iPhone ni kama gereza la kifahari. Ni kwajili ya fasheni tu, hutaweza kufanya vitu muhimu vifuatavyo...

biashara mkuu. watu hawafiki bei na mashart tu.
 
kitu gani apple analeta kipya na cha kipekee, zaidi ya kurudia walikotoka wenzie na kuboresha.

ultrasonic fingerprint hajaweka leo utashangaa 2023 ndio anawekea wateja wake.
 
Ukinunua flagships za Android, specs zinafanana almost zote. Wanachoweza kuongeza ni 'skins' kwenye Android.

Lakini apple anaweza akakuletea kitu chake pekee.
Huku android kila kitu kipo, huko apple no rahisi kuongezea vitu kwa kuwaiga android, mfano apple anaweza kuongeza radio kama android, kuruhusu kuweka default app, n.k.

Pia iphone kanunua processor zake kwa matoleo mengi tu ya iPhone,
 
Ha ha ha ha ha mke wang huyo[emoji1787] nlimpata baaday ya yey kuniona natumia iphone[emoji38][emoji38][emoji38]
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Sasa huyu jamaa anapata wapi Nguvu ya kuiponda iphone??? Pisi moja makini...msalimie mzee
 
Hapa Bongo kuna watu wanamiliki simu tena smart phone lakini hata kudownload whatsap hawezi na tena wengi wao wakiwa masister du
 
Huku android kila kitu kipo, huko apple no rahisi kuongezea vitu kwa kuwaiga android, mfano apple anaweza kuongeza radio kama android, kuruhusu kuweka default app, n.k.

Pia iphone kanunua processor zake kwa matoleo mengi tu ya iPhone,

Apple ndiyo the largest company by market cap dunia nzima. Apple ndiyo the most valuable company on planet. Hakuna kampuni duniani ambayo inaweza kuuzwa kwa bei ghali kama apple. Mnapokuja na vi android vyenu tembeleeni page za stocks and money.
 
Apple ndiyo the largest company by market cap dunia nzima. Apple ndiyo the most valuable company on planet. Hakuna kampuni duniani ambayo inaweza kuuzwa kwa bei ghali kama apple. Mnapokuja na vi android vyenu tembeleeni page za stocks and money.

iPhone ambae ni monopoly kwenye industry ya iphones, Kwa vile ni monopoly hata bei hazi affect elasticity of demand inabaki kuwa ine astic

Android ni industry yenye firms nyingi sana kama Samsung, Huawei, Motorola, One plus one, Sony, Nokia, Lenovo Xiamoni n.k.

Industry ya android ina thamani mno kuliko industry ya iPhones. Naomba kabla hujaja ku comment uwe na uelewa wa indsustry na firms, Kwa vile huku hakuna monopoly hata demand inakuwa elastic sana ila over rall industry inabaki kuwa juu.

Kwa hio kabla hujakurupuka ni vyema ukijua ni wazi kabisa industry ya android ukiunganisha kampuni zote ni ghali kuliko industry ya ios ya iPhone.

Pia linapokuja swala la Market Share Iphone anashika namba 4, akipitwa na simu kama samsung, huawei na nyingine

Kwa mujibu wa ripoti ya Idc kampuni hizi ndio zimeteka soko

1.Samsung - 21.2 %
2. Huawei - 17.8%
3. Apple - 13%
4. Vivo - 9%
5. Others (mostly android os) - 28%
 
Main point hapo ni kwamba inabidi upitie pirika pirika nyingi ili uweze kufanya kitu ambacho kwa android kipo tayari, Ama kweli Iphone ni Tatizo.....
 
Kuna watu iPhone ni mkombozi wao kwa ulinzi wa data. Kama unaona iPhone inakubana sana basi sio level yako maana kila kitu ni ghali na very limited.
Usalama wa data ( ulinzi ) , unategemea na mtumiaji na matumizi yake. Hata android ipo salama pia. Nakumbuka kipindi nafanya certification zangu cyber, wadau walikuwa wanasema window haina usalama compare to ubuntu.. nikawa naambai haya nendeni mka hack hiyo windo iliyo nyepesi
 
Mkuu afadhali umenisaidia kusema la moyoni, kiukweli kabisa na tatizo la kujieleza ila kwa maelezo yako umesema nilicho kuwa na tamani kueleza. Kiufupi Iphone ni kama urembo tu hauezi customise wala haina features nyingi kama android, wanacho tusumbua nacho zaidi labda security kwa hilo.kweli wako vizuri ila ipo siku na amini android wata kuwa na udhibiti mkali kama iphone.
 
Tunapozungumzia usalama ndio iPhone ni salama lakini pia android nayo ina ukuta wa ulinzi (sio pazia), Hapa ni kama darasani iPhone ma android wanapewa mtihani iPhone anapata 90% android anapata 80% na wote wana alama ya A.

ila kwa iPhone security wameikaza kiasi hata mtumiaji anakosa raha ya uhuru wa kawaida, inakuwa kama mtoto wa geti kali yupo salama ila yupo ndani mda wote hata kupata furaha kwa kujichanganya na wenzie nje hana.

iphone ilishawahi kudukuliwa na picha kibao zilivujishwa za watu maarufu za uchi. Pia hata mapolisi walimkamata gaidi marekani walifanikiwa kuivunja hio iphone ndanibya mda mfupi tu, licha ya kampuni ya iPhone kukataa kuwapa msaada polisi ila walifanikiwa.

Kwa hapa kwetu bongo hata simu ya kitochi ukiweka pincode upo salama maama hata wasomo wa IT wengi ni wa kufaulu kwenye vueti sio ujuzi, IT wengine wanamaliza vyuo hata kupiga window hawajui ila vyeti viko fresh sasa huyu atamtishia nani usalama wake wa simu 😁😁.

Haya mambo ya ulinzi kwa hapa bongo naona ukiweka ulinzi wa kuchora pattern au kuingiza pincode ushamaliza mchezo na wala sijawahi kusikia mtu akilalamika hapa bongo mambo ya kudukuliwa simu yake kama aliweka pin au pattern.

Hata wasanii kibao wanaolalamika instagram zao zimedukuliwa huwa wanatumia iPhone ila kwasababu ya uzembe wao, majangili hawanaga hata haja ya kushika simu zao ili wadukue account zao za insta

Mtaalam aliebobea mambo ya security anadukua chochote anachotaka na hakuna wa kumzuia maana hakunaga system ambayo ina usalama 100% na ndio maana hata apple walipokataa kutoa ushirikiano kwenye kuivunja system ya gaidi mwenye iphone kuna wataalam waliweza kuivunja.
 
anayesifu apple kwa minajirj ya ulinzi nchi za africa hajitambui. au ndio ule ule ushamba wa kukielezea kitu kwa mkumbo.

mtu unakuta ana iphone 6 leo 2020,na bado anakwambia aisee apple ni balaa, wakati hizo android tukitia pascode tu, data zimefika pahala pake. data zenyewe picha za selfie[emoji38][emoji38].
 
biashara mkuu. watu hawafiki bei na mashart tu.
Kumbuka iPhone inabeba 60% ya faida kwenye biashara ya smartphone ulimwenguni. Hiyo 40% ndo wengine wote waliobaki wanaigombania.

Kwahiyo kwa CEO wa Apple, hataona incentive yeyote ya kuruhusu kampuni nyingine watumie iOS.

Apple wana ecosystem ambayo ipo complex sana. Kampuni ingine haiwezi kuaccess hiyo ecosystem kienyeji tu.
 
Huku android kila kitu kipo, huko apple no rahisi kuongezea vitu kwa kuwaiga android, mfano apple anaweza kuongeza radio kama android, kuruhusu kuweka default app, n.k.

Pia iphone kanunua processor zake kwa matoleo mengi tu ya iPhone,
Apple wanaweka kitu na kukitoa kukiwa na sababu maalumu. Hawafuati mkumbo kama watu wa Android. Sioni utofauti wowote wa simu za Android labda 'skins' zinazowekwa juu ya Android OS.

Teknolojia inakua sana, kuna baadhi ya vitu huwa haviwekwi kwasababu vimeshapitwa na wakati. Mfano, headphone jack. Hata mimi sioni faida yake tena.

Sasahivi kuna wireless charging, hakuna haja ya kutembea na miwaya tena wakati almost vitu vinavyozalishwa sasa vinaendana na tech iliopo. Mfano, kuna magari yana sehemu za kuchajia simu wirelessly. Kwahiyo usishangae iphone 12 au 13 wataondoa sehemu ya kuchaji, mtachaji simu zenu wirelessly.
 
wenzie wanagombania 40 sababu yeye hawekezi katka research na kutumia pesa nyingi. ndio sababu anakuwa mtu wa kurudia vilivyokwisha fanyika tayari.

halafu swala la kutumia software sio la kuiiba, ni mapatano na makubaliano ya biashara. tokea kampuni inaanzishwa jobs alikiri wazi kwamba,kama unataka kuwa serious kwenye ulimwengu huo tengeneza software na hardware mwenyewe. so kinachofanya apple wasigawe patents kwa wadau ni hiyo woga ya kutoamini ubora wa vifaa kutoka eneo lingine, wakafunga milando ya ofa.

lakini kama ilivyo ada, tech ndio inaamua, leo hii apple wanatengeneza simu kubwa(haukua msimamo wao),wana line mbili(haukua msimamo wao). hatujui mbeleni itakuwaje.
 
Hizo kampuni mbili zinauza hadi low range phones including zile features phones.

Iphone atakupa flagship moja yenye basic na pro model, baada ya miezi 6 atakupa mid range yake.

Kwahiyo almost model 3 au 4 tu.

Mfano mwaka jana, apple ametoa iphone 11, iphone 11 pro na iphone 11 pro max. Mwezi wa 6 akakupa mid range yake ambayo wanatumia chip za hizo flagships.

Njoo kwa Samsung sasa. Ana S20 flagship series, Note Series, A series, J series, M series. Na nyingine nisizozifahamu. Anaweza akatoa hata models 30 tofauti kwa mwaka mmoja ila apple anakupa model 4.

Kwahiyo sishangai Samsung na Huawei kufanya vizuri interms of unit sold ila kwenye net profit, Apple amebeba 60% ya faida ya smartphone market.
 
Mkuu ume elezea vizuri sana na kitaalam ila point hapa je iphone ni user friendly kama ilivyo android ambayo una weza customize to your preferences stil una pata variaty of applications toka play store na sehemu zingine kibao? Jibu ni NO. Iphone kama ulivyo kwisha eleze wameifunga mno mpka imekosa taste ina baki kuwa ya fashion kupiga simu na kutuma insta chats ila kwa ladha ya apps tofauti kwa iphone huwezi enjoy kitu iko so limited.
Tuendele kupeana mawazo tofauti plz
 
hiyo sababu huwa haipo, wao ndio huileta. rejea msimamo wao katika innovation. wanasema(usimpe mteja kitu bila kumwelekeza matumizi) ndio atajua thamani yake.

kuiacha wireless pekee ktk simu utakuwa ni zaidi ya ubabe,wengine hawakumuiga katka earphone jack maana waliona ni upuuzi, yeye anafanya kwa ustawi wa biashara zake(auze earpods), wengine wanafanya kumtizama na mteja pia.

japo ni mpango huo wa kuondoa kabisa matundu kwenye simu, ila wataahirisha wafanye kama kwenye earphone jack 2 options, maana wajuba ukizingua wanakuacha na upuuzi wako.
 
apple anakuja huku bro, soko ni pumbavu sana.mwaka jana mizigo hiyo sokoni. mwaka huu hatujapoa tumepigwa iphone se2. kabla october hatujapewa packege ya kutosha.

ukijifanya premium, watu wanakaba premium mpaka garbage products[emoji38][emoji38].
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…