Intelligensia juu ya Mabomu ya Arusha

Watz tuache kulalamika,serikali ya ccm inahusika na ndio maana haitaki kuundwa kwa tume huru kuchunguza matukio haya kwa hofu ya kuumbuliwa.Wasingekuwa wanahusika hiki kigugumizi cha kuunda tume huru ya kijaji/kimahakama yenye watu huru kuchunguza mauaji haya kisingekuwepo.
 
Bahati mbaya sana kuna watu immature wasio na hekima, wanataka kuaminishwa watu hivyo kwa kauli zao. Na kwa namna hiyo hiyo ni makosa kuanza kuwanyooshea vidole nchi jirani au watu fulani bila kuwa na ushahidi dhairi. Kinachochangia hizi speculation ni udhaifu wa vyombo vyetu vya usalama kwa kutofanya uchunguzi haraka na kutoa taarifa kwa umma.

Kwa uongozi bora sasa duniani na mkakati sahihi kupambana na uhalifu wa jinsi hii/ugaidi ni kuhakikisha tuna vyombo imara vya uchunguzi na kila hatua ya uchunguzi itolewe kwa watu ili kuzuia upotoshaji. Lakini si Upotoshaji tu bali kutoa taarifa za kina na sahihi zinasaidia kuwaogopesha waalifu/magaidi kutenda uhalifu/ugaidi wao.

Tuliona mwaka jana huko Boston Marekani walipopata dhahama kwenye mbio za marathon jinsi uchunguzi na taarifa zilivyokuwa zikitolewa kwa umma. Sisi hapa kwetu kauli za polisi na viongozi kila baada ya tukio zinajirudia na huitaji hatakusikiliza kwa sababu unajua kitakachotamkwa.
 
Gud analysis ila umeharibu uliposema Kenya sijui hawakupendezwa na nn sjui, wao huko kwao hapakaliki kwa mabomu ya alshabab then waje waanze kuhangaika na sisi hapana mimi ntakua wa mwisho kuliamini hilo
 
Sidhani kama ni sahihi kusema CCM wanajua. Kauli hii ina maana secretariat, Kamati kuu au halmashauri ya taifa wajumbe wake wote pamoja au kikundi chao wanahusika. Haiwezekani kuwepo kitu kama hicho. Halikadhalika si sahihi kwa wale wanaofikiria ni vyama vya upinzani. Bali ninafikiria ni kikundi au watu fulani ambao wana malengo mabaya wanafanya haya kwa kutumia udhaifu uliopo.
 
Kofia ya kichina ya Mwigulu Nchemba ina uhusiano mkubwa na milipuko ya mabomu
 
Kenya should be condemned for such barbaric acts towards our national peace and security, we have all the rights to retaliate, of which according to the current threesome security pact its allies may join forces, I smell a regional war!
 

Swali lingine ni kwamba hao magaidi walipue mikutano ya CHADEMA tu, wakati hata CCM wana mikutano maeneo hayo hayo? Kumbuka NAPE na MWIGULU walitangulia kuonya juu ya hatari ya kutokea maafa kwenye mikutano ya CHADEMA, hivyo kuwataka wananchi waende kwenye mikutano ya CCM kwani huko ni salama.

Aidha, kipindi kama hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu mwaka 2005 media za serikali na chama cha CCM ziliendesha programu za kurusha machafuko ya Burundi,DRC na Rwanda ili kuwatisha wananchi kwamba vyama pinzani vitaleta vita vya wenyewe kwa wenyewe na machafuko nchini.

Milipuko hii ni janja ya mafisadi na CCM yao. Hakuna ugaidi hapo.
 

Usiwe mvivu wa kufikiri. kama kweli ni majirani kwa nini polisi walimkamata mwendesha bodaboda (Ambrosi)
 
Wakenya wanaumia kuwa Tanzania inainuka kwa kasi. Mabomu haya yote ni yao, Arusha vs Nairobi, and Zanzibar vs Malindi in tourism.
Kenya is our TOP ENEMY!
 
Watanzania wa leo sio wakulazimishwa kuamini kile unachokiamini. Dunia ya leo ni kuchukua habari na kuifanyia kazi hili kuona kuna ukweli au la.

Mimi bado na imani kubwa sana na idara zote za ulinzi na usalama hapa Tanzania. Yote haya yataisha na wausika watajulikana siku moja tu.

Mungu ibariki Tanzania na watu wake.
 
Wakenya wanaumia kuwa Tanzania inainuka kwa kasi. Mabomu haya yote ni yao, Arusha vs Nairobi, and Zanzibar vs Malindi in tourism.
Kenya is our TOP ENEMY!
Mkuu wangu nimekuuliza kama wanao choma makanisa,biashara za Watanganyika na kuua Mapadri huko Zanzibar ni Wakenya bado hujajibu!! Bado nakuuliza nakuuliza hao ni Wakenya?
 
ili kuteka soko la mboga mboga na maua toka Arusha, Wakenya walianza ku delay flight za ndege zilizokuwa zimebeba bidhaa hizo toka Arusha ili ziharibike, na zikataliwe na hivyo tupoteze soko walikamate wao....Kuna anaye jiuliza ni kwanini SHOPRITE imefilisika na sasa biashara wanauziwa NAKUMAT ya Kenya???....
 
Kwanini kiongozi wa chama cha siasa avae kijeshi kombati na kofia yenye nembo ya jeshi la nchi fulani? Huyu anatoa meseji fulani kuna kitu anakijua na anaipenda nchi yake.
 
Tatizo la mabomu halihusiani na udhaifu wa serikali, kwani mabomu yanalipuliwa hata Marekani, Uingereza na kwingineko ambako usalama ni imara, usipotoshe hoja ya mtoa mada
 
Milipuko ya mabomu ni kitu sensitive sana kwa usalama wa nchi, kitu cha kujiuliza ni kwa nini serikali ilikataa kuunda tume?
 
Unashindwa kuelewe kitu gani kujua mahusiano ya Arusha na Vivutio vya Utalii kama Serengeti,Ngorongoro,Kilimanjaro,nk? Hii elimu duni inasababisha watu wavivu kufikiri.

Mbona wakati anazungumzia mauaji ya mpeketoni na Nairobi hakutaja habari za masaimara, utalii na huduma za bandari kuwa na uwezekano wa kuathiriwa na mabomu? kwanini iwe serengeti na mabomu? kuwa paranoid ni muhimu maishani kwa usalama wa mtu na mali zake. Nahisi wewe ni Mkenya
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…