Ingawa sijawaona Pele na Maradona, ila nina uhakika hawamfikii Gaucho

Viol

JF-Expert Member
Joined
Dec 15, 2009
Posts
25,420
Reaction score
18,298
Sahau kina Pele na Maradona, Ronaldinho ni kitu kingine.

Weka mbali takataka kama Messi na Christiano Ronaldo. Kwenye historia ya mpira ushawahi kumwona nani bonge la shuti katuliza kwa mgongo na ikakaa?
 
Gaucho alikuwa anacheza kwa pride yake binafsi, hata hivyo ni mchezaji mzuri...

Maradona na Pele walikuwa wanacheza kuweka historia binafsi na za timu...
 
Hebu tafuta clip ya pele kwanza,kisha uje utupe majibu
 
Sahau kina pele na maradona Ronaldinho ni kitu kingine,weka mbali takataka kama messi na christiano.Kwenye historia ya mpira ushawahi kumwona nani bonge la shuti katuliza kwa mgongo na ikakaa?

Ubora na umaarufu wa mchezaji ni kuwezesha timu yake kuchukua ubingwa na pia kuwezesha timu yake ya taifa kuchukua ubingwa wa dunia ndivyo Pele na Maredona walivyofanya. Huyo unayemtaja nini amefanya kwa timu ya taifa lake kuwezesha kuchukua kombe la dunia? Usipime kwa mtazamo wako ila angalia macho ya wengi pamoja na jopo la vyombo vya habari na wataalamu wa mchezo huo kwa vigezo vyenye mizani ya ukweli si ushabiki wa kile moyo ukipenda.
 

Dinho kashinda Vikombe vyote....Kabati lake limejaa!!
 
Muanzisha mada anamzungumzia gaucho na si timu ya gaucho
 
Unajua ushabiki uko wa aina nyingi... Kuna mtu anashabikia ujuzi binafsi wa mchezaji, mwingine anashabikia jitihada binafsi za mchezaji... na mwingine udambwiudambi wa mchezaji kwake sio deal ila mchezaji kaisaidiaje timu kufikia malengo... Sasa tuwachambue..

Pele> Mfalme wa soka anaishi: Huyu jamaa ni balaa,, labda tufe wote then wazaliwe wengine ndiyo atokee kama yeye... Kwanza fikiria amecheza kipindi hicho black au waafrika tulikuwa hatuthaminiwi kama watu,.. wazungu walikuwa wanatudharau na kutuona kama hazijatimia.. Lakini huyu mwanaume aliwaonyesha kazi.. piga goli kama mvua,, japo hakuwa mtu wa udambwi sana lakini aliamini kuisaidia timu yake kwa kufunga magoli ndiko kitu muhimu katika maisha yake ya soko..

Maradona> Huyu jamaa yuko vizuri mno kwenye kuchezea mpira (ball dancer).. Ufupi wake na kasi ulimsaidia sana kutesa mijitu yenye miraba minne ya Ulaya... Japo alikuwa na kapaji na kuisaidia timu yake lakini hakujitambua kapewa kipaji na mungu ili akifanyie nini.. Uvutaji madawa na ulevi vilimfanya ashindwe kuvunja rekodi za Pele...

Ronaldinho Gaucho>.. Huyu jamaa ni kizazi kipya cha soka. vyenga vya hatari, dribbling za kutosha, nguvu na kumiliki mpira huyu jamaa utampenda.. Tatizo la dunia ya sasa watu wanaweka rekodi kwa maana umefunga magoli mangapi, assist ngapi na umenyanyua kwapa mara ngapi... sio vyenga, cjui kazu, tobo.. no, huo mpia sasa hivi hakuna.. Ulikuwepo enzi ya Maradona.... Japo kabeba vikombe kadhaa kwa timu zake, Barcelona na Brazil lakini historia za wachezaji wa zamani wa timu hizo zinamficha asionekane..

Messi>.Sasa kwa mpira wa kisasa huyu ndiyo mwenyewe... Waswahili wanasema kila kizazi na nabii wake.. Kwenye mpira wa leo huyu jamaa ni nabii wetu. Kumbuka mpira wa sasa unaunganisha style zote hizo za juu na kuziweka pamoja.. Messi anajua kuuchezea mpira, vyenga vipo, anajua nini timu yake inataka ndiyo maana huwa hajing'ang'nizi kufunga hata kama hayuko kwenye nafasi.. Lakini muhimu kuliko yote ni determination ya kuvunja record za dunia na huwezi kuzivunja kama huna discipline ya kwako mwenyewe pamoja na timu kwa ujumla.. Ukitaka kuamini angalia timu nzima ya Barcelona yaani kila mchezaji jicho kwa Messi na kila mmoja anafurahia mafanikio ya huyu dogo.. Aombe kwa Mungu aendelee kuwa na maisha marefu ya soka may be, just may be anaweza akafikisha magoli 1000 kama si kuvunja kabisa rekodi ya Pele.. Ana miaka 27 mungu akimjalia acheze miaka saba mingine katika kiwango hiki tutakuwa tunazungumzia mengine...

CR7> Anaujua.. Mchezaji mwenye kaliba zote za soka la kisasa... kasi, nguvu na chenga zake za break ni balaa.. Unajicho lenye lenzi kali sana ya goli liliko.. Kachukua ufundi kidogo wa maradona na umakini wa Pele.. Ila tatizo kwa CR7 ni kama Nabii asiyekuwa na kizazi. kwa maana gani..? kumbuka kuwa CR7 alianza kutamba kipindi wafalme wengine wanatawala.. Amemkuta Ronaldo mwenyewe, alimkuta Zinedine Zidane mbaya zaidi alimkuta Ronaldinho Gaucho yuko moto vibaya sana...!! Ingekuwa ngumu kwake kutamba mbele wa miamba hao.. Sasa hao jamaa enzi zao zilivyoisha bahati mbaya tena kwake, kizazi kipya cha soka kinaibuka, makao makuu Katalunya.. Anakutana na kina Messi wananjaa ya kufa mtu.. tatizo jingine akaenda Real Madrid ambao ni mahasimu wa Barcelona... Kwa misimu kama mitatu mfululizo Madrid wameteseka sana kwa Barcelona.. Hicho ndicho kinachomficha CR7 awe nyuma ya hao vigogo wa soka waliowahi kutokea duniani..

Hizi tuzo za FIFA wakati mwingine ni mbwembwe tu.. Ila record zinabaki kama msahafu.

Kama una swali uliza, kama una ya kuongeza uongeza!!
 
Kwa hiyo mnataka kuniambia kwa msimu huu peke yake,elias maguli wa simba ni mchezaji bora kuliko mesi kwa sabb maguli wa simba ameisaidia simba kubeba mtani jembe na kombe la mainduzi wakati mesi hana kombe hata moja...na bado huyo maguli anatarajia kubeba kombe la rowasacup octoba
 
Khamis gagarino,method mogela"fundi",malota soma"ball jugler",zamoyoni mogela"golden boy",……
 
Sahau kina pele na maradona Ronaldinho ni kitu kingine,weka mbali takataka kama messi na christiano.Kwenye historia ya mpira ushawahi kumwona nani bonge la shuti katuliza kwa mgongo na ikakaa?

Pele na D10S hujawaona, huo uhakika unautoa wapi? Bora ungesema una 'amini', halafu huu ni 'mpira wa miguu /football" sio mpira wa mgongo. Na hivi mbwembwe za kuuchezea mpira ndio zinamfanya mchezaji kuwa bora zaidi? Kama ni hivyo basi Okocha alikua bora kuliko Weah
Bila kuweka vigezo vya kutoa mwongozo wa kulinganisha na kutofautisha ubora wa mchezaji mmoja mmoja, kila mtu atakuja na mchezaji wake na kuandika ngonjera kama hizo zako.
Na ungetaka msaada wa kumsifia Dinho kwa mbwembwe, tambo, majigambo, ngonjera na danganya toto za kufa mtu, ungemuita huyu buluda, Gang Chomba, maana huyu ukiwa karibu yake ukamsema vibaya Dinho, anaweza kukugeuza kitumbua
 
Last edited by a moderator:

Gaucho hajasababisha Brazil ichukue Ubingwa WC-2002? Ni Gaucho huyo aliwatungua Waingereza nadhan robo au nusu fainali goli 2-0 na kisha kutolewa kwa kadi nyekundu. Ni kwa ushindi huo timu ilifika Fainali na kuifunga Ujerumani na kisha kutwaa kombe la dunia 2002, ulitaka afanyeje? Pamoja na ubora wa Messi na CR7, Gaucho atakumbukwa kwa vipaji vya kuuchezea mpira atakavyo utafikiri anatumia mikono.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…