Inachofanya CCM ni kukomboa Majimbo yake yaliyokwenda Upinzani 2015 lakini Wapinzani bado wanamiliki majimbo yao kasoro lile la Ukerewe

Inachofanya CCM ni kukomboa Majimbo yake yaliyokwenda Upinzani 2015 lakini Wapinzani bado wanamiliki majimbo yao kasoro lile la Ukerewe

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Habari njema kwa upinzani ni kwamba Majimbo yote yaliyorudi CCM kupitia chaguzi ndogo awali yalikuwa chini ya CCM kabla hayajazolewa na mafuriko ya Laigwanan Edward Lowassa.

Kilichofanyika hadi sasa ni CCM kuyakomboa majimbo yake na kujipatia nyongeza ya jimbo la Ukerewe.

Kule Singida mashariki na Arumeru utaratibu wake ulikuwa wa kibunge zaidi na si kichama hivyo sitauhusisha hapa.

Majimbo ya upinzani ni Iringa mjini, Mbeya mjini, Arusha mjini, Kawe, Kibamba, Hai, Moshi mjini, Mbozi, Rombo na Karatu ambayo nadhani yapo salama hadi muda huu japokuwa pale Rombo na Kibamba lolote linaweza kutokea.

Niishie hapo.

Maendeleo hayana vyama!
 
Rombo uko sawa lakini sio Kibamba kamwe Mnyika mtamsika kwenye vyombo vya habari tu hamtampata kamwe.
 
Back
Top Bottom