Ingekuwa heri JK uage sasa
MHESHIMIWA Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, salaam aleykum. Juma lililopita
niliwasiliana na Watanzania wote kwa njia hii ya makala.
Nilijaribu kuwachokonoa ili kupata mawazo yao juu yako.
Na kwa bahati nzuri nilikuwa nimeongea moja kwa moja na
Watanzania wote wakiwamo wasaidizi wako muhimu. Na ili
kuwahakikishia kwamba niliwalenga na wao pia niliamua
kuwataja kabisa pale niliposema, "Yote kwa yote ni
kwamba
kila mtu anajua sasa Rais Kikwete uwezo wake wa
kuliongoza
taifa na chama chake umepungua.
"Ninaamini ndani ya dhamiri yangu kwamba hata
wasaidizi wake, wakiwamo usalama wa taifa, mawaziri na
manaibu mawaziri, wanamtandao na wapambe wake, wabunge,
viongozi wenzake ndani ya chama, watendaji wake
serikalini
na wasaidizi wake wengineo wote wanajua hili".
Nilifanya hivyo kwa makusudi ili kupata maoni yao juu ya
hili. Nawatambua sana wasaidizi wako. Ni watu mahiri sana
kwa kulinda maslahi yao na ya wakubwa wao. Nilijua
watanijibu haraka haraka kwa kukanusha ukweli huo mdomoni
huku mioyoni mwao wakiutambua. Lakini hawakufanya hivyo.
Hii inathibitisha kwamba hata wao ukweli uliwagusa na
wamefikia mahali ambapo hawawezi kupingana nao.
Wa kwanza kabisa kuwasiliana nami ni kiongozi wa zamani wa
CCM katika mojawapo ya nafasi za uongozi ndani ya chama
ngazi ya kitaifa. Yeye alinipigia simu kabisa na
kujitambulisha kwa jina, nami nikamtambua kwa sauti
kwamba
ni yeye. Akanipongeza kwa kusema nimeandika vizuri sana na
kwa kweli maneno yake na sauti yake yalionyesha dhahiri
kukubaliana na ukweli niliouainisha.
Huyu ndiye akazidi kuthibitisha nilichokizungumza katika
aya hiyo hapo juu. Ukweli umewasuta ndani ya dhamira zao
na
kwa kweli umefika wakati ambao ukweli hauwezi kufichika
tena. Wengi sasa wanaogopa kukutetea hadharani
wasijeonekana vituko kwa kuupinga ukweli ulio wazi (naked
truth).
Mheshimiwa Rais, wasomaji walionitumia ujumbe mfupi wa
simu, walionipigia simu, walionitumia barua pepe na hata
waliozungumza nami uso kwa uso, wote wamenipongeza kwa
ujumbe uliokuwa wazi ukieleza ukweli halisi na kila mmoja
wao aliishia kusema 'atang'oka' 2010. Baada
ya
kutafakari ujumbe wa wasomaji na matukio yaliyoripotiwa
kwenye vyombo vya habari juma lililopita, nimeamua
kukuandikia waraka huu ili nikupatie ushauri makini
lakini
bure.
Msomaji mmoja, kwa mfano, aliongea kwa uchungu jinsi
ulivyojibu swali la mwanahabari kule Ufaransa.
Ulipokuuliza
kwa nini nchi yako ni maskini ukasema eti hata wewe
hujui.
Kwa maoni yake ilikuwa ni aibu kubwa kwa kiongozi wa nchi
kujibu hivyo tena mbele ya viongozi na wanahabari wa
kimataifa. Uliuonyesha ulimwengu kwamba nchi hii ni ya
ajabu na watu wake ni wa ajabu. Ni kama ulikuwa
unathibitisha kauli iliyopata kutolewa na mwandishi mmoja
kwamba Tanzania ni nchi pekee duniani inayoweza kukaa
miaka
10 bila rais na bado ikabaki na amani.
Kwa maoni yangu pia, rais wa nchi kusema hajui umaskini wa
wananchi wake unatokana na nini ni sawa na kusema nchi
haina kiongozi. Rais wa namna hiyo hawezi kuhangaika na
mipango ya kuiondoa nchi katika umaskini, maana hajui kwa
nini wananchi ni maskini. Anafikiri pengine ni
"wavivu tu
wa kufikiri" ama "fursa zipo ila kwa ujinga wao
hawataki
kuzitumia".
Rais wa namna hiyo hawezi kujua madhara ya ufisadi wa EPA,
Meremeta, Tangold, Kiwira, mikataba ya Richmond, IPTL na
jinsi inavyochangia umaskini wa watu wake. Hawezi kuona
ubaya wa rais na mke wake kujiingiza kwenye biashara kwa
kutumia ofisi, fursa na vyeo vyao vya Ikulu kuwanyonga
wananchi. Na kwa sababu hiyo hawezi kujihangaisha
kuyashughulikia madudu kama hayo kama unavyofanya wewe
hivi
sasa.
Rais wa namna hiyo atakuwa 'busy' na safari za nje
zisizo na kikomo, kukutana na marais wakubwa kama akina
George Bush tena wanapokutana Bush atampiga piga mabegani
rais kama huyo kama alivyofanya alipokuja hapa Dar es
Salaam, na tungetamani kupata tafsiri ya kitendo hicho
cha
George Bush, ambaye wafuatiliaji wanasema hata
mlipokutana
Japan alikupiga piga begani tena, kutoka kwa Salva
Rweyemamu yule mwandishi wa zamani aliyeisakama serikali
kwa kalamu yake, lakini baadaye akawa mwanakampeni wako
mahiri kwa kutumia kalamu hiyo hiyo na baadaye
ukamzawadia
ukurugenzi wa mawasiliano Ikulu.
Mheshimiwa, watu wanashangaa hata kitendo cha serikali yako
kushindwa kutumia vyanzo mbalimbali vya maji,
visivyokauka
tulivyonavyo hapa nchini na ardhi safi tena kubwa
inayofaa
kwa kilimo cha umwagiliaji kujihakikishia chakula cha
kutosha. Lakini badala yake unakwenda Italia kwa kutumia
mamilioni ya shilingi kuomba chakula kwa WFP.
Mheshimiwa Rais, si siri ni aibu kubwa. Mabilioni
yaliyopotea kwenye ufisadi yangetosha kuanzisha
'scheme' kubwa 13 za umwagiliaji kwenye mikoa 13
ya
nchi hii. Na hesabu zake ni rahisi mno wala huhitaji
kutumia shahada yako ya kwanza ya uchumi ambayo hata
hivyo
sijui kma umewahi kuitumia.
Chukua milioni 152 kwa siku kwa mwaka mmoja tu zilizolipwa
kwa Richmond/Dowans ambazo kwa siku 365 za mwaka ni
bilioni
55. Jumlisha bilioni 2,098 zilizolipwa kwa IPTL kwa miaka
minane tu kwa kuzingatia kauli ya aliyekuwa Naibu Waziri
wa
Nishati na Madini, William Ngeleja, bungeni Dodoma
Agosti6,
2007 kwamba kwa kipindi cha Julai 2005 hadi March 2006
peke
yake IPTL ililipwa jumla ya bilioni 262.3. Kwa vipindi
vinane tu kama hivyo kampuni hiyo imelipwa jumla ya
bilioni
2,098. Jumlisha bilioni 133 zilizoibwa kupitia EPA, kisha
juu yake ongeza bilioni zisizopungua 600 zilizopotea
kupitia ujenzi wa minara miwili pacha pale BoT. Halafu
umalizie na mabilioni yaliyopotea kupitia viufisadi
vingine
vingine kama ubinafsishaji wa TTCL, NBC, Kiwira, n.k
ambazo
nazo si chini ya 100.
Halafu chukua hiyo jumla inayofikia bilioni 2,986 bila
kuongeza bilioni ulizozitumia wewe kwa safari zako za nje
tangu uchaguliwe kuwa rais. Igawanye jumla hiyo kwa
gharama
za mradi mzima wa kupeleka maji Shinyanga ulioshikiwa
bango
na best yako ili aje kuonekana anafaa kuwa waziri mkuu wa
nchi hii. Utapata 13 ambazo ni scheme kubwa za
umwagiliaji
zenye thamani ya sh bilioni 225 kila moja.
Ina maana tungeweza kuwa na scheme kama hizo katika mikoa
13 inayoongoza kwa ardhi inayofaa kwa umwagiliaji. Njaa
ingetupata wapi. Hivi sasa dunia inapolia na kupanda kwa
bei za vyakula sisi tunaoita kilimo uti wa mgongo wa
uchumi
wetu tungekuwa matajiri kwa kuuza chakula.
Lakini hivi sasa eti serikali yako inapiga marufuku kuuza
chakula nje ya nchi, mkulima anayetegemea kuuza chakula
chake cha ziada ili apate matumizi yake mengine ikiwamo
kusomesha watoto unamwambi nini?
Mheshimiwa Rais, watu waliodunisha maisha ya Watanzania
kiasi hicho eti bado hutaki kuwachukulia hatua hadi leo.
Umeunda tume juu ya tume nyingine lakini mafisadi
wanaendelea kutesa. Ajabu zaidi chama unachokiongoza juma
lililopita, kimetangaza eti kumpa onyo kali aliyekuwa
naibu
meya wa Ilala na kumzuia kugombea cheo chochote zaidi ya
udiwani alionao, sababu eti ni kushiriki bomoabomoa ya
Tabata Dampo na kuisababishia hasara serikali ya sh
bilioni
1.8, kuwasababishia usumbufu wananchi wa Tabata Dampo na
kukiaibisha chama.
Gazeti hili likaiandika habari hiyo Jumatatu wiki hii, kwa
kichwa kilichosema; 'CCM yacharuka'. Naomba
kupingana moja kwa moja na maneno aliyoyatumia mwandishi
wa
habari hiyo. Kimsingi CCM haijacharuka. Bali ina mkakati
pengine unaosimamiwa na wewe mwenyewe mwenyekiti wako
kukisafisha chama. Msitudanganye kiasi hicho, kwamba mna
uchungu sana na pesa za serikali, mnawajali wananchi na
kulinda hadhi ya chama chenu.
Fikiria hasara za mabilioni ya serikali niliyoyataja hapo
juu, yote yamesababishwa na wana-CCM, fikiria Watanzania
milioni 40 wanaoteseka kwa ajili ya wana CCM na ukumbuke
jinsi hadhi, si tu ya chama unachokiongoza bali pia ya
serikali unayoiongoza ilivyoporomoka ndani ya mwaka
mmoja,
kwa ajili ya wana-CCM. Lakini hamjawakaripia wala
kuwafuta
uanachama kama mlivyofanya kwa Naibu Meya Yakubu.
Huu ni usanii ambao umeshajulikana kwa Watanzania.
Mheshimiwa Rais, juma lililopita umetoa kali nyingine ya
mwaka. Umewaasa Watanzania wavumilie shida wasikate
tamaa.
Hii nayo ni kauli nyingine ya mzaha kwa Watanzania kama
ile
ya kusema hujui umaskini wao unasababishwa na nini.
Natamani ungekuwa unasoma maoni ya wasomaji. Siku hizi
Tanzania Daima imeanzisha sehemu ya maoni ya wasomaji
wanaosoma gazeti hili, kwenye tovuti. Msomaji mmoja
aliposoma alisema hivi: "Kaka yetu usipate tabu wewe
sema
tu.
Sisi tumezoea shida, huna tofauti na Karume anayewaambia
Wazanzibari watazoea tu. Sasa sisi tumezoea na wewe
endelea
kula nchi maana mafuta si kazi yako. Wewe linda mtandao
wako
usisambaratike, maana inabidi uutumie kurudi madarakani
mwaka 2010." Haya si maoni ya mtu anayekuambia kwa
wema.
Huyu ana uchungu ndani ya moyo wake na kwa ujumla maneno
yake ni laana kwa serikali yako.
Mwingine akasema hivi: "...Kikwete suala la mafuta na
maisha magumu havimhusu kabisa. Ndiyo, si anatuonyesha
hivyo kwa kuwalinda mafisadi? Na sasa kapata kisingizio
cha
bei ya mafuta basi ndiyo itakuwa hadithi. Hivi
wadanganyika
wenzangu mnafikiri bei ya mafuta ikishuka (let's say)
hadi nusu, ndiyo maisha yatakuwa bora kwa kila
mdanganyika?
"Dhahabu imepanda sana bei katika soko la dunia. Kwa
nini vitu kama hivi vimeshindwa kufidia pengo la mafuta
yaliyopanda?
Watu wengine wanafananisha Bongo na Marekani - eti na
Marekani maisha yamepanda. Nyie ndugu zangu hebu acheni
mzaha! Wewe unakula humburg na pizza Macdonald halafu
unatuambia maisha yamepanda? "Chonde chonde jamani.
Natamani mngerudi huku mkapigika mkashindia kauzu ndiyo
mngejua watu wanaongea nini " Ukurasa huu
hautatosha
kukupatia maoni ya kila msomaji, lakini natamani
ungejisomea mwenyewe habari hiyo kisha chini yake usome
maoni ya watu.
Wasaidizi wako wanaweza kukusaidia kutembelea
http://www.freemedia.co.tz/daima/2008/7/21/habari1
Mheshimiwa Rais ningekushauri jambo moja tu. Kukubali pia
ni uungwana wa aina yake na Watanzania wanapenda watu
waungwana.
Baada ya ziara yako ndefu mkoani Tanga, utakaporejea Ikulu
fanya jambo moja tu. Andaa hotuba yako ya mwezi bila
kumshirikisha msaidizi wako yeyote. Ita waandishi wa
habari
kana kwamba unakuja kujibu tu maswali watakayokuuliza
halafu
wakisha fika toa hotuba yako kabla hujaulizwa maswali.
Waeleze wanahabari na Watanzania kwa ujumla kwamba wakati
unachukua fomu za kugombea urais mwaka 2005 hukuijua
vizuri
sababu ya umaskini wa Watanzania. Waeleze kwamba wewe
ulidhani kazi uliyokuwa nayo ni kuwaita tu wawekezaji
uliokuwa umeshazoeana nao sana ukiwa waziri wa Mambo ya
Nje
na Ushirikiano wa Kimataifa, na kwamba wakishakuja
kuwekeza
tayari maisha bora kwa kila Mtanzania yanajipa.
Sema kwamba umekuja kugundua kuwa mambo sivyo yalivyo.
Umaskini wa Watanzania una uhusiano wa karibu mno na
utawala wa nchi. Na kwamba utawala wa nchi kwa miaka
mingi
umebaki kuwa mbovu hasa kupitia 'system'
iliyojengwa na
Chama chako Cha Mapinduzi ya kulindana viongozi, bila
kujali
madhara yanayosababishwa na viongozi mafisadi hapa nchini
na
hivyo hata malaika akiwa rais wa nchi hii kupitia CCM
hakuna
maendeleo yatakayopatikana.
Sema wazi wazi kwamba kama rais wa nchi hata kama ungekuwa
na dhamira ya kuikwamua nchi kutoka kwenye umaskini
unaosababishwa na uongozi mbovu, ungeshindwa kwa kuwa
kikulacho ki nguoni mwako. Maswahiba zako waliofanya juu
chini upate urais ndiyo hao hao mafisadi waliokubuhu hata
jina la mafisadi haliwafai tena. Nasikia wengine wameanza
kuwaita 'mafisidi'.
Na wewe huwezi kuwatupa wakati ungali ukikumbuka mchango
wao mwaka 2005. Kwa sababu hiyo, ili kulinda uhusiano
wako
nao na wakati huo huo kulinda heshima kupita kiasi
uliyopewa na watanzania, umeamua kuachia ngazi na hivyo
mwaka 2010 hutagombea tena.
Wapatie Watanzania nafasi ya kuanza kufikiria tangu sasa
chama kitakachowafaa kuongoza nchi hii hapo 2010,
kutokana
na sera zake kabla hawajafikiria ni nani atawafaa kuwa
rais wa nchi baada yako. Uhakika mmoja tu nakupatia kwamba
hutabaki ulivyo machoni mwa Watanzania.
Najua wapambe wako watakulaumu sana, maana kwa kung'oka
wewe utakuwa umewakosesha ulaji mkubwa. Lakini utakuwa
umejiweka katika nafasi nzuri ya kuwa shujaa mbele ya
Watanzania, kwa kutoboa ukweli na utapumzika kwa amani
baada ya miaka 10 ya kusaka urais na miaka mitano ya
kushutumiwa na Watanzania kwa kutotoa (not delivering)
kile
ulichotarajiwa.
Naamini pensheni itatosha, isipotosha utaongezea kilimo cha
kisasa. Fanya uamuzi sasa ama utakuja kujuta
utakapostaafu.
Watafanya kama walivyomfanyia Chiluba hadi
utashangaa.
Uamuzi ni wako Mheshimiwa Rais
MHESHIMIWA Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, salaam aleykum. Juma lililopita
niliwasiliana na Watanzania wote kwa njia hii ya makala.
Nilijaribu kuwachokonoa ili kupata mawazo yao juu yako.
Na kwa bahati nzuri nilikuwa nimeongea moja kwa moja na
Watanzania wote wakiwamo wasaidizi wako muhimu. Na ili
kuwahakikishia kwamba niliwalenga na wao pia niliamua
kuwataja kabisa pale niliposema, "Yote kwa yote ni
kwamba
kila mtu anajua sasa Rais Kikwete uwezo wake wa
kuliongoza
taifa na chama chake umepungua.
"Ninaamini ndani ya dhamiri yangu kwamba hata
wasaidizi wake, wakiwamo usalama wa taifa, mawaziri na
manaibu mawaziri, wanamtandao na wapambe wake, wabunge,
viongozi wenzake ndani ya chama, watendaji wake
serikalini
na wasaidizi wake wengineo wote wanajua hili".
Nilifanya hivyo kwa makusudi ili kupata maoni yao juu ya
hili. Nawatambua sana wasaidizi wako. Ni watu mahiri sana
kwa kulinda maslahi yao na ya wakubwa wao. Nilijua
watanijibu haraka haraka kwa kukanusha ukweli huo mdomoni
huku mioyoni mwao wakiutambua. Lakini hawakufanya hivyo.
Hii inathibitisha kwamba hata wao ukweli uliwagusa na
wamefikia mahali ambapo hawawezi kupingana nao.
Wa kwanza kabisa kuwasiliana nami ni kiongozi wa zamani wa
CCM katika mojawapo ya nafasi za uongozi ndani ya chama
ngazi ya kitaifa. Yeye alinipigia simu kabisa na
kujitambulisha kwa jina, nami nikamtambua kwa sauti
kwamba
ni yeye. Akanipongeza kwa kusema nimeandika vizuri sana na
kwa kweli maneno yake na sauti yake yalionyesha dhahiri
kukubaliana na ukweli niliouainisha.
Huyu ndiye akazidi kuthibitisha nilichokizungumza katika
aya hiyo hapo juu. Ukweli umewasuta ndani ya dhamira zao
na
kwa kweli umefika wakati ambao ukweli hauwezi kufichika
tena. Wengi sasa wanaogopa kukutetea hadharani
wasijeonekana vituko kwa kuupinga ukweli ulio wazi (naked
truth).
Mheshimiwa Rais, wasomaji walionitumia ujumbe mfupi wa
simu, walionipigia simu, walionitumia barua pepe na hata
waliozungumza nami uso kwa uso, wote wamenipongeza kwa
ujumbe uliokuwa wazi ukieleza ukweli halisi na kila mmoja
wao aliishia kusema 'atang'oka' 2010. Baada
ya
kutafakari ujumbe wa wasomaji na matukio yaliyoripotiwa
kwenye vyombo vya habari juma lililopita, nimeamua
kukuandikia waraka huu ili nikupatie ushauri makini
lakini
bure.
Msomaji mmoja, kwa mfano, aliongea kwa uchungu jinsi
ulivyojibu swali la mwanahabari kule Ufaransa.
Ulipokuuliza
kwa nini nchi yako ni maskini ukasema eti hata wewe
hujui.
Kwa maoni yake ilikuwa ni aibu kubwa kwa kiongozi wa nchi
kujibu hivyo tena mbele ya viongozi na wanahabari wa
kimataifa. Uliuonyesha ulimwengu kwamba nchi hii ni ya
ajabu na watu wake ni wa ajabu. Ni kama ulikuwa
unathibitisha kauli iliyopata kutolewa na mwandishi mmoja
kwamba Tanzania ni nchi pekee duniani inayoweza kukaa
miaka
10 bila rais na bado ikabaki na amani.
Kwa maoni yangu pia, rais wa nchi kusema hajui umaskini wa
wananchi wake unatokana na nini ni sawa na kusema nchi
haina kiongozi. Rais wa namna hiyo hawezi kuhangaika na
mipango ya kuiondoa nchi katika umaskini, maana hajui kwa
nini wananchi ni maskini. Anafikiri pengine ni
"wavivu tu
wa kufikiri" ama "fursa zipo ila kwa ujinga wao
hawataki
kuzitumia".
Rais wa namna hiyo hawezi kujua madhara ya ufisadi wa EPA,
Meremeta, Tangold, Kiwira, mikataba ya Richmond, IPTL na
jinsi inavyochangia umaskini wa watu wake. Hawezi kuona
ubaya wa rais na mke wake kujiingiza kwenye biashara kwa
kutumia ofisi, fursa na vyeo vyao vya Ikulu kuwanyonga
wananchi. Na kwa sababu hiyo hawezi kujihangaisha
kuyashughulikia madudu kama hayo kama unavyofanya wewe
hivi
sasa.
Rais wa namna hiyo atakuwa 'busy' na safari za nje
zisizo na kikomo, kukutana na marais wakubwa kama akina
George Bush tena wanapokutana Bush atampiga piga mabegani
rais kama huyo kama alivyofanya alipokuja hapa Dar es
Salaam, na tungetamani kupata tafsiri ya kitendo hicho
cha
George Bush, ambaye wafuatiliaji wanasema hata
mlipokutana
Japan alikupiga piga begani tena, kutoka kwa Salva
Rweyemamu yule mwandishi wa zamani aliyeisakama serikali
kwa kalamu yake, lakini baadaye akawa mwanakampeni wako
mahiri kwa kutumia kalamu hiyo hiyo na baadaye
ukamzawadia
ukurugenzi wa mawasiliano Ikulu.
Mheshimiwa, watu wanashangaa hata kitendo cha serikali yako
kushindwa kutumia vyanzo mbalimbali vya maji,
visivyokauka
tulivyonavyo hapa nchini na ardhi safi tena kubwa
inayofaa
kwa kilimo cha umwagiliaji kujihakikishia chakula cha
kutosha. Lakini badala yake unakwenda Italia kwa kutumia
mamilioni ya shilingi kuomba chakula kwa WFP.
Mheshimiwa Rais, si siri ni aibu kubwa. Mabilioni
yaliyopotea kwenye ufisadi yangetosha kuanzisha
'scheme' kubwa 13 za umwagiliaji kwenye mikoa 13
ya
nchi hii. Na hesabu zake ni rahisi mno wala huhitaji
kutumia shahada yako ya kwanza ya uchumi ambayo hata
hivyo
sijui kma umewahi kuitumia.
Chukua milioni 152 kwa siku kwa mwaka mmoja tu zilizolipwa
kwa Richmond/Dowans ambazo kwa siku 365 za mwaka ni
bilioni
55. Jumlisha bilioni 2,098 zilizolipwa kwa IPTL kwa miaka
minane tu kwa kuzingatia kauli ya aliyekuwa Naibu Waziri
wa
Nishati na Madini, William Ngeleja, bungeni Dodoma
Agosti6,
2007 kwamba kwa kipindi cha Julai 2005 hadi March 2006
peke
yake IPTL ililipwa jumla ya bilioni 262.3. Kwa vipindi
vinane tu kama hivyo kampuni hiyo imelipwa jumla ya
bilioni
2,098. Jumlisha bilioni 133 zilizoibwa kupitia EPA, kisha
juu yake ongeza bilioni zisizopungua 600 zilizopotea
kupitia ujenzi wa minara miwili pacha pale BoT. Halafu
umalizie na mabilioni yaliyopotea kupitia viufisadi
vingine
vingine kama ubinafsishaji wa TTCL, NBC, Kiwira, n.k
ambazo
nazo si chini ya 100.
Halafu chukua hiyo jumla inayofikia bilioni 2,986 bila
kuongeza bilioni ulizozitumia wewe kwa safari zako za nje
tangu uchaguliwe kuwa rais. Igawanye jumla hiyo kwa
gharama
za mradi mzima wa kupeleka maji Shinyanga ulioshikiwa
bango
na best yako ili aje kuonekana anafaa kuwa waziri mkuu wa
nchi hii. Utapata 13 ambazo ni scheme kubwa za
umwagiliaji
zenye thamani ya sh bilioni 225 kila moja.
Ina maana tungeweza kuwa na scheme kama hizo katika mikoa
13 inayoongoza kwa ardhi inayofaa kwa umwagiliaji. Njaa
ingetupata wapi. Hivi sasa dunia inapolia na kupanda kwa
bei za vyakula sisi tunaoita kilimo uti wa mgongo wa
uchumi
wetu tungekuwa matajiri kwa kuuza chakula.
Lakini hivi sasa eti serikali yako inapiga marufuku kuuza
chakula nje ya nchi, mkulima anayetegemea kuuza chakula
chake cha ziada ili apate matumizi yake mengine ikiwamo
kusomesha watoto unamwambi nini?
Mheshimiwa Rais, watu waliodunisha maisha ya Watanzania
kiasi hicho eti bado hutaki kuwachukulia hatua hadi leo.
Umeunda tume juu ya tume nyingine lakini mafisadi
wanaendelea kutesa. Ajabu zaidi chama unachokiongoza juma
lililopita, kimetangaza eti kumpa onyo kali aliyekuwa
naibu
meya wa Ilala na kumzuia kugombea cheo chochote zaidi ya
udiwani alionao, sababu eti ni kushiriki bomoabomoa ya
Tabata Dampo na kuisababishia hasara serikali ya sh
bilioni
1.8, kuwasababishia usumbufu wananchi wa Tabata Dampo na
kukiaibisha chama.
Gazeti hili likaiandika habari hiyo Jumatatu wiki hii, kwa
kichwa kilichosema; 'CCM yacharuka'. Naomba
kupingana moja kwa moja na maneno aliyoyatumia mwandishi
wa
habari hiyo. Kimsingi CCM haijacharuka. Bali ina mkakati
pengine unaosimamiwa na wewe mwenyewe mwenyekiti wako
kukisafisha chama. Msitudanganye kiasi hicho, kwamba mna
uchungu sana na pesa za serikali, mnawajali wananchi na
kulinda hadhi ya chama chenu.
Fikiria hasara za mabilioni ya serikali niliyoyataja hapo
juu, yote yamesababishwa na wana-CCM, fikiria Watanzania
milioni 40 wanaoteseka kwa ajili ya wana CCM na ukumbuke
jinsi hadhi, si tu ya chama unachokiongoza bali pia ya
serikali unayoiongoza ilivyoporomoka ndani ya mwaka
mmoja,
kwa ajili ya wana-CCM. Lakini hamjawakaripia wala
kuwafuta
uanachama kama mlivyofanya kwa Naibu Meya Yakubu.
Huu ni usanii ambao umeshajulikana kwa Watanzania.
Mheshimiwa Rais, juma lililopita umetoa kali nyingine ya
mwaka. Umewaasa Watanzania wavumilie shida wasikate
tamaa.
Hii nayo ni kauli nyingine ya mzaha kwa Watanzania kama
ile
ya kusema hujui umaskini wao unasababishwa na nini.
Natamani ungekuwa unasoma maoni ya wasomaji. Siku hizi
Tanzania Daima imeanzisha sehemu ya maoni ya wasomaji
wanaosoma gazeti hili, kwenye tovuti. Msomaji mmoja
aliposoma alisema hivi: "Kaka yetu usipate tabu wewe
sema
tu.
Sisi tumezoea shida, huna tofauti na Karume anayewaambia
Wazanzibari watazoea tu. Sasa sisi tumezoea na wewe
endelea
kula nchi maana mafuta si kazi yako. Wewe linda mtandao
wako
usisambaratike, maana inabidi uutumie kurudi madarakani
mwaka 2010." Haya si maoni ya mtu anayekuambia kwa
wema.
Huyu ana uchungu ndani ya moyo wake na kwa ujumla maneno
yake ni laana kwa serikali yako.
Mwingine akasema hivi: "...Kikwete suala la mafuta na
maisha magumu havimhusu kabisa. Ndiyo, si anatuonyesha
hivyo kwa kuwalinda mafisadi? Na sasa kapata kisingizio
cha
bei ya mafuta basi ndiyo itakuwa hadithi. Hivi
wadanganyika
wenzangu mnafikiri bei ya mafuta ikishuka (let's say)
hadi nusu, ndiyo maisha yatakuwa bora kwa kila
mdanganyika?
"Dhahabu imepanda sana bei katika soko la dunia. Kwa
nini vitu kama hivi vimeshindwa kufidia pengo la mafuta
yaliyopanda?
Watu wengine wanafananisha Bongo na Marekani - eti na
Marekani maisha yamepanda. Nyie ndugu zangu hebu acheni
mzaha! Wewe unakula humburg na pizza Macdonald halafu
unatuambia maisha yamepanda? "Chonde chonde jamani.
Natamani mngerudi huku mkapigika mkashindia kauzu ndiyo
mngejua watu wanaongea nini " Ukurasa huu
hautatosha
kukupatia maoni ya kila msomaji, lakini natamani
ungejisomea mwenyewe habari hiyo kisha chini yake usome
maoni ya watu.
Wasaidizi wako wanaweza kukusaidia kutembelea
http://www.freemedia.co.tz/daima/2008/7/21/habari1
Mheshimiwa Rais ningekushauri jambo moja tu. Kukubali pia
ni uungwana wa aina yake na Watanzania wanapenda watu
waungwana.
Baada ya ziara yako ndefu mkoani Tanga, utakaporejea Ikulu
fanya jambo moja tu. Andaa hotuba yako ya mwezi bila
kumshirikisha msaidizi wako yeyote. Ita waandishi wa
habari
kana kwamba unakuja kujibu tu maswali watakayokuuliza
halafu
wakisha fika toa hotuba yako kabla hujaulizwa maswali.
Waeleze wanahabari na Watanzania kwa ujumla kwamba wakati
unachukua fomu za kugombea urais mwaka 2005 hukuijua
vizuri
sababu ya umaskini wa Watanzania. Waeleze kwamba wewe
ulidhani kazi uliyokuwa nayo ni kuwaita tu wawekezaji
uliokuwa umeshazoeana nao sana ukiwa waziri wa Mambo ya
Nje
na Ushirikiano wa Kimataifa, na kwamba wakishakuja
kuwekeza
tayari maisha bora kwa kila Mtanzania yanajipa.
Sema kwamba umekuja kugundua kuwa mambo sivyo yalivyo.
Umaskini wa Watanzania una uhusiano wa karibu mno na
utawala wa nchi. Na kwamba utawala wa nchi kwa miaka
mingi
umebaki kuwa mbovu hasa kupitia 'system'
iliyojengwa na
Chama chako Cha Mapinduzi ya kulindana viongozi, bila
kujali
madhara yanayosababishwa na viongozi mafisadi hapa nchini
na
hivyo hata malaika akiwa rais wa nchi hii kupitia CCM
hakuna
maendeleo yatakayopatikana.
Sema wazi wazi kwamba kama rais wa nchi hata kama ungekuwa
na dhamira ya kuikwamua nchi kutoka kwenye umaskini
unaosababishwa na uongozi mbovu, ungeshindwa kwa kuwa
kikulacho ki nguoni mwako. Maswahiba zako waliofanya juu
chini upate urais ndiyo hao hao mafisadi waliokubuhu hata
jina la mafisadi haliwafai tena. Nasikia wengine wameanza
kuwaita 'mafisidi'.
Na wewe huwezi kuwatupa wakati ungali ukikumbuka mchango
wao mwaka 2005. Kwa sababu hiyo, ili kulinda uhusiano
wako
nao na wakati huo huo kulinda heshima kupita kiasi
uliyopewa na watanzania, umeamua kuachia ngazi na hivyo
mwaka 2010 hutagombea tena.
Wapatie Watanzania nafasi ya kuanza kufikiria tangu sasa
chama kitakachowafaa kuongoza nchi hii hapo 2010,
kutokana
na sera zake kabla hawajafikiria ni nani atawafaa kuwa
rais wa nchi baada yako. Uhakika mmoja tu nakupatia kwamba
hutabaki ulivyo machoni mwa Watanzania.
Najua wapambe wako watakulaumu sana, maana kwa kung'oka
wewe utakuwa umewakosesha ulaji mkubwa. Lakini utakuwa
umejiweka katika nafasi nzuri ya kuwa shujaa mbele ya
Watanzania, kwa kutoboa ukweli na utapumzika kwa amani
baada ya miaka 10 ya kusaka urais na miaka mitano ya
kushutumiwa na Watanzania kwa kutotoa (not delivering)
kile
ulichotarajiwa.
Naamini pensheni itatosha, isipotosha utaongezea kilimo cha
kisasa. Fanya uamuzi sasa ama utakuja kujuta
utakapostaafu.
Watafanya kama walivyomfanyia Chiluba hadi
utashangaa.
Uamuzi ni wako Mheshimiwa Rais