Inauma sana nahaivumiliki

Hee hii ni kuingilia maisha ya watu engelikuwa wewe ndie mwenye mume ninge sikitika na pia kukuombe kwa Mungu lakini unataka kumuingilia mdogo wako kwenye mji wake.

Kakutuma kujalalamika nakuomba ushauri hapana kuttokana na maelezo yako ujue mapenzi yao mpaka wamepata watoto wapo hiyo 10 sijui nikidado vyovyote vile mdogowako anampenda jama ndomana yupo nae naanaelewa hilo mwenyewe anajua kwanini anaishinae kwahiyo wewe achananayo muhim nduguyako karizika nae
 
Wacha umbea wewe maisha ya watu wewe yanakuhusu nini.
Mke na mume wamekubaliana wewe unawashwa nini?
Kama ni dada yako kamchukue akulishe wewe!
 
Hii imekaa kichuki binafsi sana. Maisha ni kusaidiana kati ya mume na mke. Nahisi wewe hujaolewa ndio maana hujui maana ya kile kiapo cha kusaidiana katika shida na raha. Tofautisha kati ya mume na buzi au mume na boi frendi.

Ehee tuambie wewe huyo mume wako unamsaidia au ndio umemgeuza ATM. Kimsingi umewadhalilisha wanawake wengi sana kwa huu upuuzi uliopost. Siungi mkono wanawake wanaodhani cashflow ni one direction na wanaofuatilia ndani ya nyumba za wenzao kujua muwe kanunua nini, katoa shs ngapi....
 
Naomba niwaulize wadada? Hivi kwa nini huwa mnapenda sana kuanika mambo mabaya ya ndoa za ndugu zenu kuliko mazuri yao? Kuna mtu aliwahi kuniambia kwamba ndoa nyingi huvunjika kwa sababu ya ufukunyuku wa ndugu wa wanandoa.

We unaogopa kumweleza shemeji yako unaleta hapa huo uzi, si afadhali ungemwambia mhusika ndo alete hiyo kitu ili tumpe ushauri kuliko wewe ambaye mbali na kumdhalilisha shemejio hadharani, umeshindwa pia kumsaidia nduguyo zaidi ya kuja na kuyaanika madhaifu ya shemejio. Omba Mungu wambea wasiende kumwambia shemejio, maana usije shangaa unasababisha matatizo zaidi kwa nduguyo.

Halafu Lizzy amekuuliza swali, lijibu ili tupate kujua upeo wako wa ufahamu wa maisha ya nduguyo kabla hajaolewa, vinginevyo tutaona kama umedandia treni/gari kwa mbele tu.
 

yawezekana mdogo wako alilazimisha ndoa sasa jamaa anamkomoa?????
 
halafu ulivyoandika kwa kukosea kosea sijui ndo hasira zenyewe hizo?
 
anakula raha au anataabika?

Jiulize kwa nini hataki kuachana na hiyo ndoa? Kuna kizuri zaidi anachokipata kinacho balance huo ubaya wa mumewe, we endelea na unung'aembe wako, mwenzio mchana taabu, usiku akienda kualala kitandani kwa raha zake!
 
Tatizo si kulishwa na kuvishwa. Tatizo ni matumizi machafu ya huyo njemba!! Hapo nuksi. Mama amkatie laini kwanza
 

Kama hujui mwanzo wao huyo jamaa alikuaje huna haki ya kumsema eti hafai...
Yawezekana mdogo wako mwenyewe alimkubali kama alivyo alafu badala ya kujilaumu yeye sasa hivi anamlaumu kaka wa watu.
 
dunia na vituko vyake mpe pole mdogo wako..........
kuna kitu sikielewi mbona idadi ya wanaume wa sampuli hii wameongezeka sana tatizo ni nini?
Malezi tunayowalea tunawaacha vijana wetu wanakimbizana na cartoon za Ben Ten, Tom and Jerry unafikiri akiwa mkubwa ataweza kukimbizana na pesa.

Kila kitu unamletea na akiwa college gari na laptop tunawapa then unategemea ni watakuja kuwa waume wa ain gani? Na kwa upande wa wasichana wetu tunawaambia wasome kwa bidii maisha ni magumu siku hizi wanaume hawataki magolikipa matokeo yake nini unafikiri?

Ndio kizazi tunachokiona sasa na tutaendelea kukiona, unless tubadilishe style ya malezi yetu.
 
jamani wadada, kwenye ile sredi nyingine si mlikuwa mnaapa pesa si tatizo, labda kaka hana hela, kazidiwa na mkewe afanyeje?

Kumbe huwa mnachangia sredi kwa swaga sio ukweli.
 
Kama mlalamikaji angekuwa mwenyewe mwenye mume wake ningechangia.Lakini kwa sababu imeletwa na mtu mwingine sichangii kitu.
 
Kweli Lizy kuna vitu vingi vinaepukika japo si vyote. Wadada inabidi wajue wanataka wanaume wa aina gani especially when it comes to crtitical behavior.

Hizi tabia huwa si za ghafla ila watu wengi wanaingia kichwa kichwa; labda kwa kuhofia kukosa ndoa. But sometimes ni bora uwe peke yako kuliko kuwa na bora ndoa.

Nina mtoto wa aunt yangu medical doctor aliolewa in late 30s na mkaka mlevi kinoma wakati kwa kina aunti zangu ni watu wa swala tano, aunti ajati uncle alhaji. Wote tulijua aliolewa bora ndoa; na hivi navyoandika walisha divorce na haukupita muda mumewe akafa. But alichopata ni kuwa na watoto ambao si haramu (ndani ya ndoa). Kwa hiyo motivation ya kuolewa inachangia pia.

 
Pesa si tatizo ila usiwe na pesa uwe na heshima na mapenzi. Sasa pesa huna afu umekazana na vimada aisee kutokuwa kwako na pesa lazima kugeuke tatizo.

If I were to choose I'd rather get married to poor with love kuliko rich kicheche. Sasa poor+kicheche= balaa

My reasoning ni kuwa where there is love its hard to notice kuwa mumeo ana pesa au hana; mtaona kuwa pesa ni yenu; na as long as inatosha it doesn't matter who contributes what. Kwenye penzi hakuna mahesabu. Ukiona couples ziko makini na kuangalia who contributes what jua penzi liko nusu nusu.
jamani wadada, kwenye ile sredi nyingine si mlikuwa mnaapa pesa si tatizo, labda kaka hana hela, kazidiwa na mkewe afanyeje?

Kumbe huwa mnachangia sredi kwa swaga sio ukweli.
 

sioni kosa kwa mwanaume, kwani mwanamke akiolewa pia na
kazi, miradi yake nk vinakuwa chini ya mme wake. vinginevyo wawe
wanagereshana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…