Hujanishawishi aisee...kuna mdau kauuliza swali LA.msingi hapo umemtolea nnje...what kind of marketing unafanya ndugu endapo swasli dogo tu hivyo hujajibu?
Then nyie mmetengeneza mfumo..mnauza likesa and followers wa watu kwa kigezo cha kuwap eti point ?? Yani ninyi mkusanye mamilioni then mumpe mtu tupoint tumoja kwa tangazo litakalofika likes 1000 kweli?
Why msifanye mkawa mnashare na watu hayo mamilioni kwa commission Fulani?
Kama mnapata milioni nyie mnampa kulingana na idadi ya viewer ama likes ..anazowapa hao makampuni.
Hivi umesoma vizuri kweli au umeamua tu kukurupuka? Umesoma hizo point zinatumia kufanya nini? Kumbuka tangazo moja litakuwa shared na watu wengi wenye social media. Na nimesema kabisa kuwa kulingana na share, likes, comments, retweet unapata points ambazo hizo points ndo utatumia ku redeem rewards ambazo inaweza kuwe pesa taslimu au kitu kingine kulingana na kampuni tunazo zifanyia matangazo. Mfano, Clouds tamasha la fiesta hawatataka kutoa hela, badala yake watatoa tickets za fiesta, kampuni ya bia inaweza amua kutoa hela au kreti la bia, Kampuni ya simu inaweza kutaka kutoa vocha au simu au hata bundle, hayo yote itategea na client.
Zawadi zitakuwa zimeorodheshwa zikionyesha points unazohitaji kuredeem kila zawadi. Wewe utachagua unataka kutumia point zako kuchukua zawadi gani kutoka kwenye list.
Kwa kuwa ni watu weni wanashare, unadhani kuna njia gani nyingine ya kushare hayo mamillioni bila kutumia points? Points ambazo unazipata kulingana na share, likes, comments na tweets ulizopata?
Maana huwezi kusema ugawane haya "mamilioni" sawa kwa sawa wakati wengine wameshare sana kuliko wengine, au wengine post zao zimepata likes na comments nyingi kuliko wengine. Njia rahisi ya kuweza kupima na kumpa mtu haki yake ni kutumia huo mfumo.
Kwa watu wenye pages zenye followers wengi, nimesema nitumie pm jina lapage yako, kiasi cha followers na kupata demo, tuma email yako nikutumie invite ya kuingia kwenye demo uone. Lakini siwezi kuku invite wakati hujakidhi vigezo.