Inashangaza sana; Yaani ile timu Magufuli yote inamsapoti Tundu Lissu licha ya kuwa wawili hao walikuwa mahasimu wakubwa

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
Mpo salama Kabisa!

Kuna Jambo linashangaza Sana.
Asilimia kubwa ya wafuasi wa Magufuli wanamuunga Mkono Tundu Lisu licha ya kuwa Wawili hao walikuwa mahasimu Wakubwa.
Lakini Leo hii wafuasi hao wameamua kumuunga Mkono Tundu Lisu.

Hii inamaanisha Jambo gani Hasa?

Wakati kwa upande wa pili Wanaomuunga Mbowe Mkono wengi wao ni Timu Msoga.
Hii inamaanisha nini?

Tupo hatupo!
 
Lissu ni msema kweli
Mzalendo wa kweli, kama alivyokuwa JPM
 
Waorodheshe ili tuwatafiti
 
Hizo timu zimesha tudunisha vya kutosha,tunataka timu tofauti kwa umoja wetu.
 
Ndio Siasa..

February Anakamba kampigia kura ya urais Suluhu
 
Tuna msapoti kwasababu Magufuli hatendewi haki na mrithi
 
Japo hatujamsamehe bado kwa kumuita mzee wetu dikteta uchwara ila twende nae kwanza tutajua huko mbeleni
 
Kama hujaropoka kama Lissu tutajie jina moja tu la mtu ambaye ni Timu Magufuli anamsapoti Lissu. Usiootaja basi jua umeropoka!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…