Inaniitaji mwaka mzima kupata mtaji wa 1.5M haya maisha mbona yanakinaisha hivi

October man

JF-Expert Member
Joined
Nov 23, 2017
Posts
3,635
Reaction score
5,012
Nina mpango wa kuanza kufanya biashara na mtaji minimum 1.5M ila kwasasa sina asije kukuongopea mtu eti mtaji sio lazima pesa uwongo, yaani nimekaa nimepiga mahesabu jinsi yakupata icho kihasi itanichukua mwaka mzima wa kufanya kazi na maumivu ya ku-save pesa kila mwezi kihasi cha 100,000/=.

Aya maisha yanakinaisha sana muda mwengine, yana kinaisha sana.
 
Dah....naona umepanik maan....tafuta pesa...acha kulialia 😎
*kihasi = negativity
Aya = aya | Ufafanuzi katika Kiswahili - Oxford Living Dictionaries
 
Mkuu, kama unaamini wazo lako jaribu kutafuta mtaji kwa ndugu, jamaa na marafiki.
Kwakuwa una kazi, utakuwa unalipa kupitia kazi na hiyo biashara utakayoanziasha.

Faida yake ni kwamba itakusaidia kuanza mapema wazo lako kabla halijapitwa na wakati.

Pia kama utafanikiwa kukopa kwa watu hao utaepuka kulipa riba kwenye biashara ambayo hujajua performance yake.
Ni hayo tuu mkuu.
 
Kupewa na ndugu haa[emoji134][emoji134] bilashaka wewe unatoka familia za kina MO, Bakhresa yaani mtaji akupe ndugu ndio maana kumbe zile kauri za mujiajiri munatoaga kirahisirahisi.

Mkuu usione nakusema sana kwa kuandika statement hiyo tu “Omba mtaji kwa ndugu” imetosha kujua kwamba ujui maisha ya Tanzania yapoje hasa hakuna atayejitaabisha miaka kutafuta mtaji ikiwa anauwezo wa kupata kwa ndugu mzee waangalie mtu kama Naja naja wangepata neema hiyo usingewaona kabisa JF na mtaji usingekuwa tatizo kamwe.

“Mtaji upewe na ndugu haaaa serious that life, that family, that tribe.

Kuna jamaa amepiga vibarua vya kuosha magari miaka miwili Just kupata mtaji wa 2M.

Kuna jamaa amepiga kazi kama mfanya usafi wa Guest House miaka mitano Just kupata mtaji wa kufanya kilimo.

Kuna wanachuo wanabana Boom miaka mitatu just kupata hata 2M.

LIFE NOT EASY BOSS labda KWAKO.
 
Na ukishamaliza kusave hivyo vilaki laki vyako utakuta biashara uliyopanga kuifanya imekuwa yeboyebo
Sina biashara nilitageti nikikusanya nitaamua yakufanya Idea is nothing too.
 
October man,


Usemayo ni kwel ndugu kukupa mtaji ni ishu maisha haya!
Lakini ukitia nia kbs kbs...ukaamua kunifunga kibwebwe mie naamini utapata!..anza biashara za mtaji mdogo kbs(toa aibu hapa)!uza miwa...nk!

Au hyo ishu unayosema ya carwash ww fanya ukiwa na lengo lako kichwani!
Usidhan kila mtu aliyefika juu alipewa mtaji .hapana!..all the best
 
October man,
Fanya ufanyavyo upate mtaji mapema mkuu. Siyo lazima kwa ndugu ila kama kuna namna unaweza kuumiza akili kupata mtaji mapema kabla wazo lako halija-expire utakuwa umejitendea haki na utakuwa umepiga hatua kubwa.

Ukishatambua jukumu la kufanikiwa au kufeli liko juu yako na kujitoa kulibeba mambo yataenda maana utatumia kila njia halali kufanikisha.

Kila la kheri
 
Uhalisia ni mgumu sana(mchungu kumeza). Biashara inayosave siyo ya laki moja.
Mambo mengine hayaelezeki, hizi business skills kwenye mitaji ya laki tunadanganyana tu.
 
Uhalisia ni mgumu sana(mchungu kumeza). Biashara inayosave siyo ya laki moja.
Mambo mengine hayaelezeki, hizi business skills kwenye mitaji ya laki tunadanganyana tu.
Sijaelewa hapa mkuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…