Inahitaji ujasiri kumiliki PASSO

Inahitaji ujasiri kumiliki PASSO

Tahadhari ndugu mtanzania, nunua gari kulingana na mahitaji yako. Usiangalie nani anafanya nn na kwa sababu gani.
Gari kwa dunia ya kesho nchi hii itakuwa ni hitaji muhimu, achana na maswala ya muonekano, kuwa practical.
Usijiingize kwenye mashindano ya nani anaendesha nn. Lengo LA Gari ni kufacilitate mobility, kama unaweza kufikisha kwa pesa kidogo Fanya hivyo. Hiyo ndio akili.
Passo ni gari safi tu. Endesheni kwa kujiamini.
BTW its your car, Why sweat over what the other guy is saying. Enjoy your ride. Hata kama ni Bajaj q..what!?
hueleweki Mkuu
hivi inatokea safari ya ghafla kweli kwenda nyumbani utawasha kiPasso na upakie wanao (panda Bus)
unataka kwenda kuchukua pumba za kuku nk kwa ajili ya mifugo utachukua Harrier chukua PASSO
PASSO na Bajaj ni gari za matumizi ya sokoni, Pick up shamba
usiwadanganye wenzako Mabasi yamejaa wayatumie wenzetu huko Nje wanatumia Tram, Train Ndege nk hawachukui vigari vinavyopeperushwa na malori
 
hueleweki Mkuu
hivi inatokea safari ya ghafla kweli kwenda nyumbani utawasha kiPasso na upakie wanao (panda Bus)
unataka kwenda kuchukua pumba za kuku nk kwa ajili ya mifugo utachukua Harrier chukua PASSO
PASSO na Bajaj ni gari za matumizi ya sokoni, Pick up shamba
usiwadanganye wenzako Mabasi yamejaa wayatumie wenzetu huko Nje wanatumia Tram, Train Ndege nk hawachukui vigari vinavyopeperushwa na malori
Mkuu nakubaliana na wewe. Kila kitu. Japo lazima ujiulize kwa watu Wa mjini kama wewe wangapi wanafuga kuku, wanataka kusafiri mpk kijiji wajiendeshe au wanataka kupakia pumba!?
Huko huko unakokuita kwa wenzetu, Mabasi yanafanya kazi vizuri tu kati ya miji na miji, na best selling cars, huko huko ni jamii ya hizi hizi passo/yaris/ist/vw golf.
Tatizo tukisha tazama TV, tu tunaanza kuasume tunachoona kwenye kioo ndio uhalisia.

Watanzania (wengi) wapo kwenye hatua ya kwanza ya kumiliki magari. Wengi huenda ni kizazi cha kwanza kumiliki magari.. Kama ilivyokuwa kwa wenzetu umma ulianzia kwenye magari raisi kuendesha na kuhudumia. Ref. People's car.. Vw Beatle..

Sasa hao miaka 50/baadae kama umma wanaelewa umuhimu Wa gari na marumizi sahihi na matunzo stahili. Sisitunataka kuruka stage. Watu waendeshe passo mpk tutakapojua magari ni nini.
 
Kuna mtu nilimsika akisema passo ikizima unashtua na powerbank sijui ni kweli?..
 
Passo iondolewe barabaran
Passo haina shida...shida ipo kwa wamiliki.....wewe umeshajua gari ni ndogo mathalani ile ya piston 3.....unailazimisha kupanda kitonga ikiwa speed 100....kwa nini isizingue..?
Unaitoa Dar to Mwanza kesho yake Mwanza to Arusha, then Arusha to Dar mfululizo na hapo unafanya ligi na mabasi kwa nini isizingue..?


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Namiliki passo mkuu, ni gari ninayoipenda pengine kuliko gari yoyote ndogo, kwanza haili mafuta, pili inatembea , tatu ni kubwa sana ndani, nne kwenye roughroads ipo confotable sana ukilinganisha na gari zingine ndogo km swift, terious nk. Pia ipo stable sana barabarani.nasema hivo sababu nlitembea nayo toka dar hadi mwanza non stop na nlitembea toka saa moja asubuhi hadi saa sita. Uniambie yako ilochemshaje labda kimeo mkuu
Mpaka kufikia hatua ya kumiliki gari aina ya PASSO inapaswa ujitoe ufahamu mbele ya kadamnasi. Gari gani isiyoweza kutembea 200 kms bila kuchemsha?

Nasubiria tamko/katazo la hizi gari toka ngazi za juu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mi natumia mafuta ya 80000 mwezi mzima. Huwa mafuta ya 50000 natembea km 350, mungu anipe nini
Huu ni mtazamo mkuu! na inawezekana ulipata gari ikiwa tayali inamatatizo. Mimi nina Passo kwasasa mbali na nyingine ninazotumia, na nimekuwa nikienda karibu mara mbili kila mwezi Mwanza - Dodoma bila kuhisi hiyo shida ya kuchemsha.

Unaweza kuangalia yafuatayo:
1. Hakikisha rejeta yako imefanyiwa ukaguzi/kusafishwa na mtu ambaye ni mtaalam.
2. Jaribu kuachana na kuweka maji ya Duwasa/Dawasco au kisima kwenye rejeta - jitahidi kutumia coolant. Napendekeza utumie coolant bora sio zile zinazouzwa gerezani. Pata kutoka BP au kampuni nyingine zinazojitambua.

3. Fanya wholesome wngine check - ipimwe system yote. Garage za veta au kwengineko wanaweza kupima gari gako na kukushauri vipuri ambavyo tayali vimechakaa na unahitaji kubadilisha.

Naamini ukifanya haya mkuu wangu, tatizo linaweza kupungua.

TATIZO LA PASSO:
Gari nyingi aina ya Passo zona shida ya usukani kuwa mgumu - kuna indicator moja inajitokeza unapowasha gari "EPS" - ikitokea hiyo unaweza kushawishika kutupa gari kwani hata baadhi ya mafindi wa toyota hasa mikoani hawajui namna ya kurekebisha.

Zaidi ya shida hii sijaona. Kinachonifurahisha zaidi ni kuwa natumia 120,000/- mwezi mzima tofauti na gari zangu nyingine nilipokuwa natumia zaidi ya 250,000/- kwa mwezi (hii nazungumzia Mwanza).

Jitahidi matunzo kwa gari yoyote - utaipenda

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wengine washenzi tu, wansjifanya wznaxo wakati pumbv t
Acheni upuuzi wenu hii ni gari amabayo naamini Watanzania wengi kutokana na hali zao ni ngumu sana kuimiliki.

Bei ya sasa ya Passo ni kuanzia milioni 7 mpaka 10. Hebu niambie ni Watanzania wangapi wanaweza kununua hii gari?.
Tusijifanye sisi ni Wajapan
Hivi Tanzania imewahi kutengeneza hata pikipiki?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
The safest speed na paso ni 100km/h ikizidi sana mwisho 120km/h nina experience kubwa sana na paso kwani ni gari yangu ya 3 kumiliko nikitokea kwenye oppa 1700cc, nimeipenda sana passo pengine nafikiria kununua tena

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom