Injinia Hersi Said: Timu za Simba na Yanga zinaendeshwa kwa hasara miaka mingi

Naomba kujua wewe ni MANARA?
 
Kuna mahala unafeli bro.

Mwenzako kahoji swali simple tu,ikiwa unadhani kwamba wawekezaji wanapiga hela ndefu kwa matangazo yale na bado wanalialia,kwanini wakiondoka klabu zetu huwa zinaenda kuwabembeleza? Kwanini klabu zisiachane na wawekezaji hao kisha zenyewe zikaanza kujibandikia matangazo yao (bila kutafuta mwekezaji mwingine)?

Sasa badala ya kujibu hoja unaishia kumkejeli mwenzako kwa kumwambia ana akili ndogo,mara sijui amekuwaje.From a psychological viewpoint,wewe ndo una akili ndogo.
 
Marehemu Geroge Mpondela na Marehemu Reginald Mengi walishauri sana Yanga ijiendesha kama kampuni ila wanachama wakagoma wakati kadi hawalipi, michango hawatoi, jezi hawanunui na uwanjani wanataka kuingia bure kupitia wale makomandoo wao.
Wawezekaji kama GSM na MO wanaumia sana, hela ziwatoke na majungu wanapigwa na watu wasiochangia hata mia.
 
Kujibandikia matangazo yao yapi kwa mfano
 
Sio kweli hiyo pesa hata usajili wa msimu tu haitoshi
 
Hivi vilabu vinataka sifa za kijinga tu kwa sababu matumizi yao ni makubwa kuliko mapato na hawana mali zozote za maana.

Tusubiri miaka miwili au mitatu ijayo hivi vilabu vitakuwa vimefirisika kwa sababu havina mapato ya kustahimili mahitaji yao.
Haviwezi kufilisika kwa sababu havina kitu
Vitaendelea hivi hivi, MO au GSM wakiondoka watakuja wengine
 
Point, hao wanawadhihaki wawekezaji, wakijitoa wanajificha kimyaa.
Kwa kudakua huwawezi.
Ndivyo walivyo umbwa.
 
Ashakum si matusi.
Utaumia kichwa kumwelewesha huyo[emoji119] . Achana naye maana anajifanya anajuwa sana. [emoji18]
 
Ukitaka kujua utamu wa ngoma ingia ukacheze. Halafu uje utupe mrejesho. Siyo ku argue bila evidence.
 
Mkuu Che mitonga, nakushauri, achana na huyo atakuumiza kichwa!!
 
Biashara ya mpira ni kama hisani bongo hii. Hakuna "Return on investment" nimeanza kusikia malalamiko haya toka wazamini enzi za kina Gulamali sio Yanga sio Simba.
Fikiria Yanga kufuzu robo Shirikisho atalamba kama 800M kwa mujibu wa vyanzo flani ila kufika hapo kaweka 1B kuendelea. The same problem kwa sasa anayo Katumbi kule Lumbumbashi kwa wale Mamba wa Mazembe na hajafuzu quarter shirikisho na pesa nzuri ipo kimataifa,mirabaha kibao n hisani. Vaa kiatu cha Katumbi kwa sasa afu kaa mezani chukua calculator ufanye hesabu za kibiashara😁
 
GSM sina uhakika, lakini kwa Mo affiliation yake kwa Simba haina mashaka na tangible.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…