Inawezekana hatujui ukweli kuhusu Suma Lee..

Inawezekana hatujui ukweli kuhusu Suma Lee..

Interest

JF-Expert Member
Joined
Apr 11, 2015
Posts
3,434
Reaction score
7,072
Tupige soga kidogo kuvusha wikiendi..

Sisi 'old skool' wa Bongofleva tuna mambo yetu. Hatushughulishwi na story za kizazi hiki cha kina Harmonize.

Ndio maana mtaona nyuzi zetu mostly zinawahusu kina Sumari, Nina, Sintah, Wanjara, Aminata, Seven na kaka zao wakiwemo hawa 'kina Sumalee.

Nisizunguke sana. Nataka tuchimbe sababu halisi za Suma kuacha muziki. Tuachane na hizi saundi za kujisalimisha kwa dini.

Pasipo kuingilia uhuru wake wa kuchagua kujielekeza kwa maulana, naamini bado tuna haki ya kujua baadhi ya mambo ili kuweka rekodi sawa.

Zipo fununu kuhusu kuharibu Kenya. Kwamba lipo jambo zito na la siri alilolifanya huko na ndilo lililompelekea hadi kuacha muziki na kuamua "kujificha" huku alipo sasa.

Ni jambo gani? Sijui. Niliona mdau fulani wa burudani hivi karibuni alitaka kugusia halafu akapotezea (tazama ambatanisho).

Ni siri nzito? Ndivyo inavyoaminika. Tunayo matukio mengi ya watu mashuhuri kujificha madhabahuni kwa lengo la kuficha siri zao.

Tukiyajua tutajifunza na kusaidia wale vijana wanaotamani kuingia huko ili kama kuna ya kuepuka, wayaepuke.

Yaani Suma aachie banger la HAKUNAGA (best comeback song ever) baada ya kufifia, halafu ghafla tu aache muziki?

Lipo jambo na hapa naamini tutayajua mengi..

IMG_20210423_034558.jpg
 
Alipata zaidi ya milioni 100 Kwa wimbo mmoja Tu hakunaga..akanunua VX milioni 70
Ikaibiwa...

Huwa inanishangaza Sana hii story..
Kwanini ilikushangaza? Hebu endelea zaidi unachotaka kusema..
 
Ila ni kweli kuna namna flani iliyompelekea kuacha muziki

Siku za nyuma kabla hajaacha muziki nilimsikia kupitia XXL akijisifia kuwa ameagiza sijui verosa sijui mark x kutoka uingereza Ila ilivyofika bongo wakampiga vifaa bandarini....nikasema dah mwamba Yuko mcharo lakini ghafla akaacha mziki iko namna...
 
Ila ni kweli kuna namna flani iliyompelekea kuacha muziki

Siku za nyuma kabla hajaacha muziki nilimsikia kupitia XXL akijisifia kuwa ameagiza sijui verosa sijui mark x kutoka uingereza Ila ilivyofika bongo wakampiga vifaa bandarini....nikasema dah mwamba Yuko mcharo lakini ghafla akaacha mziki iko namna...
Na aliacha akiwa yupo vizuri na 'muziki' ukiwa umeanza kumlipa.
 
Back
Top Bottom