Intanet yaanza kusumbua Kenya, NetBlocks yaeleza changamoto inayotokea

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Shirika la Uchunguzi la Mtandao la NetBlocks limethibitisha kuwa Data ya Mtandao ya moja kwa moja inaonyesha kuna usumbufu mkubwa wa muunganisho wa Intaneti Nchini Kenya, ikiwa ni siku moja pia tangu Mamlaka kudai hakutakuwa na kuzimwa kwa Mtandao.

Watumiaji mbalimbali wa Mitandao hasa wa X (zamani Twitter) wameandika kuwa wanalazimika kutumia VPN ili kuendelea kupata uwezo wa kutumia Intaneti

NetBlocks imeeleza changamoto hiyo ya Mtandao inayoendelea inadaiwa pia kuathiri Nchi Jirani zikiwemo Uganda na Burundi, hali hiyo inadaiwa inaweza kupunguza utangazaji wa matukio ya maandamano yanayoendelea
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…