mkuu sio kutukana. Hili ni jukwa la kutoa mawazo na kubishana/ kushindana kwa hoja.Kila mtu humu anaweza kutukana ila tunaheshimu utu na mawazo ya kila mtu.
Hakuna cha hoja hapa , huna njia ambadala ya kuhoji report ya CSG.
 
Upinzani ndio vichwa stahiki sana vya kuliongoza hili taifa... CCM wengi ni vilaza aiseee....
 
Magufuli ni fisadi papa aliekuwa anajificha kwenye mwavuli wa propaganda ili kuonekana ni mchapa kazi!
 
Mkuu ndani ya miaka mitano iliyopita hapakuwa na ripoti za CAG zaidi ya usanii uliopitiliza. Watu "walishikiwa bastola" kuwasilisha kile mkubwa alipenda kukisikia. Ona sasa wanavyofunguka; you can note something.
Fact !!!!
 
At least we breath!

FB_IMG_16499978077661400.jpg
 
Inasikitisha sana tena inahuzunisha kuona ripoti ya CAG ya safari hii baada ya mwendazake kuzikwa, ikiibua madudu mengi mno, tofauti na ripoti zilizokuwa zikiwakilishwa hapo nyuma wakati wa utawala huu wa awamu ya 5 ambazo zilikuwa zinampamba sana mwendazake na kueleza Taifa letu linapaa sana kiuchumi!

Ushahidi wa mazingira ya ninachokisema hapa ni kutokana na kauli aliyoitoa Rais Samia Suluhu Hassan, wakati akipokea ripoti hiyo akimwelekeza CAG kicheere kuwa hapaswi kuwa na kigugumizi chochote na anapaswa kueleza kila kitu kwa uwazi katika ripoti yake ili watanzania ambao ndiyo walipa kodi wa nchi hii, waelewe namna pesa yao inavyotumika.

Nasema kuwa ripoti za awali zilikuwa zinakuwa "edited" kwa kuwa katika ripoti za nyuma za CAG tulikuwa tukiambiwa kuwa ATCL imetengeneza faida ya Shilingi bilioni 28, wakati katika ripoti hii ya CAG inasema wazi kuwa katika miaka 5 ya nyuma mfululizo, ATCL imekuwa ikipata hasara na katika mwaka Wa fedha wa 2019/2020 ilipata hasara ya shilingi bilioni 60!

Vile vile tujikumbishe kile kilichompata CAG aliyepita, Profesa Mussa Assad baada ya kuibua ufisadi wa shilingi trillion 1.5 nini kilimpata baada ya kuibua ufisadi huo?

Kila mwananchi wa nchi hii ni shahidi namna CAG huyo alivyoundiwa "zengwe" na Spika Ndugai na Mwendazake, kwa kudhalilishwa sana hadi akatishiwa na Spika Ndugai kuwa akigoma kuja kuhojiwa na Kamati yake ya maadili, basi ataviagiza vyombo "vyake" vya dola vimlete pale bungeni akiwa amefungwa pingu mikononi!

Nini kilimpata CAG huyo kila mwananchi ni shahidi, namna CAG huyo alivyofurushwa kwa nguvu na kutimuliwa kazi!

Hivi kwa hii "trend" inayoendelea hapa nchini, ni mwananchi gani atakayeamini takwimu zilizokuwa zonatolewa chini ya utawala wa mwendazake, ambazo kwa maoni ya wananchi walio wengi zilikuwa ni za kughushi na zilizojaa uzushi na propaganda nyingi?
Utawala wa jiwe ulikuwa wa kifisadi haswaa
 
So na report ya sasa inafanyiwa editing kuficha uozo kwenye serikali ya mama na kuonesha uozo serikali ya mwendazake Kama ambavyo serikali ya mwendazake ilivoficha uozo wake na Kuonesha uozo wa mkuu Wa Msoga..ccm ni matapishi matupu
 
Sehemu nyeti za Chato zimeanikwa, kende zote nje, alizoea kutudanganya
 
Usiamini ripoti ya CAG 100%. Kama Clouds Media Group wana uthibitisho wa malipo ya risiti na CAG alipewa, lakini bado report yake inaonyesha kuna ufujaji kwanini tumuamini?
Hivi ukitoa receipt unabaki nayo au unampa aliyekupa pesa? Naamini CAG aliomba receipt kwa mkaguliwa wake ambaye si Clouds!
 
Back
Top Bottom