DOKEZO Inachofanya TRA ni kuifilisi au kuiua Hospitali ya Massana, Watumishi wa Hospitali tunahisi kupoteza matumaini

DOKEZO Inachofanya TRA ni kuifilisi au kuiua Hospitali ya Massana, Watumishi wa Hospitali tunahisi kupoteza matumaini

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
A

Anonymous

Guest
Hospitali ya Massana ambayo ipo mitaa ya Mbezi Beach Jijini Dar es Salaam ipo mbioni kufilisika au kufa kabisa kutokana na zoezi la Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuchukua fedha kwenye Akaunti za Benki za Hospitali hiyo kwakile wanachodaiwa kuwa ni madeni wanayoidai Hospitali.

Kwasasa sisi Watumishi na Wafanyakazi wa Massana Hospitali hatujalipwa mishahara tangu Mwezi Mei 2024, hata miezi ya nyuma pia mishahara yetu ilikuwa ya kusuasua.

Mwanzoni mwa Mwaka huu (2024) viongozi wetu walitudokeza kuwa TRA imekuwa ikichukua fedha zote kwenye Akaunti za Hospitali hiyo kiasi kwamba ofisi yetu imeyumba.

Hali inatoendelea tayari uongozi wa Hospitali umetangaza hali ya tahadhari kwetu wote tunaotumikia ajira zetu katika taasisi hiyo ya afya.

Massana Hospitali inahudumia Wagonjwa lakini pia ina Chuo cha Afya na Wafanyakazi wote wa pande zote hatujapokea mishahara, mazingira ambayo yamesababisha huduma tunzotoa zianze kusuasua.

Niwe wazi kama ni kweli TRA wo ndio chanzo cha hiki tunachopitia, basi wao ndio chanzo cha Wafanyabiashara au watoa huduma wengi wetu kuwa na hali mbaya za kimaisha, tunakoselea TRA inaua taasisi yetu na inaelekea kutumaliza Watanzania zaidi ya 100 tunaotegemea Hospitali ya Massana kuendesha maisha yetu pamoja na wale ambao wanatutegemea.

Tunamuomba Waziri wa Afya huyu mpya aliyeingia madarakani kuja kuokoa ajira na maisha yetu kwani wengine tuna wategemezi wengi nyuma yetu, anguko la waajiriwa wa Massana ni anguko la mamia ya Watanzani wengine walio nyuma yetu.

Mbali na hapo sisi Watumishi wa afya tunahitaji kuwa na ukamilifu Kisaikolojia ili tutimize majukumu vizuri kwa kuwa tunahusika na afya za watu, kushughulikia fya ya mtu wakati wewe afya yako ya akili haipo sawa ni hatari.

Rais Samia Suluhu ujumbe huu ukufikie Watanzania wenzako tunateketea huku tunajiona, msaada wako unahitajika.
 
Hospitali ya Massana ambayo ipo mitaa ya Mbezi Beach Jijini Dar es Salaam ipo mbioni kufilisika au kufa kabisa kutokana na zoezi la Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuchukua fedha kwenye Akaunti za Benki za Hospitali hiyo kwakile wanachodaiwa kuwa ni madeni wanayoidai Hospitali.

Kwasasa sisi Watumishi na Wafanyakazi wa Massana Hospitali hatujalipwa mishahara tangu Mwezi Mei 2024, hata miezi ya nyuma pia mishahara yetu ilikuwa ya kusuasua.

Mwanzoni mwa Mwaka huu (2024) viongozi wetu walitudokeza kuwa TRA imekuwa ikichukua fedha zote kwenye Akaunti za Hospitali hiyo kiasi kwamba ofisi yetu imeyumba.

Hali inatoendelea tayari uongozi wa Hospitali umetangaza hali ya tahadhari kwetu wote tunaotumikia ajira zetu katika taasisi hiyo ya afya.

Massana Hospitali inahudumia Wagonjwa lakini pia ina Chuo cha Afya na Wafanyakazi wote wa pande zote hatujapokea mishahara, mazingira ambayo yamesababisha huduma tunzotoa zianze kusuasua.

Niwe wazi kama ni kweli TRA wo ndio chanzo cha hiki tunachopitia, basi wao ndio chanzo cha Wafanyabiashara au watoa huduma wengi wetu kuwa na hali mbaya za kimaisha, tunakoselea TRA inaua taasisi yetu na inaelekea kutumaliza Watanzania zaidi ya 100 tunaotegemea Hospitali ya Massana kuendesha maisha yetu pamoja na wale ambao wanatutegemea.

Tunamuomba Waziri wa Afya huyu mpya aliyeingia madarakani kuja kuokoa ajira na maisha yetu kwani wengine tuna wategemezi wengi nyuma yetu, anguko la waajiriwa wa Massana ni anguko la mamia ya Watanzani wengine walio nyuma yetu.

Mbali na hapo sisi Watumishi wa afya tunahitaji kuwa na ukamilifu Kisaikolojia ili tutimize majukumu vizuri kwa kuwa tunahusika na afya za watu, kushughulikia fya ya mtu wakati wewe afya yako ya akili haipo sawa ni hatari.

Rais Samia Suluhu ujumbe huu ukufikie Watanzania wenzako tunateketea huku tunajiona, msaada wako unahitajika.
Sasa mtu asogee hapo hospital ajifanye ana mafua na uchovu wa mwili uone watakavyomuwashia moto
 
Screenshot_20240817-232202.png
 
Kama ndivyo basi Masana Hospital wafanye kila kilicho ndani ya uwezo wao ili yasije yakawafika kama yale yaliyomkuta marehemu Dr. Ferdinand Masau na hospitali yake ya Tanzania Heart Institute (THI) ambapo serikali kupitia NSSF walihakikisha wanaiangusha kabisa ile hospitali yake.
 
TRA hasa ya Samia haijawahi kumwonea mtu.
Hapo kuna mchezo mchafu wa utakatishaji pesa au ukwepaji wa kodi ulikubuhu.
Yes, wafanyakazi mnateseka ila uongozi unajua jinsi ulivyoyakanyaga
 
TRA hasa ya Samia haijawahi kumwonea mtu.
Hapo kuna mchezo mchafu wa utakatishaji pesa au ukwepaji wa kodi ulikubuhu.
Yes, wafanyakazi mnateseka ila uongozi unajua jinsi ulivyoyakanyaga
Punguza ujuaji bwana mdogo muda mwingine ni bora kuacha yakupite kuliko kuonekana mjinga kiasi hiki

Yaan wewe ulienje ya Taasisi unajua kuliko walio ndani ya taasisi,

Kweli wewe ni Kiboko,
 
Punguza ujuaji bwana mdogo muda mwingine ni bora kuacha yakupite kuliko kuonekana mjinga kiasi hiki

Yaan wewe ulienje ya Taasisi unajua kuliko walio ndani ya taasisi,

Kweli wewe ni Kiboko,
Mtoa mada kazungumzia upande mmoja tu kwasababu mbili.
Hajui yaliyo uvunguni mwa taasisi yake au anajua sababu ya TRA kufanya hivyo lakini kashindwa kusema ukweli.
Siwezi kuamini TRA kwamba wanaweza kuifanyia mchezo mchafu Hospitali kongwe kama ile
 
Back
Top Bottom