Internet service provider

Internet service provider

unajibu kwa busara sana... Jitahidi hivo hivo si unajua tena watu na fake ID zao...
sasa vp na kuhusu mikoani eg.kanda ya ziwa kuna ela sana coz migodi mingi kwanini usipeleke na huko wapate huduma...
Kiongozi upo mkoa gan??
 
Scars package tutakubaliana na mteja, anataka speed gan? Na matumizi yake yapoje? Mfano anataka kwaajili ya home kucheki movie, kuperuzi, na matumiz ya smartphone kawaida. Atapewa speed inayoendana na matumizi yake kwa bei rafiki na nafuu sana
Mi nafikiri nyie suppliers ndio mnakuwa tayari mmeshapanga kila kitu pamoja na bei yake kisha mteja anajichagulia kulingana na uwezo wake.

Nyie ndio mnapanga packages kulingana na aina ya huduma zenu (labda ni dedicated) na hivyo vifurushi vyenu mkaamua kuviuza kwa bei ambayo nyinyi mmekaa chini na kupiga hesabu na kuona itawalipa.

Sasa kusema bei yenu nimakubaliano na mteja maana yake upo uwezekano wa mtu kuweza kulipa kifurushi gharama tofauti kubwa wakati kifurushi hicho hicho kuna mwingine analipia kwa gharama ya chini kwasababu mwingine hakukaza kwenye makubaliano.
 
Mi nafikiri nyie suppliers ndio mnakuwa tayari mmeshapanga kila kitu pamoja na bei yake kisha mteja anajichagulia kulingana na uwezo wake.

Nyie ndio mnapanga packages kulingana na aina ya huduma zenu (labda ni dedicated) na hivyo vifurushi vyenu mkaamua kuviuza kwa bei ambayo nyinyi mmekaa chini na kupiga hesabu na kuona itawalipa.

Sasa kusema bei yenu nimakubaliano na mteja maana yake upo uwezekano wa mtu kuweza kulipa kifurushi gharama tofauti kubwa wakati kifurushi hicho hicho kuna mwingine analipia kwa gharama ya chini kwasababu mwingine hakukaza kwenye makubaliano.
Ok. Ni kweli kabisa lakn unapofanya mpangilio wa bajet kumbuka kuna watumiaji ambao asubuhi mpaka jioni hayupo nyumbani. Wapo watoto tu. Matumizi yake yanakuwa ya kawaida sana. Ni bora bei kuwa rafiki ili mteja aweze kufanya malipo vizuri kila mwezi..karibu kwa maoni kiongozi ningependa kufahamu unapatikana wapi hapa dar es salaam
 
Basi huu uzi hautakuwa na maana yoyote kama unaotutarajia kuwa wateja wako tunafichwa gharama za vifurushi vyenu.
Hapana scars nitaleta brochures soon zitakavyokuwa tayari zimeandaliwa.
 
Ok. Ni kweli kabisa lakn unapofanya mpangilio wa bajet kumbuka kuna watumiaji ambao asubuhi mpaka jioni hayupo nyumbani. Wapo watoto tu. Matumizi yake yanakuwa ya kawaida sana. Ni bora bei kuwa rafiki ili mteja aweze kufanya malipo vizuri kila mwezi..karibu kwa maoni kiongozi ningependa kufahamu unapatikana wapi hapa dar es salaam
Mkuu sisi tunatambua kuwa gharama za internet za fiber au unlimited yeyote haitozwi kwa aina ya matumizi yako.

Hii sio kama DAWASCO kwamba matumizi yako yakiwa madogo basi utegemee bili ndogo mwisho wa mwezi.

Na mwezi ambao hujatumia kabisa maji basi hautalipia.

Kwenye unlimited plan swala la mtu kutotumia internet haliwezi kuwa excuse ya kutolipia gharama zilizoorodheshwa kwenye mkataba.

Mtu mpaka anachukua package ya 50K kwa mwezi maana yake swala la yeye kutotumia haliwezi kuwahusu nyinyi.

Labda ashindwe kutumia kwasababu ya miundombinu yenu ime corrupt, yani nyie ndio muwe sababu za yeye kushindwa kupata internet.
 
Mkuu sisi tunatambua kuwa gharama za internet za fiber au unlimited yeyote haitozwi kwa aina ya matumizi yako.

Hii sio kama DAWASCO kwamba matumizi yako yakiwa madogo basi utegemee bili ndogo mwisho wa mwezi.

Na mwezi ambao hujatumia kabisa maji basi hautalipia.

Kwenye unlimited plan swala la mtu kutotumia internet haliwezi kuwa excuse ya kutolipia gharama zilizoorodheshwa kwenye mkataba.

Mtu mpaka anachukua package ya 50K kwa mwezi maana yake swala la yeye kutotumia haliwezi kuwahusu nyinyi.

Labda ashindwe kutumia kwasababu ya miundombinu yenu ime corrupt, yani nyie ndio muwe sababu za yeye kushindwa kupata internet.
Shukrani kwa ushauri wako mkuu scars, tumeyapokea na tutalifanyia kazi, soon nitaleta packages zetu hapa.
 
Haujakomaa kwenye Marketing ndugu, naona unazunguka zunguka tu bila mpango unashindwa kukaa panapotakiwa. Iko hivi, kwa maisha ya sasa Umeme na Internet na gari ni vitu vya msingi sana katika maisha ya mwanadamu mwenye akili timamu.

Unaulizwa kuhusu bei unakaa kututia saundi tu, umelileta huku kufanya nin ikiwa hamjui mnataka mhudumu kwa bei kiasi gani angalau hata nakisi tu ya bei?
 
Haujakomaa kwenye Marketing ndugu, naona unazunguka zunguka tu bila mpango unashindwa kukaa panapotakiwa. Iko hivi, kwa maisha ya sasa Umeme na Internet na gari ni vitu vya msingi sana katika maisha ya mwanadamu mwenye akili timamu.

Unaulizwa kuhusu bei unakaa kututia saundi tu, umelileta huku kufanya nin ikiwa hamjui mnataka mhudumu kwa bei kiasi gani angalau hata nakisi tu ya bei?
Sawa kiongozi, naleta bei za vifurushi
 
Habari wana jukwaa. Natangaza huduma ya mtandao majumbani na maofisini kwa vifurushi nafuu kabisa. Huduma hii itaanza kuanzia mwezi wa 10 mwishoni mara tu baaada ya kukamilisha vibali vya serikali.
Walengwa ni kama ifuatavyo-Majumbani, Maofisini, Stationery, Pharmacy.

Maeneo ambayo tayari miundo mbinu imefika.: Tegeta, Mbweni, Makumbusho, Kinondoni, Kijitonyama, Mwananyamala, Mikocheni, Kawe, Sinza, Magomeni, Msasani, Masaki, Morroco, Mwenge, Makongo juu...

Tafadhari karibu kwa maulizo na maombi na utaje sehemu uliyopo. Kauli mbiu yetu mteja ni dhahabu kwetu. Ahsante.
Wote mnakimbilia maeneo ya kisure kugombea wateja,njooni na uswazi huku kuna watumiaji wa internet wengi tu
 
Kiluvya, kibamba, Gogoni, Mloganzila mtafika?
 
Back
Top Bottom