Inakuwaje mashujaa hawa walioinusuru TANU hawajaadhimishwa hadi leo?

Inakuwaje mashujaa hawa walioinusuru TANU hawajaadhimishwa hadi leo?

Kitabu hiki nakipataje make ukienda bookshops vitabu vya hivi havipatikani!! Naomba kujua nakipataje hadi kunifikia nilipo bukoba, means naomba kujua gharama zote
WilboardG,
Kitabu cha Abdul Sykes Kiswahili na Kiingereza vinapatikana
Ibn Hazm Media Centre, Msikiti wa Mtoro na Manyema na pia
Tanzania Publishing House (TPH) Dar es Salaam.

Ibn Hazm wanakiuza kwa shs: 10,000.00.
TPH wanakiuza kwa shs: 15,000.00
 
Samahani ndugu, mbona vitabu vya hivi hatuwezagi kuvikuta bookshops zaidi ya kukuta vya nyambari?? Nielekeze pa kukipata ikibidi niambiwe na gharama za kukifikisha Bukoba make ndo nyumbani
84fb6016df29ca5c9dcd483f129d4bb4.jpg
kitabu kinapatikana ilala Amana karibu BOA BANK
afa3fa1497ea8272f2fc821e206e2f25.jpg
 
Mohamed Said,
Mimi sipo dar labda ningepewa utaratibu wa namna ya kukipata huku mikoani
 
WilbroadG,
Bahati mbaya mimi ni mwandishi maduka ya vitabu ndiyo wanaouza ikiwa watapenda.
 
Waislamu kwenye siasa wanaleta dini, kwenye elimu dini, kila kitu udini. Siku gani mtaweka dini pembeni mjadili mambo bila kuwaingiza wazee wenu waislamu ambao hawakuleta uhuru zaidi ya kumsomea mkoloni albadir? Usomi wa Nyerere ndiyo ulitupatia uhuru na hiyo ni fact! Waislamu wa Tanganyika at the time walikuwa hawana shule zaidi ya elimu ya madras.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
PATWA%2B-%2BCopy.jpg

Mwalimu JK Nyerere na Bw. Patwas kualia kwake unapoitazama picha. Kulia mwenye koti na kofia Mzee Rashid Makoko Babu na wa pili yake ni mwanae Mamboleo Makoko na kushoto mwenye koti na kofia mzee Makata Mwinyimtwana.
Tarehe 23 Oktoba,1955 wanachama wa mwanzo wa TANU huko Tanga walikutana kuchagua uongozi wao chama. Hamisi Heri alichaguliwa kuwa mwenyekiti na Peter Mhando katibu. Jumla ya watu arobaini na tano walihudhuria mkutano huo na wakapewa kadi za TANU. Mwalimu Kihere alihudhuria mkutano ule lakini hakuchaguliwa katika nafasi yoyote ya uongozi. Kamati ya wanachama iliundwa kutokana na wale wanachama kumi na moja waasisi waliokutana katika ule mkutano wa kwanza mwezi uliopita. Kamati hiyo ilikuwa na wajumbe wafuatao: Abdallah Rashid Sembe, Mohamed Kajembe, Victor Mkello, Dhili Mgunya, Ali Mohamed, Abdallah Mohamed na Mohamed Sadik. Peter Mhando alijitolea nyumba yake kuwa ofisi ya kwanza ya tawi la TANU mjini Tanga. Mara tu baada ya mkutano huu wazee wa Tanga wakiongozwa na Makoko Rashid, mwanachama wa zamani wa TAA walianza kufanya kampeni kwa ajili ya TANU. Chama kilipata msukumo mwingine na kuongezeka nguvu wakati Sadik Ali Patwa Muasia tajiri alipoingia TANU.

20431205_2305043049522045_5715176440330895933_n.jpg


Patwa alikuwa Muislam wa madhehebu ya Shia. Patwa alikuwa amehamia Tanganyika kutoka Zanzibar mwaka 1918 baada ya kumalizika kwa Vita Kuu ya Kwanza. Pale Tanga Patwa alianzisha kiwanda cha soda na akatajirika. Wakati huo wa zama za ukoloni wakati Waasia wenzake walikuwa wakiwabagua Waafrika, Patwa alikuwa akikaa na Waafrika wa rika lake akinywa nao kahawa. Halikadhalika watoto wake wakawa wanacheza kandanda na vijana wenzao wa Kiafrika katika vilabu vya Tanga. Hili lilikuwa jambo geni na lisilokuwa la kawaida kutoka kwa familia ya Kiasia wakati wa ukoloni. Patwa alisaidia harakati za kudai uhuru kwa hali na mali, na akaifanyia kampeni TANU miongoni mwa jamii yake mwenyewe ya Kiasia. Wakati wa harakati Nyerere alikuwa akifanyiana maskhara na Patwa akimwambia, ‘’Mzee Patwa baada ya kupata uhuru nadhani tukuteuwe uwe balozi wetu India.’’ Lakini Patwa hakuiona Tanganyika huru, alifariki kabla ya uhuru kupatikana.

Baada ya kufungua tawi la TANU mjini Tanga, uongozi wa chama ulimwalika Julius Nyerere, Bibi Titi Mohamed, John Rupia na Mbutta Milando kufanya ziara Tanga. Nyerere alifikia nyumbani kwa Hamisi Heri. Ujumbe huu kutoka makao makuu ya TANU ulipata makaribisho makubwa yaliyoandaliwa na vyama vya lelemama ambavyo kwa kawaida vilikuwa vingi sana katika pwani ya Afrika ya Mashariki kutoka Mombasa nchini Kenya hadi Mikindani, Tanganyika. Kiongozi wa akina mama hawa mjini Tanga aliyesaidia kuieneza TANU alikuwa Bibi Mwanamwema bint Sultan, ndugu wa mbali wa mwenyekiti wa TANU Tanga, Hamisi Heri.

Matokeo ya ziara ya Nyerere Tanga ilikuwa ni kumrudisha Mwalimu Kihere katika siasa. Baada ya kushindwa kupata nafasi yoyote katika chama, Mwalimu Kihere alipoteza shauku ya siasa. Nyerere alipokuja Tanga kuifanyia kampeni TANU ndipo Mwalimu Kihere alikaribishwa kujiunga na chama. Mwalimu Kihere alifahamiana na Nyerere mwaka 1946 walipokutana Dar es Salaam katika mkutano wa mwaka wa African Association. Nyerere alipozuru Tanga Mwalimu Kihere alitaka kufanya dhifa nyumbani kwake kwa heshima yake. Uongozi wa TANU, hususan Hamisi Heri na Mzee Makoko walikataa kumruhusu Nyerere kuhudhuria dhifa hiyo kwa sababu Mwalimu Kihere alikuwa hajaonesha kuiunga mkono TANU. Nyerere akitambua utu uzima wa Mwalimu Kihere, uzoefu na sifa yake ya uongozi katika African Association, alishauri uongozi wa TANU Tanga usiache fursa ile ipite bure. Nyerere alitoa hoja kuwa, ilikuwa muhimu kukubali mwaliko wa Mwalimu Kihere na kutumia fursa hiyo kumuomba arudi kwenye harakati kwa kuwa TANU ingefaidika kutokana na uzoefu wake alioupata katika African Association. Kwa ajili ya nasaa hiyo TANU ilikubali mwaliko wa Mwalimu Kihere na Nyerere alihudhuria dhifa ile nyumbani kwa Mwalimu Kihere pamoja na wanachama wengine.

20479660_2305040996188917_2590609322615442244_n.jpg

Mwalimu Kihere

Mwalimu Kihere alikuwa mwanasiasa wa msimamo wa wastani, alikuwa mbali na msimamo mkali dhidi ya serikali. Kwa ajili hii Mwalimu Kihere alielewana vizuri na utawala wa kikoloni. Hii ilikuwa kinyume kabisa na wazalendo wengine kama Mzee Makoko Rashid ambaye kwa miaka mingi alijulikana kwa chuki yake dhidi ya Waingereza. Inasadikiwa kwamba watu wawili wataingia katika historia kwa chuki zao mahsusi dhidi ya Waingereza, mtu wa kwanza ni Abdillah Schneider Plantan na wa pili ni Mzee Makoko Rashid. Wote wawili walifungwa gerezani kwa sababu ya msimamo wao dhidi ya serikali ya kikoloni. PC na DC wake wote wawili walikukubali mwaliko wa Mwalimu Kihere. Mwalimu Kihere alimtambulisha Nyerere kwa wageni mashuhuri na alimuomba azungumze maneno machache. Nyerere kwa kipaji chake cha ufasaha wa kuzungumza alitoa hotuba kuhusu lengo la TANU na kanuni za kidemokrasia kama zilivyoelezwa na Umoja wa Mataifa. P.C. alisimama baada ya Nyerere kuzungumza na akatoa hotuba kwa niaba ya serikali. P.C. alimsifu Nyerere kuwa ni mwanasiasa mzuri kinyume na vile alivyosikia kabla ya kukutana naye. Hapo hapo alitoa ruhusa kwa Nyerere na TANU kufanya mikutano ya hadhara katika wilaya zote za jimbo hilo. Lakini uhusiano huu haukudumu, serkali iliyapiga marufuku matawi kadhaa ya TANU Tanga mara tu baada ya kuundwa kwa UTP.

Siku iliyofuata mabingwa wa hotuba wa TANU, Julius Nyerere na Bibi Titi Mohamed walihutubia mkutano wa hadhara kwenye uwanja wa Tangamano. Hii ilikuwa hatua kubwa sana kwa TANU, na kwa harakati dhidi ya ukoloni pale Tanga. Ilikuwa muda mrefu umepita tangu zile siku za zile siasa za wasomi katika Discussion Group, kikundi cha majadiliano; na ile mizozo baina yao na ule uongozi Waarabu katika TAA. Baada ya hapo, Mwalimu Kihere alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa TANU Tanga badala ya Hamisi Heri na Amos Kissenge alichaguliwa katibu. Abdallah Rashid Sembe mmoja wa wanachama waasisi wa mwanzo kabisa wa TANU alichaguliwa kuwa mjumbe wa Kamati Kuu ya Taifa ya TANU akiwakilisha Jimbo la Tanga.

Ilikuwa chini ya hali ya hewa ya kisiasa kama hii ndipo TANU iliingia kwenye uchaguzi wake wa kwanza katika Tanganyika, chaguzi wa Kura tatu wa mwaka wa 1958 Tanga ambako United Tanganyika Party (UTP) ilikuwa imara, TANU iliwachagua John Keto, B. Krishna na R. N. Donaldson kama wagombea wake. John Keto akiwa miongoni mwa walimu wa St. Mary’s School, Minaki na alikuwa amefanya kazi kubwa katika siku za mwanzo kufungua matawi ya TANU huko Kisarawe. TANU iliamua kumteua Keto kusimama Tanga ambako ndiyo kulikuwa kwao. Katika uchaguzi huu serikali iliacha uandikishaji wa wapiga kura kwa vyama vyenyewe. Mzee Makoko Rashid, mwanasiasa wa makamo mwenye msimamo thabiti wa chama na kijana Mmaka Omari walikuwa maofisa waandikishaji wa wapiga kura katika wa TANU mjini Tanga. Makoko na Mmaka walikamatwa na kushitakiwa kwa kosa la kuwaandikisha watu ambao hawakutimiza masharti yaliyoelezwa na ilani ya uchaguzi. Katika ghera yao kwa TANU kushinda ule uchaguzi muhimu, Mzee Makoko alimsajili Mwafrika yoyote aliyetaka kuipigia kura TANU bila kujali sifa zake. Bhoke Munanka alikamatwa vilevile kule Mwanza kwa kosa hilo hilo. Hakukuwa na ushahidi wa kutosha dhidi ya Mmaka Omari kwa hiyo aliachiwa huru mara tu baada ya kukamatwa kwake. Mzee Makoko Rashid alipatikana na hatia na alihukumiwa kufungwa jela. Adhabu ya kifungo ilidhoofisha sana afya yake na mara baada ya kufunguliwa kutoka gereza baya sana la Maweni Mzee Makoko alifariki.

Iweje leo hawa mashujaa hakuna kumbukumbu zao Tanga ukitoa Makoko Road. Hivi ule Mtaa wa Maua pale katika ya mji una akisi kitu gani? Dessa una sauti CCM wakumbushe na wazindue kuhusu historia hii kama hawaijui mimi nitakuja kwa nauli yangu kuja kutoa mhadhara In Shaa Allah.

Mkutano wa Tabora ulitishia kuigawa TANU katika makundi hasimu yaliyokuwa yakivutana, kama isingekuwa kwa ule mkakati uliopangwa kule Mnyanjani, kijiji kidogo nje ya mji wa Tanga. Waliopanga mkakati huo - Nyerere mwenyewe, Amos Kisenge, Hamisi Heri, mwenyekiti wa TANU Tanga, Mwalim Kihere mwanasiasa mkongwe wa African Association, Sheikh Abdallah Rashid Sembe, Ng’anzi Mohamed, Mustafa Shauri na Abdallah Makata - Hawa ndiyo waliinusuru TANU isinase katika mtego uliotegwa na wakoloni ambao ungeifanya TANU igawike katika mapande mawili na kila moja dhaifu kuweza peke yake kuikabili serikali ya kikoloni.





Shujaa Julius Nyerere tu! Wengine wenye vibandiko wasoma albadir tu!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Historia iliyofichwa
Historia inaandikwa au haiandikwi? Kama hao mashijaa wenu wangekuwa na elimu ya maana, na siyo ya madras basi wangeandika. Hakuna aliyeficha historia, nyinyi waislamu ni wachochezi sana. Kwani hiyo historia yenu Ilifichwa wapi na Nyerere?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
WilboardG,
Kitabu cha Abdul Sykes Kiswahili na Kiingereza vinapatikana
Ibn Hazm Media Centre, Msikiti wa Mtoro na Manyema na pia
Tanzania Publishing House (TPH) Dar es Salaam.

Ibn Hazm wanakiuza kwa shs: 10,000.00.
TPH wanakiuza kwa shs: 15,000.00
Vitabu vya chokochoko tu hivyo! Unamjua Abdul Sykes wewe?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Shujaa Julius Nyerere tu! Wengine wenye vibandiko wasoma albadir tu!

Sent using Jamii Forums mobile app
Mberoya,
Mbona ndugu yangu umeghadhibika kiasi hicho na hapa tuko katika
mjadala tu hatugombani?

Umesema kweli na umempa Baba wa Taifa haki na heshima stahiki
yake.

Lakini peke yake bila ya kupokelewa na wenye mji Baba wa Taifa
angeshindwa.

Unakijua kisa cha Rashid Ali Meli?

Unakijua kisa cha Idd Faiz Mafungo?
Unamjua Sheikh Mohamed Ramiyya?

8lS-bGcfJLi-US4KM0clKL332ZwGi0MysIEH5ffaAkw=w680-h510-no

Wa Kwanza Kushoto ni Idd Faiz Mafongo Mwekahazina wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika wa Mwekahazina wa TANU. Wanaofuatia ni: Sheikh Mohamed Ramiya wa Bagamoyo, Julius Nyerere, Saadan Abdu Kandoro na Haruna Taratibu. Picha Hii ilipigwa Dodoma Railway Station Mwaka 1956 Wakati wa Kueneza TANU Katika Majimbo.

Unamjua Bi. Shariffa Bint Mzee?
Kukutajia majina machache.

Unajua historia za wazalendo hawa katika kupigania uhuru wa
Tanganyika?

Unajua hata historia ya Baba wa Taifa haiwezi kukamilika wala
kunoga bila ya kutaja michango ya wazalendo hawa?

Je unalijua Baraza la Wazee wa TANU chini ya Mwenyekiti Sheikh
Suleiman Takadir
(1954 - 1958) kisha Idd Tulio (1958 - 1963)?

Baraza lenyewe ndilo hilo hao chini:

zsZAAe_iGQIsvcGpBPzur4047KO_y37fJNHBWY6-SF0z6iMzwTsF_U97Pc80TwJ2epILeXCkbImXcZ11w_LIsSpTrQr3Qv9_K3P-XM2hdKVi-roOi2FJeM2JnRkb0WLlYWmpv1S4V9qbct-TnZjQASrizWkwJBYkGHJre0sY9KlZ8mzBYBCZHRFLRN_H7z2soAfd13SAZEDNzg4C0K1sikBlG1O-tjxe6NEv4YDc0Tx4cGTGyZVfMx-Kqs_jevvZ9ypC7UGKi0P0qta7HftPftFwuqrAmOO0lEivflm9gvc7jvkoRXz6hLbryFsZhSV4RTtwgdq4VFKV5PslvxjJ4UiVaX8WEkuv4Hs5VUAUxxaRbcNekoefYdxt6DoatGSuPQRBNq4EGBGMaeneZtInWTkwWJyvFcN9Mztkl65xl2kyaZ2-NPTgizMTJVht0bjGLtovz4r88wbQSTW3_yBs_NgEBEBZAMXT7YCgKuBzf4o4uyTMkliEBbEvFiZTily-5z9I4ynZx_EMYOe_0TYGbEmOlEv36kldJ9im2D3cXl6tCyrG5Ly8bzPDi5ftguojevzfEWwENsF3hul-82ikTkfGUwFnzg20dBNxieX2VA=w839-h629-no


Mohamed Said: Idd Faiz Mafongo Mweka Hazina wa Safari ya Nyerere UNO 1955
Mohamed Said: KUTOKA JF: ALI MWINYI TAMBWE, RASHID ALI MELI NA IDD FAIZ MAFUNGO - SAFARI YA NYERERE UNO 1955
 
Back
Top Bottom