Rejea kwenye utangulizi wa mada yako pale umeshangazwa na mwanaume kusikiliza muziki wa taarabu!
Hili la mipasho labda liwe kwenye mengineyo!
Mambo ya mipasho sasa hayo inategemea na mapokeo.
Miziki ya zamani ya kina mzee Issa Matona , Shakira n.k wala haikuwaga sana na hayo mambo ya mipasho n.k!
Binafsi mfano namkubali sana Bi Sabaha Salum Muchacho kwa kuwa anakuwa na utulivu flani ktk kuimba ,
Kimsingi huyu madam ndiye aliyepaswa kuwa malkia wa nyimbo za taarabu nchini kuliko hiyo anaetajwa kwa muda mrefu!
Kopa nyimbo zake zina makelele na mipasho mipasho tuuu binafsi sijui hata kwa vipi anajiita malkia!
Sent using
Jamii Forums mobile app