NDOA; Nyumbani Daima Omba Amani
Wakati wakuapa anakumbuka alisema nini?anakumbuka nyakati zote alizoahidi kua atakua na mkewe?
Wanaume jamani kutandika au kuweka net kuna ishu gani??
Nijuavyo wanaume ni watu wasiopenda malumbano sasa mbona huyu anakua tofauti?ushajua mkeo mjamzito,awe anavunga au ni kweli usjali,wewe fanya pale alipogoma wala asibishane nae hata dk moja,kama huyo mwanamke yuko sawa atajirudi tena kabla hajazaa,ajifunze kuwa mkimya na kufanya anachogoma bila majibizano mana hayo ndio yanampa mkewe power yakuongea kwa kufanya hivyo lazima atanyooka na tendo la ndoa kama kawaida ajaribu wiki tu aone,naamini mwanaume alieoa anaweza.
Kutafuta wa pembeni simshauri coz pesa nayopoteza kwa malaya huyo ni bora akazitumia kuandaa vitu vya mtoto na maandaizi ya mkewe kujifungua kwenye hospital nzuri na kuhakikisha anapata lishe bora ili azae mtoto mwenye afya
Sijui mwenzangu ni mkristo au mwislam ila biblia yangu inasema kwenye Mithali 6:32-33 aziniye na mwanamke ni mpumbavu na ukiendelea mbele utapata maneno mazuri tuuu,pia kumbuka huyo ni mkeo na bado mtazaaa na kuzaa na pia mtakua pamoja hadi kifo kiwatenganishe sasa utabadili wangapi? na Mungu anakuangalia tu au?
"Usifanye kosa kwakua mwenzio amekosa"