demigod
JF-Expert Member
- Jan 2, 2015
- 8,292
- 15,250
Kuna kipindi huwa nacheka tu. Pale nionapo Usajili wa kukurupuka unaofanywa na Klabu ya Simba.
Najiuliza ni nini huwa wanafikiria hasa pale wafanyapo usajili wa wachezaji wapya.
Tatizo kubwa sana ambalo wamekuwa nalo tangu Tambwe awanyooshee mkono wa kwa heri, ni nafasi ya Ushambulizi.
Ila cha ajabu zaidi ni pale wanapopata mshambuliaji mwenye ubora wa wastani na kushindwa kukaa naye kwa kipindi kirefu.
Mimi binafsi sikuona Tija ya kumuondoa Blagnon. Basi tukadhani kuwa kunafanyika usajili wa Upgrade. Yaani kuleta kilicho bora zaidi. Nilishtuka na kupigwa na butwaa baada ya kusikia Juma Luizio kutoka Zesco ndio anakuja kuchukua nafasi ya Blagnon. Kwa lugha nyingine ni kwamba yeye ni bora kuliko Blagnon.
Tukiwa tunasema pengine ukawa ni usajili mzuri, tukumbuke kuwa Juma Luizio si mshambuliaji na haijawahi kuwa mshambulizi wa kutegemewa huko Zesco. Alikiwa ni mchezaji wa ziada, na amepata kucheza mechi chache sana akiwa ameanza.
Je anaweza kuwa na impact zaidi ya ile ya Blagnon?
Ukisikia usajili wa Kamari/Kubahatisha ndio huu sasa.
Ninachokiona ni kwamba mzunguko wa pili Simba itafunga mabao machache sana kuliko mzunguko wa kwanza. View attachment 446316View attachment 446317
Juma Luizio amezaliwa mwaka 1997 - Ana miaka **
Najiuliza ni nini huwa wanafikiria hasa pale wafanyapo usajili wa wachezaji wapya.
Tatizo kubwa sana ambalo wamekuwa nalo tangu Tambwe awanyooshee mkono wa kwa heri, ni nafasi ya Ushambulizi.
Ila cha ajabu zaidi ni pale wanapopata mshambuliaji mwenye ubora wa wastani na kushindwa kukaa naye kwa kipindi kirefu.
Mimi binafsi sikuona Tija ya kumuondoa Blagnon. Basi tukadhani kuwa kunafanyika usajili wa Upgrade. Yaani kuleta kilicho bora zaidi. Nilishtuka na kupigwa na butwaa baada ya kusikia Juma Luizio kutoka Zesco ndio anakuja kuchukua nafasi ya Blagnon. Kwa lugha nyingine ni kwamba yeye ni bora kuliko Blagnon.
Tukiwa tunasema pengine ukawa ni usajili mzuri, tukumbuke kuwa Juma Luizio si mshambuliaji na haijawahi kuwa mshambulizi wa kutegemewa huko Zesco. Alikiwa ni mchezaji wa ziada, na amepata kucheza mechi chache sana akiwa ameanza.
Je anaweza kuwa na impact zaidi ya ile ya Blagnon?
Ukisikia usajili wa Kamari/Kubahatisha ndio huu sasa.
Ninachokiona ni kwamba mzunguko wa pili Simba itafunga mabao machache sana kuliko mzunguko wa kwanza. View attachment 446316View attachment 446317
Juma Luizio amezaliwa mwaka 1997 - Ana miaka **